< Luke 23 >
1 And the whole multitude of them arose, and led him to Pilate.
Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
2 And they began to accuse him, saying, We found this [man] perverting the nation, and forbidding to give tribute to Cesar, saying, that he himself is Christ a king.
Wakaanza kumshtaki wakisema: “Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme.”
3 And Pilate asked him, saying, Art thou the King of the Jews? And he answered him and said, Thou sayest [it].
Pilato akamwuliza Yesu, “Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
4 Then said Pilate to the chief priests, and [to] the people, I find no fault in this man.
Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, “Sioni kosa lolote katika mtu huyu.”
5 And they were the more fierce, saying, He stirreth up the people, teaching throughout all Judea, beginning from Galilee to this place.
Lakini wao wakasisitiza wakisema: “Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa.”
6 When Pilate heard of Galilee, he asked whether the man was a Galilean.
Pilato aliposikia hayo, akauliza, “Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?”
7 And as soon as he knew that he belonged to Herod's jurisdiction, he sent him to Herod, who himself was also at Jerusalem at that time.
Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
8 And when Herod saw Jesus, he was exceeding glad: for he had been for a long time, desirous to see him, because he had heard many things of him; and he hoped to see some miracle done by him.
Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
9 Then he questioned with him in many words; but he answered him nothing.
Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
10 And the chief priests and scribes stood and vehemently accused him.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11 And Herod with his troops set him at naught, and mocked [him], and arrayed him in a gorgeous robe, and sent him again to Pilate.
Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
12 And the same day Pilate and Herod were made friends together; for before they were at enmity between themselves.
Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
13 And Pilate, when he had called together the chief priests, and the rulers, and the people,
Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
14 Said to them, Ye have brought this man to me, as one that perverteth the people: and behold, I, having examined [him] before you, have found no fault in this man, touching those things of which ye accuse him;
akawaambia, “Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
15 No, nor yet Herod: for I sent you to him; and lo, nothing worthy of death is done to him:
Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
16 I will therefore chastise him, and release [him].
Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.”
17 (For of necessity he must release one to them at the feast.)
Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18 And they cried out all at once, saying, Away with this [man], and release to us Barabbas:
Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!”
19 (Who, for a certain sedition made in the city, and for murder, was cast into prison.)
(Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20 Pilate therefore, willing to release Jesus, spoke again to them.
Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21 But they cried, saying, Crucify, crucify him.
lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
22 And he said to them the third time, Why, what evil hath he done? I have found no cause of death in him; I will therefore chastise him, and let [him] go.
Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”
23 And they were urgent with loud voices, requiring that he might be crucified: and the voices of them, and of the chief priests prevailed.
Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
24 And Pilate gave sentence that it should be as they required.
Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
25 And he released to them him that for sedition and murder had been cast into prison, whom they had desired; but he delivered Jesus to their will.
Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
26 And as they led him away, they laid hold upon one Simon a Cyrenian, coming out of the country, and on him they laid the cross, that he might bear [it] after Jesus.
Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
27 And there followed him a great company of people, and of women, who also bewailed and lamented him.
Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
28 But Jesus turning to them, said, Daughters of Jerusalem, weep not for me, but weep for yourselves, and for your children.
Yesu akawageukia, akasema, “Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
29 For behold, the days are coming, in which they shall say, Blessed [are] the barren, and the wombs that never bore, and the breasts which never nourished infants.
Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
30 Then shall they begin to say to the mountains, Fall on us; and to the hills, Cover us.
Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
31 For if they do these things in a green tree, what will be done in the dry?
Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?”
32 And two others, [who were] malefactors, were led with him to be put to death.
Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
33 And when they had come to the place which is called Calvary, there they crucified him, and the malefactors; one on the right hand, and the other on the left.
Walipofika mahali paitwapo, “Fuvu la Kichwa,” ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
34 Then said Jesus, Father, forgive them: for they know not what they do. And they parted his raiment, and cast lots.
Yesu akasema, “Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya.” Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
35 And the people stood beholding. And the rulers also with them derided [him], saying, He saved others; let him save himself, if he is Christ the chosen of God.
Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: “Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!”
36 And the soldiers also mocked him, coming to him, and offering him vinegar,
Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
37 And saying, If thou art the King of the Jews, save thyself.
wakisema: “Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe.”
38 And a superscription also was written over him, in letters of Greek, and Latin, and Hebrew, THIS IS THE KING OF THE JEWS.
Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: “Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi.”
39 And one of the malefactors, who were hanged, railed on him, saying, If thou art Christ, save thyself and us.
Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: “Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia.”
40 But the other answering, rebuked him, saying, Dost not thou fear God, seeing thou art in the same condemnation?
Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: “Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
41 And we indeed justly; for we receive the due reward of our deeds: but this man hath done nothing amiss.
Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya.”
42 And he said to Jesus, Lord, remember me when thou comest into thy kingdom.
Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.”
43 And Jesus said to him, Verily I say to thee, This day shalt thou be with me in paradise.
Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.”
44 And it was about the sixth hour, and there was a darkness over all the land until the ninth hour.
Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
45 And the sun was darkened, and the vail of the temple was rent in the midst.
na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
46 And when Jesus had cried with a loud voice, he said, Father, into thy hands I commend my spirit: and having said thus, he expired.
Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako.” Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
47 Now when the centurion saw what was done, he glorified God, saying, Certainly this was a righteous man.
Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: “Hakika huyu alikuwa mtu mwema.”
48 And all the people that came together to that sight, beholding the things which were done, smote their breasts, and returned.
Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
49 And all his acquaintance, and the women that followed him from Galilee, stood afar off beholding these things.
Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
50 And behold, [there was] a man named Joseph, a counselor: [and he was] a good man, and a just:
Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
51 (The same had not consented to the counsel and deed of them) [he was] of Arimathea, a city of the Jews; who also himself waited for the kingdom of God.
Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
52 This [man] went to Pilate, and begged the body of Jesus.
Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53 And he took it down, and wrapped it in linen, and laid it in a sepulcher that was hewn in stone, in which man was never before laid.
Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
54 And that day was the preparation, and the sabbath drew on.
Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
55 And the women also, who came with him from Galilee, followed after, and beheld the sepulcher, and how his body was laid.
Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
56 And they returned, and prepared spices and ointments; and rested on the sabbath, according to the commandment.
Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.