< Numbers 28 >

1 And the LORD spoke to Moses, saying,
BWANA akanena na Musa akamwambia,
2 Command the children of Israel, and say to them, My offering, [and] my bread for my sacrifices made by fire, [for] a sweet savor to me, shall ye observe to offer to me in their due season.
“Waamuru wana wa Isrseli uwaambie, 'Mtanitolea sadaka kwa wakati uliopangwa, chakula cha sadaka yangu kilichotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa ajili yangu.
3 And thou shalt say to them, This [is] the offering made by fire which ye shall offer to the LORD; two lambs of the first year without spot day by day, [for] a continual burnt-offering.
Pia uwaambie, 'Hii ni sadaka iliyotengenezwa kwa moto ambayo mtaitoa kwa BWANA- mwanakondoo dume wa mwaka mmoja asiyekuwa na waa, wawili kila siku kuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku.
4 The one lamb shalt thou offer in the morning, and the other lamb shalt thou offer at evening.
Mwanakodoo mmoja atatolewa sadaka asubuhi, na mwingine atatolewa sadaka jioni.
5 And a tenth [part] of an ephah of flour for a meat-offering, mingled with a fourth [part] of a hin of beaten oil.
Mtatoa sadaka ya sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa.
6 [It is] a continual burnt-offering, which was ordained in mount Sinai for a sweet savor, a sacrifice made by fire to the LORD.
Hii ni sadaka ya ya kuteketezwa ya kila siku iliyoamriwa mlima Sinai ili kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili ya BWANA.
7 And the drink-offering of it [shall be] the fourth [part] of a hin for the one lamb: in the holy [place] shalt thou cause the strong wine to be poured to the LORD [for] a drink-offering.
Pamoja na robo ya hini ya sadaka ya kinywaji kwa mmoja wa hao wanakondoo. Utaimimina mahali patakatifu hiyo sadaka ya kinywaji kwa BWANA.
8 And the other lamb shalt thou offer at evening; as the meat-offering of the morning, and as the drink-offering of it, thou shalt offer [it], a sacrifice made by fire, of a sweet savor to the LORD.
Yule mwanakondoo mwingine utamtoa sadaka jioni pamoja na sadaka ya unga kama kama yule wa asubuhi alivyotolewa. Pia utatoa tena sadaka ya kinywaji pamoja naye, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA.
9 And on the sabbath-day two lambs of the first year without spot, and two tenth-parts of flour [for] a meat-offering, mingled with oil, and its drink-offering.
Katika siku ya Sabato utatoa wanakondoo dume wawili, wa umri wa mwaka mmoja kila mmoja wasiokuwa na dosari, na sehemu ya kumi mbili ya efa ya unga mwembamba kwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, pamoja na sadaka ya kinywaji.
10 [This is] the burnt-offering of every sabbath, besides the continual burnt-offering, and his drink-offering.
Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa kila siku ya Sabato, kama nyongeza ya ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya kinywaji.
11 And in the beginnings of your months ye shall offer a burnt-offering to the LORD; two young bullocks, and one ram, seven lambs of the first year without spot;
Kila mwanzo wa mwezi, mtatoa sadaka za kuteketezwa kwa BWANA. Utatoa sadaka ya fahari wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari.
12 And three tenth-parts of flour [for] a meat-offering, mingled with oil, for one bullock; and two tenth-parts of flour [for] a meat-offering, mingled with oil, for one ram;
Pia mtatoa sehemu ya kumi tatu ya efa unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari, na sehemu za kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa yule kondoo mume mmoja.
13 And a several tenth-part of flour mingled with oil [for] a meat-offering to one lamb, [for] a burnt-offering of a sweet savor, a sacrifice made by fire to the LORD.
Pia mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga kwa kila mwanakondoo. Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa, ya kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajilI ya BWANA.
14 And their drink-offering shall be half a hin of wine to a bullock, and the third [part] of a hin to a ram, and a fourth [part] of a hin to a lamb: this [is] the burnt-offering of every month throughout the months of the year.
Sadaka ya kinywaji ya watu itakuwa nusu ya hini ya divai ya yule fahari, sehemu ya tatu ya hini ya kondoo dume, na robo ya hini ya mwanakondoo. Hii ndiyo itakuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi kwa miezi yote ya mwaka.
15 And one kid of the goats for a sin-offering to the LORD shall be offered, besides the continual burnt-offering, and his drink-offering.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kwa BWANA. Hii itakuwa nyongeza kwa ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya viinywaji.
16 And on the fourteenth day of the first month [is] the passover of the LORD.
Katika siku kumi na nne, ya mwezi wa kwanza itakuwa Pasaka ya BWANA.
17 And on the fifteenth day of this month [is] the feast: seven days shall unleavened bread be eaten.
Katika sku ya kumi na tano ya mwezi huu kutakuwa na sikukuu. Mtakuka mikate isiyo na chachu kwa siku saba.
18 On the first day [shall be] a holy convocation; [in it] ye shall do no manner of servile work.
Katika siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA. Katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku
19 But ye shall offer a sacrifice made by fire [for] a burnt-offering to the LORD; two young bullocks, and one ram, and seven lambs of the first year: they shall be to you without blemish:
Hata hivyo, mtatoa sadaka iliyotengenezwa kwa moto, sadaka ya kuteketezwa kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari wawili, kondoo dume mmoja, na kondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wakamilifu.
20 And their meat-offering [shall be of] flour mingled with oil: three tenth-parts shall ye offer for a bullock, and two tenth-parts for a ram;
Pamoja na yule fahari, mtatoa sadaka sehemu za tatu efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, pamoja na yule kondoo mume sehemu za pili za kumi.
21 A several tenth-part shalt thou offer for every lamb, throughout the seven lambs:
Kwa kila wale wanakondoo saba, mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta,
22 And one goat [for] a sin-offering, to make an atonement for you.
na beberu mmoja kuwa sdaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
23 Ye shall offer these besides the burnt-offering in the morning, which [is] for a continual burnt-offering.
Mtotoa hivi vitu kama sadaka ya nyongeza katika ile sadaka ya kila siku inayotakiwa kila asubuhi.
24 After this manner ye shall offer daily throughout the seven days, the food of the sacrifice made by fire, of a sweet savor to the LORD: it shall be offered besides the continual burnt-offering, and his drink-offering.
Kama ilivyofafanuliwa hapa, mtatoa sadaka hizi kila siku, kwa zile siku saba za Pasaka, kile chakula cha sadaka kilichotengenezwa kwa moto kuwa harufu nzuri kwa BWANA. Hiki kitatolewa kuwa sadaka ya nyongeza ya ile sadaka ya kuteketezwa na pamoja na ile sadaka ya vinywaji.
25 And on the seventh day ye shall have a holy convocation; ye shall do no servile work.
Siku ya saba mtakuwa na kusanyiko takatifu ili kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye zile kazi zenu zakila siku.
26 Also in the day of the first-fruits, when ye bring a new meat-offering to the LORD, after your weeks [are ended], ye shall have a holy convocation; ye shall do no servile work:
Pia katika siku ya malimbuko, mtakapokuwa mnatoa sadaka ya unga mpya katika sikukuu zenu za Majuma, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku.
27 But ye shall offer the burnt-offering for a sweet savor to the LORD; two young bullocks, one ram, seven lambs of the first year;
Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari wawili wachanga, kondoo mume mmoja, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja.
28 And their meat-offering of flour mingled with oil, three tenth-parts to one bullock, two tenth-parts to one ram,
Pamoja na hiyo mtatoa sadaka ya unga: unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari na sehemu kumi mbili za yule kondoo mume.
29 A several tenth part to one lamb, throughout the seven lambs;
Toeni sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila wale wanakondoo saba,
30 [And] one kid of the goats, to make an atonement for you.
na beberu mmoja ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
31 Ye shall offer [them] besides the continual burnt-offering and his meat-offering (they shall be to you without blemish) and their drink-offerings.
Mtakapotoa hao wanyama wasio na dosari, pamoja na sadaka zake za vinywaji, hii itakuwa sadaka ya nyongeza katika zile sadaka za kila siku na pamoja na zile sadaka za unga.'”

< Numbers 28 >