< Psalms 6 >
1 To the chief Musician on Neginoth upon Sheminith, A Psalm of David. O LORD, rebuke me not in thy anger, neither chasten me in thy hot displeasure.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Have mercy upon me, O LORD; for I [am] weak: O LORD, heal me; for my bones are agitated.
Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 My soul is also greatly disquieted: but thou, O LORD, how long?
Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
4 Return, O LORD, deliver my soul: Oh save me for thy mercies sake.
Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 For in death [there is] no remembrance of thee: in the grave who will give thee thanks? (Sheol )
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol )
6 I am weary with my groaning; all the night I make my bed to swim; I water my couch with my tears.
Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
7 My eye is consumed because of grief; it groweth old because of all my enemies.
Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Depart from me, all ye workers of iniquity; for the LORD hath heard the voice of my weeping.
Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 The LORD hath heard my supplication; the LORD will receive my prayer.
Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
10 Let all my enemies be ashamed and greatly disquieted: let them return [and] be suddenly ashamed.
Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.