< Judges 20 >

1 Then all the children of Israel went out, and the congregation was assembled as one man, from Dan even to Beer-sheba, with the land of Gilead, to the LORD in Mizpeh.
Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
2 And the chief of all the people, [even] of all the tribes of Israel, presented themselves in the assembly of the people of God, four hundred thousand footmen that drew sword.
Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
3 (Now the children of Benjamin heard that the children of Israel were gone up to Mizpeh.) Then said the children of Israel, Tell [us], how was this wickedness?
(Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
4 And the Levite, the husband of the woman that was slain, answered and said, I came into Gibeah that [belongeth] to Benjamin, I and my concubine, to lodge.
Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
5 And the men of Gibeah rose against me, and surrounded the house upon me by night, [and] thought to have slain me: and my concubine have they forced, that she is dead.
Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
6 And I took my concubine, and cut her in pieces, and sent her throughout all the country of the inheritance of Israel: for they have committed lewdness and folly in Israel.
Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
7 Behold, ye [are] all children of Israel; give here your advice and counsel.
Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
8 And all the people arose as one man, saying, We will not any [of us] go to his tent, neither will we any [of us] turn into his house:
Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
9 But now this [shall be] the thing which we will do to Gibeah: [we will go up] by lot against it;
Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
10 And we will take ten men of a hundred throughout all the tribes of Israel, and a hundred of a thousand, and a thousand out of ten thousand, to fetch provisions for the people, that they may do, when they come to Gibeah of Benjamin, according to all the folly that they have wrought in Israel.
Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
11 So all the men of Israel were gathered against the city, knit together as one man.
Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
12 And the tribes of Israel sent men through all the tribe of Benjamin, saying, What wickedness [is] this that is done among you?
Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
13 Now therefore deliver [us] the men, the children of Belial, who [are] in Gibeah, that we may put them to death, and banish evil from Israel. But the children of Benjamin would not hearken to the voice of their brethren, the children of Israel:
Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
14 But the children of Benjamin assembled out of the cities to Gibeah, to go out to battle against the children of Israel.
Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
15 And the children of Benjamin were numbered at that time out of the cities twenty and six thousand men that drew sword, besides the inhabitants of Gibeah, who were numbered seven hundred chosen men.
Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
16 Among all this people [there were] seven hundred chosen men left-handed; every one could sling stones to a hair -[breadth], and not miss.
Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
17 And the men of Israel, besides Benjamin, were numbered four hundred thousand men that drew sword: all these [were] men of war.
Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
18 And the children of Israel arose, and went up to the house of God, and asked counsel of God, and said, Which of us shall go up first to the battle against the children of Benjamin? And the LORD said, Judah [shall go up] first.
Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
19 And the children of Israel rose in the morning, and encamped against Gibeah.
Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
20 And the men of Israel went out to battle against Benjamin; and the men of Israel put themselves in array to fight against them at Gibeah.
Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
21 And the children of Benjamin came forth from Gibeah, and destroyed down to the ground of the Israelites that day twenty and two thousand men.
Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
22 And the people the men of Israel encouraged themselves, and set their battle again in array in the place where they put themselves in array the first day.
Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
23 (And the children of Israel went up and wept before the LORD until evening, and asked counsel of the LORD, saying, Shall I go up again to battle against the children of Benjamin my brother? And the LORD said, Go up against him.)
Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
24 And the children of Israel came near against the children of Benjamin the second day.
Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
25 And Benjamin went forth against them out of Gibeah the second day, and destroyed down to the ground of the children of Israel again eighteen thousand men; all these drew the sword.
Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
26 Then all the children of Israel, and all the people, went up, and came to the house of God, and wept, and sat there before the LORD, and fasted that day until evening, and offered burnt-offerings and peace-offerings before the LORD.
Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
27 And the children of Israel inquired of the LORD, (for the ark of the covenant of God [was] there in those days,
Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
28 And Phinehas, the son of Eleazar, the son of Aaron, stood before it in those days, ) saying, Shall I yet again go out to battle against the children of Benjamin my brother, or shall I cease? And the LORD said, Go up; for to-morrow I will deliver them into thy hand.
na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
29 And Israel set liers in wait around Gibeah.
Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
30 And the children of Israel went up against the children of Benjamin on the third day, and put themselves in array against Gibeah, as at other times.
Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
31 And the children of Benjamin went out against the people, [and] were drawn away from the city; and they began to smite of the people, [and] kill, as at other times, in the highways, of which one goeth up to the house of God, and the other to Gibeah in the field, about thirty men of Israel.
Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
32 And the children of Benjamin said, They [are] smitten down before us, as at the first. But the children of Israel said, Let us flee, and draw them from the city to the highways.
Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
33 And all the men of Israel rose out of their place, and put themselves in array at Baal-tamar: and the liers in wait of Israel came forth out of their places, [even] out of the meadows of Gibeah.
Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
34 And there came against Gibeah ten thousand chosen men out of all Israel, and the battle was severe: but they knew not that evil [was] near them.
Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
35 And the LORD smote Benjamin before Israel: and the children of Israel destroyed of the Benjaminites that day twenty and five thousand and a hundred men: all these drew the sword.
Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
36 So the children of Benjamin saw that they were smitten: for the men of Israel gave place to the Benjaminites, because they trusted to the liers in wait which they had set beside Gibeah.
Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
37 And the liers in wait hasted, and rushed upon Gibeah; and the liers in wait drew [themselves] along, and smote all the city with the edge of the sword.
Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
38 Now there was an appointed sign between the men of Israel and the liers in wait, that they should make a great flame with smoke to rise from the city.
Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
39 And when the men of Israel retired in the battle, Benjamin began to smite [and] kill of the men of Israel about thirty persons: for they said, Surely they are smitten down before us, as [in] the first battle.
ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
40 But when the flame began to rise from the city with a pillar of smoke, the Benjaminites looked behind them, and behold, the flame of the city ascended to heaven.
Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
41 And when the men of Israel turned again, the men of Benjamin were amazed: for they saw that evil had come upon them.
Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
42 Therefore they turned [their backs] before the men of Israel to the way of the wilderness; but the battle overtook them; and them who [came] out of the cities they destroyed in the midst of them.
Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
43 [Thus] they inclosed the Benjaminites on all sides, [and] chased them, [and] trod them down with ease over against Gibeah towards the sun-rising.
Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
44 And there fell of Benjamin eighteen thousand men; all these [were] men of valor.
Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
45 And they turned and fled towards the wilderness to the rock of Rimmon: and they gleaned of them in the highways five thousand men; and pursued hard after them to Gidom, and slew two thousand men of them.
Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
46 So that all who fell that day of Benjamin were twenty and five thousand men that drew the sword; all these [were] men of valor.
Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
47 But six hundred men turned and fled to the wilderness to the rock Rimmon, and abode in the rock Rimmon four months.
Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
48 And the men of Israel turned again upon the children of Benjamin, and smote them with the edge of the sword, as well the men of [every] city, as the beast, and all that came to hand: also they set on fire all the cities that they came to.
Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.

< Judges 20 >