< Psalms 114 >

1 When Israel went out of Egypt, the house of Jacob from a people of a foreign language;
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Judah was his sanctuary, [and] Israel his dominion.
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 The sea saw [it], and fled: Jordan was driven back.
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 The mountains skipped like rams, [and] the little hills like lambs.
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 What [ailed] thee, O thou sea, that thou fleddest? thou Jordan, [that] thou wast driven back?
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 Ye mountains, [that] ye skipped like rams; [and] ye little hills, like lambs?
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Tremble, thou earth, at the presence of the LORD, at the presence of the God of Jacob;
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 Who turned the rock [into] a standing water, the flint into a fountain of waters.
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

< Psalms 114 >