< Proverbs 13 >

1 A wise son [heareth] his father's instruction: but a scorner heareth not rebuke.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 A man shall eat good by the fruit of [his] mouth: but the soul of the transgressors [shall eat] violence.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 He that keepeth his mouth keepeth his life: [but] he that openeth wide his lips shall have destruction.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 The soul of the sluggard desireth, and [hath] nothing: but the soul of the diligent shall be made fat.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 A righteous [man] hateth lying: but a wicked [man] is lothsome, and cometh to shame.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 Righteousness keepeth [him that is] upright in the way: but wickedness overthroweth the sinner.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 There is that maketh himself rich, yet [hath] nothing: [there is] that maketh himself poor, yet [hath] great riches.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 The ransom of a man's life [is] his riches: but the poor heareth not rebuke.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 The light of the righteous rejoiceth: but the lamp of the wicked shall be extinguished.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 Only by pride cometh contention: but with the well-advised [is] wisdom.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 Wealth [gotten] by vanity shall be diminished: but he that gathereth by labor shall increase.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 Hope deferred maketh the heart sick: but [when] the desire cometh, [it is] a tree of life.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 Whoever despiseth the word shall be destroyed: but he that feareth the commandment shall be rewarded.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 The law of the wise [is] a fountain of life, to depart from the snares of death.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 Good understanding giveth favor: but the way of transgressors [is] hard.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Every prudent [man] dealeth with knowledge: but a fool layeth open [his] folly.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 A wicked messenger falleth into mischief: but a faithful embassador [is] health.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 Poverty and shame [shall be to] him that refuseth instruction: but he that regardeth reproof shall be honored.
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 The desire accomplished is sweet to the soul: but [it is] abomination to fools to depart from evil.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 He that walketh with wise [men] shall be wise: but a companion of fools shall be destroyed.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 Evil pursueth sinners: but to the righteous good shall be repaid.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 A good [man] leaveth an inheritance to his children's children: and the wealth of the sinner [is] laid up for the just.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 Much food [is in] the tillage of the poor: but there is [that is] destroyed for want of judgment.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 He that spareth his rod hateth his son: but he that loveth him chasteneth him betimes.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 The righteous eateth to the satisfying of his soul: but the belly of the wicked shall want.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.

< Proverbs 13 >