< Numbers 4 >

1 And the LORD spoke to Moses and to Aaron, saying,
BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
2 Take the sum of the sons of Kohath from among the sons of Levi, after their families, by the house of their fathers;
Fanya sensa ya uzao waume wa Kohathi kutoka kwa Walawi, kwa kufuata jamaa na na familia za koo.
3 From thirty years old and upward, even until fifty years old, all that enter into the host, to do the work in the tabernacle of the congregation.
Uwahesabu wanaume ambao wana umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Hawa wataungana na kundi linalotumika kutoa huduma kwenye hema ya kukutania.
4 This [shall be] the service of the sons of Kohath in the tabernacle of the congregation, [about] the most holy things.
Uzao wa Kohathi watalinda vile vitu vitakatifu zaidi vilivyohifadhiwa kwa ajili yangu katika hema ya kukutania.
5 And when the camp moveth forward, Aaron shall come, and his sons, and they shall take down the covering vail, and cover the ark of testimony with it:
Wakati kambi inapojiandaa kusonga mbele, Haruni na wanawe lazima waende hemani, kulishusha pazia linalotenganisha mahali patakatifu na kulifunika sanduku la ushuhuda kwa pazia hilo. Watalifunika hilo sanduku kwa ngozi za pomboo.
6 And shall put on it the covering of badgers' skins, and shall spread over [it] a cloth wholly of blue, and shall put in the staffs of it.
Watatandika juu yake nguo za rangi ya samawi. Watachomeka hiyo miti ya kubebea.
7 And upon the table of show-bread they shall spread a cloth of blue, and put on it the dishes, and the spoons, and the bowls, and covers to cover with: and the continual bread shall be upon it.
Watatandika nguo ya rangi ya samawi kwenye meza ya mikate ya wonyesho. Juu yake wataweka sahani, vijiko, mabakuli na vikombe vya kumiminia. Mikate itakuwepo daima mezani.
8 And they shall spread upon them a cloth of scarlet, and cover the same with a covering of badgers' skins, and shall put in the staffs of it.
Wataifunika na nguo ya rangi nyekundu na ngozi za pomboo. na kuweka miti ya kubebea.
9 And they shall take a cloth of blue, and cover the candlestick of the light, and its lamps, and its tongs, and its snuff-dishes, and all its oil vessels, with which they minister to it:
Watachukua nguo ya rangi ya samawi na kukifunika kinara, pamoja na taa zake, na koleo zake, na sahani zake na vikombe vyake vya kuwekea mafuta ya taa.
10 And they shall put it, and all its vessels, within a covering of badgers' skins, and shall put [it] upon a bar.
Wataweka kinara na vifaa vyake vikiwa vimefunikwa na ngozi ya pomboo, na wataweka kwenye miti ya kukibebea.
11 And upon the golden altar they shall spread a cloth of blue, and cover it with a covering of badgers' skins, and shall put to it its staffs.
Watafunika na nguo ya samawi katika madhabau ya dhahabu. Wataifunika na ngozi za pomboo, na kuweka ile miti ya kubebea.
12 And they shall take all the instruments of ministry, with which they minister in the sanctuary, and put [them] in a cloth of blue, and cover them with a covering of badgers' skins, and shall put [them] on a bar.
Watavichukua vyombo vyote vya kazi takatifu na kuvizonga kwenye hiyo nguo ya rangi ya samawi. Watavifunika na ngozi za pomboo na kuviweka hivyo vyombo kwenye miti ya kubebea.
13 And they shall take away the ashes from the altar, and spread a purple cloth upon it:
Watayaondoa majivu kwenye madhabahu na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake.
14 And they shall put upon it all its vessels, with which they minister about it, [even] the censers, the flesh-hooks, and the shovels, and the basins, all the vessels of the altar; and they shall spread upon it a covering of badgers' skins, and put to it its staffs.
Watavieka kwenye miti ya kubebea vyombo vyote wanavyovitumia kwa kazi ya madhabahuni. Vyombo hivi ni vyetezo, majembe, mabakuli na vitu vingine vya madhabahuni. Wataifuniks madhabahu na ngozi za pomboo na kuweka ile miti ya kubebea.
15 And when Aaron and his sons have made an end of covering the sanctuary, and all the vessels of the sanctuary, as the camp is to move forward; after that, the sons of Kohath shall come to bear [it]: but they shall not touch [any] holy thing, lest they die. These [things are] the burden of the sons of Kohath in the tabernacle of the congregation.
Wakati Haruni na wanawe walipokuwa wamekamilisha kupafunika mahali patakatifu na vyombo vyote, na kambi itakapoanza kuendelea mbele, ndipo wana wa Kohathi watakapokuja kubeba vitu vya mahali patakatifu. Kama watagusa vyombo vitakatifu, lazima watakufa. Hii ni kazi ya wana wa uzao wa Kohathi, kubeba mapambo ya hema ya kukutania.
16 And to the office of Eleazar the son of Aaron the priest [pertain] the oil for the light, and the sweet incense, and the daily meat-offering, and the anointing oil, [and] the oversight of all the tabernacle, and of all that [is] in it, in the sanctuary, and in its vessels.
Eliazari mwana wa Haruni kuhani atalinda na kusimamia mafuta ya taa, ubani mzuri, sadaka za mara kwa mara na mafuta ya upako. Atasimamia ulinzi wa hema lote na vyote vilivyomo, mahali patakatifu na vyombo vyake.”
17 And the LORD spoke to Moses and to Aaron, saying,
BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema,
18 Cut ye not off the tribe of the families of the Kohathites from among the Levites:
Usiruhusu kabila la Wakohathi kuondolewa kati ya Walawi.
19 But thus do to them, that they may live, and not die, when they approach to the most holy things: Aaron and his sons shall go in, and appoint them every one to his service and to his burden:
Walinde waishi ili wasije wakafa, kwa kufanya hivi. Wanapokuwa wanasogelea
20 But they shall not go in to see when the holy things are covered, lest they die.
wasije wakaingia ndani ili kuona eneo takatifu hata kwa kitambo, vinginevyo watakufa. Bali Haruni na wanawe wanaweza kuingia, ndipo Haruni na Wanawe watakapowapangia Wakohathi kazi maalumu ya kufanya, kwa kila mmoj.”
21 And the LORD spoke to Moses, saying,
BWANA akanena na Musa tena, Akasema, “Fanya sensa kwa wana Gerishoni pia, kwa kufuata familia za mababu zao, koo zao.
22 Take also the sum of the sons of Gershon, throughout the house of their fathers, by their families;
Uwahesabu wale wenye umri wa mika thelathini hadi miaka hamsini.
23 From thirty years old and upward until fifty years old shalt thou number them; all that enter in to perform the service, to do the work in the tabernacle of the congregation.
Uwahesabu wote ili waje kuungana na wale wanaotumika katika hema ya kukutania.
24 This [is] the service of the families of the Gershonites, to serve, and for burdens:
Hii ndiyo itakuwa kazi ya koo za Gerishoni, wanapotumikia na wanachobeba.
25 And they shall bear the curtains of the tabernacle, and the tabernacle of the congregation, its covering, and the covering of the badgers' skins that [is] above upon it, and the hanging for the door of the tabernacle of the congregation,
Watabeba pazia la masikani, hema la kukutania, na vifunikio vyake, vifuniko vya ngozi ya pomboo ambvyo viko juu yake, na pazia kwenye lango la hema ya kukutania.
26 And the hangings of the court, and the hanging for the door of the gate of the court, which [is] by the tabernacle and by the altar round about, and their cords, and all the instruments of their service, and all that is made for them: so shall they serve.
Watabeba pazia la ua, pazia la kwenye mlango wa ua, ambao uko karibu na maskani karibu na madhabahu, kamba zake na vifaa vyote vya utumishi wake. Chochote kinachotakiwa kufanywa kutokana na vitu hivi, wao ndio watakaofanya.
27 At the appointment of Aaron and his sons shall be all the service of the sons of the Gershonites, in all their burdens, and in all their service: and ye shall appoint to them in charge all their burdens.
Haruni na wanawe ndio watakaongoza utumishi wa uzao wa Wagerishoni, kwa vitu vyote vile vya kusafirisha, na katika utumishi wao wote. Lazima uwagawie majukumu yao yote.
28 This [is] the service of the families of the sons of Gershon in the tabernacle of the congregation: and their charge [shall be] under the hand of Ithamar the son of Aaron the priest.
Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa wana wa Wagerishoni katka hema ya kukutania. Ithamari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza katika utumishi.
29 As for the sons of Merari, thou shalt number them after their families, by the house of their fathers;
Utawahesabu uzao wa Merari kwa koo zao, na uwapange katika familia za mabau zao,
30 From thirty years old and upward even to fifty years old shalt thou number them, every one that entereth into the service, to do the work of the tabernacle of the congregation.
kuanzia wenye umri wa miaka thelatini hadi miaka hamsini. Umuhesabu kila atakayeungana na kundi lenye utumishi katika hema ya kukutania.
31 And this [is] the charge of their burden, according to all their service in the tabernacle of the congregation; the boards of the tabernacle, and its bars, and its pillars, and its sockets,
Huu ndio wajibu na kazi yao katika utumishi wao kwenye hema ya kukutania. Watazilinda mbao za maskani, mataluma yake, nguzo na makalishio yake,
32 And the pillars of the court round about, and their sockets, and their pins, and their cords, with all their instruments, and with all their service: and by name ye shall reckon the instruments of the charge of their burden.
pamoja na nguzo za ua zinazozunguka masikani, makalishio yake, vigingi na kamba zake, na vifaa vinginevya ujenzi. Waorodheshe kwa majina na majukumu yao.
33 This [is] the service of the families of the sons of Merari, according to all their service, in the tabernacle of the congregation, under the hand of Ithamar the son of Aaron the priest.
Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa Merari, ambao wanatakiwa kufanya katika hema ya kukutania, chini ya uongozi wa Ithmari mwana wa Haruni kuhani.”
34 And Moses and Aaron and the chief of the congregation numbered the sons of the Kohathites after their families, and after the house of their fathers,
Musa na Haruni na viongozi wa watu waliwahesabu wana wa uzao wa Wakohathi kwa kufuata koo za familia za mababu zao.
35 From thirty years old and upward even to fifty years old, every one that entereth into the service, for the work in the tabernacle of the congregation:
Waliwahesabu wale wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Walimhesabu kila mmoja aliyepaswa kuungana na kundi linalotoa huduma ya utumishi kwenye hema ya kukutania.
36 And those that were numbered of them by their families were two thousand seven hundred and fifty.
Waliwahesabu wanaume 2, 750 kwa kufuata koo zao.
37 These [were] they that were numbered of the families of the Kohathites, all that might do service in the tabernacle of the congregation, whom Moses and Aaron numbered according to the commandment of the LORD by the hand of Moses.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote kutoka koo na familia za Wakohathi ambao hutumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi kwa kumtii BWANA aliyewaagiza kupitia kwa Musa.
38 And those that were numbered of the sons of Gershon, throughout their families, and by the house of their fathers,
Uzao wa Gerishoni walihesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao,
39 From thirty years old and upward even to fifty years old, every one that entereth into the service, for the work in the tabernacle of the congregation,
kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kwa kila mmoja aliyetakiwa kuungana na watu wanaotoa huduma kwenye hema ya kukutania.
40 Even those that were numbered of them, throughout their families, by the house of their fathers, were two thousand and six hundred and thirty.
Wanaume wote waliohesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao walikuwa 2, 630.
41 These [are] they that were numbered of the families of the sons of Gershon, of all that might do service in the tabernacle of the congregation, whom Moses and Aaron numbered according to the commandment of the LORD.
Musa na Haruni walizihesabu koo za uzao wa Gerishoni ambao watatumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi ili kutii ambacho BWANA aliwaamuru kufanya kuptia kwa Musa.
42 And those that were numbered of the families of the sons of Merari, throughout their families, by the house of their fathers,
Uzao wa Merari walihesabiwa kwa koo kupitia familia za mababu zao,
43 From thirty years old and upward even to fifty years old, every one that entereth into the service for the work in the tabernacle of the congregation,
kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kila anayepaswa kuungana na watu wanaotumika kwenye hema ya kukutania.
44 Even those that were numbered of them after their families, were three thousand and two hundred.
Wanaume wote waliohesabiwa kupitia koo za familia za mababu zao walikuwa 3. 200.
45 These [are] those that were numbered of the families of the sons of Merari, whom Moses and Aaron numbered according to the word of the LORD by the hand of Moses.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume hawa, uzao wa Merari. Kw kufanya hivi walitii amri ya BWANA aliyowaaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
46 All those that were numbered of the Levites, whom Moses and Aaron and the chief of Israel numbered, after their families, and after the house of their fathers,
Kwa hiyo Musa na Haruni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kw kufuata koo na familia za mababu zao
47 From thirty years old and upward even to fifty years old, every one that came to do the service of the ministry, and the service of the burden in the tabernacle of the congregation,
kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. walimhesabu kila aliyepaswa kufanya kazi kwenye masikani, na kila aliyepaswa kubeba na kulinda vitu vya kwenye hema ya kukutania.
48 Even those that were numbered of them, were eight thousand and five hundred and eighty.
Waliwahesabu wanaume 8, 580.
49 According to the commandment of the LORD they were numbered by the hand of Moses, every one according to his service, and according to his burden: thus were they numbered by him, as the LORD commanded Moses.
Kwa agizo la BWANA, Musa alimhesabu kila mwanamume na kutunza kumbukumbu ya kazi ambayo kila mmoja anaweza kufanya. Kwa hivyo, walitii kile ambacho BWANA alikuwa amewaagiza kufanya kupitia kwa Musa.

< Numbers 4 >