< Luke 2 >

1 And it came to pass in those days, that there went out a decree from Cesar Augustus, that all the world should be taxed.
Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2 ([And] this taxing was first made when Cyrenius was governor of Syria.)
Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
3 And all went to be taxed, every one into his own city.
Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
4 And Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, into Judea, to the city of David, which is called Bethlehem; (because he was of the house and lineage of David)
Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
5 To be taxed with Mary his espoused wife, being great with child.
Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
6 And so it was, that while they were there, the days were accomplished that she should be delivered.
Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
7 And she brought forth her first-born son, and wrapped him in swaddling-clothes, and laid him in a manger; because there was no room for them in the inn.
akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
8 And there were in the same country shepherds abiding in the field, keeping watch over their flock by night.
Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
9 And lo, the angel of the Lord came upon them, and the glory of the Lord shone around them; and they were in great fear.
Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
10 And the angel said to them, Fear not: for behold, I bring you good tidings of great joy which shall be to all people.
Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
11 For to you is born this day, in the city of David, a Savior, who is Christ the Lord.
Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
12 And this [shall be] a sign to you; Ye shall find the babe wrapped in swaddling-clothes, lying in a manger.
Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
13 And suddenly there was with the angel a multitude of the heavenly host praising God, and saying,
Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
14 Glory to God in the highest, and on earth peace, good will towards men.
“Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
15 And it came to pass, when the angels had departed from them into heaven, the shepherds said one to another, Let us now go even to Bethlehem, and see this thing which is come to pass, which the Lord hath made known to us.
Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
16 And they came with haste, and found Mary and Joseph, and the babe lying in a manger.
Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
17 And when they had seen [it], they made known abroad the saying which was told them concerning this child.
Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
18 And all they that heard [it], wondered at those things which were told them by the shepherds.
Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
19 But Mary kept all these things, and pondered [them] in her heart.
Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
20 And the shepherds returned, glorifying and praising God for all the things that they had heard and seen, as it was told to them.
Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
21 And when eight days were accomplished for the circumcising of the child, his name was called JESUS, who was so named by the angel before he was conceived in the womb.
Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
22 And when the days of her purification according to the law of Moses were accomplished, they brought him to Jerusalem, to present [him] to the Lord;
Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
23 (As it is written in the law of the Lord, Every male that is the first born of his mother shall be called holy to the Lord)
Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
24 And to offer a sacrifice according to that which is said in the law of the Lord, A pair of turtle-doves, or two young pigeons.
Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
25 And behold, there was a man in Jerusalem, whose name [was] Simeon; and the same man [was] just and devout, waiting for the consolation of Israel: and the Holy Spirit was upon him.
Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
26 And it was revealed to him by the Holy Spirit, that he should not see death, before he had seen the Lord's Christ.
Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
27 And he came by the spirit into the temple; and when the parents brought in the child Jesus, to do for him after the custom of the law,
Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
28 Then he took him up in his arms, and blessed God, and said,
Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
29 Lord, now lettest thou thy servant depart in peace, according to thy word:
“Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30 For my eyes have seen thy salvation,
Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
31 Which thou hast prepared before the face of all people;
ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
32 A light to enlighten the Gentiles, and the glory of thy people Israel.
Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
33 And Joseph and his mother marveled at those things which were spoken concerning him.
Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
34 And Simeon blessed them, and said to Mary his mother, Behold, this [child] is set for the fall and rising again of many in Israel; and for a sign which shall be spoken against;
Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
35 (And a sword shall pierce through thy own soul also) that the thoughts of many hearts may be revealed.
na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
36 And there was one Anna, a prophetess, the daughter of Phanuel, of the tribe of Asher: she was of a great age, and had lived with a husband seven years from her virginity;
Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
37 And she [was] a widow of about eighty four years, who departed not from the temple, but served [God] with fastings and prayers night and day.
Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
38 And she coming in that instant, gave thanks likewise to the Lord, and spoke of him to all them that looked for redemption in Jerusalem.
Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
39 And when they had performed all things according to the law of the Lord, they returned into Galilee, to their own city Nazareth.
Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
40 And the child grew, and became strong in spirit, filled with wisdom: and the grace of God was upon him.
Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
41 Now his parents went to Jerusalem every year at the feast of the passover.
Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42 And when he was twelve years old, they went up to Jerusalem according to the custom of the feast.
Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43 And when they had fulfilled the days, as they returned, the child Jesus tarried behind in Jerusalem; and Joseph and his mother knew not [of it].
Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
44 But they, supposing him to be in the company, went a day's journey; and they sought him among [their] relations and acquaintance.
Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
45 And when they found him not, they returned to Jerusalem, seeking him.
Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
46 And it came to pass, that after three days they found him in the temple, sitting in the midst of the doctors, both hearing them, and asking them questions.
Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 And all that heard him were astonished at his understanding and answers.
Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
48 And when they saw him, they were amazed: and his mother said to him, Son, why hast thou thus dealt with us? behold, thy father and I have sought thee sorrowing.
Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
49 And he said to them, How is it that ye sought me? knew ye not that I must be about my Father's business?
Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
50 And they understood not the saying which he spoke to them.
Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
51 And he went down with them, and came to Nazareth, and was subject to them: but his mother kept all these sayings in her heart.
Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
52 And Jesus increased in wisdom and stature, and in favor with God and man.
Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.

< Luke 2 >