< Proverbs 9 >

1 Wisdom hath built her house, she hath hewn out her seven pillars:
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo saba kutoka katika miamba.
2 She hath killed her beasts; she hath mingled her wine; she hath also furnished her table.
Ameandaa wanyama wake kwa chakula cha usiku; ameichanganya divai yake; na kuandaa meza yake.
3 She hath sent forth her maidens: she crieth upon the highest places of the city,
Amewatuma watumishi wake kupeleka mialiko na kutoka mahali pa juu sana kwenye mji anaita:
4 Whoever [is] simple, let him turn in hither: [as for] him that wanteth understanding, she saith to him,
“Wale wasiofunzwa waje hapa!” anawaambia wale wasionaufahamu.
5 Come, eat of my bread, and drink of the wine [which] I have mingled.
Njoo, ule chakula, na unywe divai nimeshaichanganya.
6 Forsake the foolish, and live; and go in the way of understanding.
Acheni njia zenu za kijinga, na mkaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 He that reproveth a scorner, getteth to himself shame: and he that rebuketh a wicked [man getteth] himself a blot.
Yeyote amrekebishaye mwenye dhihaka hukaribisha matusi na yeyote anayemshutumu mtu mbaya atapata madhara.
8 Reprove not a scorner, lest he shall hate thee: rebuke a wise man, and he will love thee.
Usimshutumu mwenye dhihaka, ama atakuchukia; mshutumu mtu mwenye busara, naye atakupenda.
9 Give [instruction] to a wise [man], and he will be yet wiser: teach a just [man], and he will increase in learning.
Mpe mafundisho mtu mwenye busara, naye atakuwa na busara zaidi; mfundishe mtu mwenye haki, naye ataongeza elimu.
10 The fear of the LORD [is] the beginning of wisdom: and the knowledge of the holy [is] understanding.
Hofu ya Mungu ni chanzo cha hekima na maarifa ya Mtakatifu ni ufahamu.
11 For by me thy days shall be multiplied, and the years of thy life shall be increased.
Maana kwa njia yangu siku zako zitazidishwa na uzima wako utaongezewa miaka.
12 If thou art wise, thou shalt be wise for thyself: but [if] thou scornest, thou alone shalt bear [it].
Kama unahekima, unahekima kwako mwenyewe, lakini ukidharau, utaibeba peke yako.
13 A foolish woman [is] clamorous: [she is] simple, and knoweth nothing.
Mwanamke mpumbavu anakelele nyingi- hajafunzwa wala haelewi chochote.
14 For she sitteth at the door of her house, on a seat in the high places of the city,
Anakaa kwenye mlango wa nyumba yake, kwenye kiti cha sehemu ya juu sana ya mji.
15 To call passengers who go right on their ways:
Anawaita kwa sauti wanaopita karibu, watu wale wanaotembea wima katika njia zao.
16 Whoever [is] simple, let him turn in hither: and [as for] him that wanteth understanding, she saith to him,
Wale ambao hamjafunzwa njoni hapa ndani!” anawaambia wale wasio na akili. “
17 Stolen waters are sweet, and bread [eaten] in secret is pleasant.
Maji ya kuiba ni matamu na mkate unaoliwa kwa siri unapendeza.”
18 But he knoweth not that the dead [are] there; [and that] her guests [are] in the depths of hell. (Sheol h7585)
Lakini hajui kwamba wafu wapo pale, wageni wake wapo kwenye vina vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbs 9 >