< Psalms 4 >

1 To the chief Musician on Neginoth, A Psalm of David. Hear me when I call, O God of my righteousness: thou hast enlarged me [when I was] in distress; have mercy upon me, and hear my prayer.
Unijibu nikuitapo, Mungu wa haki yangu; uniokoe niwapo katika hatari. Unihurumie na usikie maombi yangu.
2 O ye sons of men, how long [will ye turn] my glory into shame? [how long] will ye love vanity, [and] seek after falsehood? (Selah)
Ninyi watu, mpaka lini mtaiabisha heshima yangu? Mpaka lini mtaendelea kupenda kile kisicho stahili na kutafuta uongo?
3 But know that the LORD hath set apart him that is godly for himself: the LORD will hear when I call to him.
Lakini mjue ya kuwa Yahweh huchagua watu wa kimungu kwa ajili yake. Nitakapo mwita Yahwe atasikia.
4 Stand in awe, and sin not: commune with your own heart upon your bed, and be still. (Selah)
Tetemekeni na kuogopa, lakini msitende dhambi! Tafakarini mioyoni mwenu kwenye vitanda vyenu na muwe kimya.
5 Offer the sacrifices of righteousness, and put your trust in the LORD.
Toeni matoleo ya haki na muweke imani yenu katika Yahweh.
6 [There are] many that say, Who will show us [any] good? LORD, lift thou upon us the light of thy countenance.
Wengi husema, “Ni nani atakaye tuonyesha chochote kilicho kizuri?” Yahweh, utuangazie nuru ya uso wako.
7 Thou hast put gladness in my heart, more than in the time [when] their corn and their wine increased.
Umeupa moyo wangu furaha kuu kuliko wao wanapozidishiwa nafaka na divai mpaya.
8 I will both lay me down in peace, and sleep; for thou only, LORD, makest me dwell in safety.
Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa.

< Psalms 4 >