< Psalms 137 >
1 By the rivers of Babylon, there we sat down, yes, we wept, when we remembered Zion.
Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
2 We hung our harps upon the willows in the midst of it.
Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
3 For there they that carried us away captive required of us a song; and they that wasted us [required of us] mirth, [saying], Sing us [one] of the songs of Zion.
Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 How shall we sing the LORD'S song in a foreign land?
Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
5 If I forget thee, O Jerusalem, let my right hand forget [her skill].
Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6 If I do not remember thee, let my tongue cleave to the roof of my mouth; if I prefer not Jerusalem above my chief joy.
Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
7 Remember, O LORD, the children of Edom in the day of Jerusalem; who said, Raze [it], raze [it], [even] to its foundation.
Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
8 O daughter of Babylon, who art to be destroyed; happy [shall he be], that rewardeth thee as thou hast served us.
Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
9 Happy [shall he be], that taketh and dasheth thy little ones against the stones.
Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.