< Psalms 46 >

1 To the chief Musician for the sons of Korah, A Song upon Alamoth. God [is] our refuge and strength, a very present help in trouble.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Therefore will we not fear, though the earth shall be removed, and though the mountains shall be carried into the midst of the sea;
Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
3 [Though] its waters shall roar [and] be disturbed, [though] the mountains shake with the swelling of it. (Selah)
Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
4 [There is] a river, the streams of which shall make glad the city of God, the holy [place] of the tabernacles of the Most High.
Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
5 God [is] in the midst of her; she shall not be moved: God shall help her, [and that] right early.
Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 The heathen raged, the kingdoms were moved: he uttered his voice, the earth melted.
Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
7 The LORD of hosts [is] with us; the God of Jacob [is] our refuge. (Selah)
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Come, behold the works of the LORD, what desolations he hath made in the earth.
Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 He maketh wars to cease to the end of the earth; he breaketh the bow, and cutteth the spear asunder; he burneth the chariot in the fire.
Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
10 Be still, and know that I [am] God: I will be exalted among the heathen, I will be exalted in the earth.
“Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
11 The LORD of hosts [is] with us; the God of Jacob [is] our refuge. (Selah)
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

< Psalms 46 >