< Joshua 1 >

1 Now after the death of Moses the servant of the LORD, it came to pass, that the LORD spoke to Joshua the son of Nun, Moses's minister, saying,
Sasa ilitokea baada ya kufa kwa Musa, mtumishi wa Yahweh, Yahweh alimwambia Yoshua, mwana wa Nuni, msaidizi mkuu wa Musa, kusema,
2 Moses my servant is dead; now therefore arise, go over this Jordan, thou, and all this people, to the land which I do give to them, [even] to the children of Israel.
“Musa, mtumishi wangu amekufa. Sasa basi inuka, vuka mto huu wa Yordani, wewe na watu hawa wote, kuingia katika nchi ambayo ninawapa - watu waisraeli.
3 Every place that the sole of your foot shall tread upon, that have I given to you, as I said to Moses.
Nimewapa ninyi kila sehemu ambapo nyayo za miguu yenu itakanyaga. Nimewapa ninyi, kama nilivyomwahidi Musa.
4 From the wilderness and this Lebanon even to the great river, the river Euphrates, all the land of the Hittites, and to the great sea towards the setting of the sun, shall be your border.
kuanzia jangwani na Lebanoni, hadi mto mkubwa wa Frati, nchi yote ya Wahiti, na hata Bahari kuu, ambako jua huzama, itakuwa nchi yenu.
5 There shall not any man be able to stand before thee all the days of thy life: as I was with Moses, [so] I will be with thee: I will not fail thee, nor forsake thee.
Hakuna mtu awaye yote atakayeweza kusimama kinyume chako siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa na Musa. Sitakupungukia wala kukuacha.
6 Be strong and of a good courage: for to this people shalt thou divide for an inheritance the land which I swore to their fathers to give them.
Uwe hodari na jasiri. Wewe utawafanya watu hawa wairithi nchi ambayo niliwaahidi baba zao kuwa ningewapa.
7 Only be thou strong and very courageous, that thou mayest observe to do according to all the law which Moses my servant commanded thee: turn not from it [to] the right hand or [to] the left, that thou mayest prosper whithersoever thou goest.
Uwe hodari na jasiri sana. uwe makini kutii sheria zote ambazo Musa mtumishi wangu alikuagiza. Usikengeuke upande wa kulia au wa kushoto, ili uweze kufanikiwa kila mahali utakapoenda.
8 This book of the law shall not depart out of thy mouth; but thou shalt meditate in it day and night, that thou mayest observe to do according to all [that is] written therein: for then thou shalt make thy way prosperous, and then thou shalt have good success.
Siku zote uuongee juu ya kitabu hiki cha sheria. Utakitafakari mchana na usiku ili kwamba uweze kutii yote yaliyoandikwa humo. Kisha utastawi na kufanikiwa.
9 Have not I commanded thee? Be strong and of a good courage; be not afraid, neither be thou dismayed: for the LORD thy God [is] with thee whithersoever thou goest.
Je si mimi niliyekuagiza? Uwe hadori na jasiri! Usiogope. Usivunjike moyo. Yahweh Mungu wako yuko pamoja nawe kila uendeko.
10 Then Joshua commanded the officers of the people, saying,
Kisha Yoshua akawaagiza viongozi wa watu,
11 Pass through the host, and command the people, saying, Prepare you provisions; for within three days ye shall pass over this Jordan, to go in to possess the land which the LORD your God giveth you to possess it.
“Nendeni katika kambi na waagizeni watu, 'andaeni chakula kwa ajili yenu. Baada ya siku tatu mtavuka mto huu wa Yordani na kuingia ndani na kuimiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi ili kuimiliki.””
12 And to the Reubenites, and to the Gadites, and to half the tribe of Manasseh, spoke Joshua, saying,
Yoshua akawaambia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
13 Remember the word which Moses the servant of the LORD commanded you, saying, The LORD your God hath given you rest, and hath given you this land.
“Kumbukeni maneno ambayo Musa, mtumishi wa Yahweh, aliwaaagiza aliposema, 'Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi pumziko, naye awapeni ninyi nchi hii.'
14 Your wives, your little ones, and your cattle shall remain in the land which Moses gave you on this side of Jordan; but ye shall pass before your brethren armed, all the mighty men of valor, and help them;
Wake zenu, na watoto wenu na mifugo yenu itakaa katika nchi ambayo Musa aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani. Lakini watu wenu wa vita wataenda pamoja na ndugu zao na kuwasaidia.
15 Until the LORD shall have given your brethren rest, as [he hath given] you, and they also have possessed the land which the LORD your God giveth them: then ye shall return to the land of your possession, and enjoy it, which Moses the LORD'S servant gave you on this side of Jordan towards the sun-rising.
Mpaka hapo Yahweh atakapowapa ndugu zenu pumziko kama alivyowapa ninyi. Na wao pia watamiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi. Kisha mtarudi katika nchi yenu na kuimiliki, nchi ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani, mahali pa mapambazuko ya jua.”
16 And they answered Joshua, saying, All that thou commandest us, we will do, and whithersoever thou sendest us, we will go.
Nao wakamjibu Yoshua, na kusema, “Mambo yote uliyotuagiza tutayafanya, na kila mahali utakapotutuma tutaenda.
17 According as we hearkened to Moses in all things, so will we hearken to thee: only the LORD thy God be with thee, as he was with Moses.
Tutakutii kama tulivyomtii Musa. Yahweh Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama aliyokuwa pamoja na Musa.
18 Every one that doth rebel against thy commandment, and will not hearken to thy words in all that thou commandest him, shall be put to death: only be strong and of a good courage.
Yeyote anayeasi maagizo yako na kutotii maneno yako atauawa. Uwe hodari na jasiri tu.

< Joshua 1 >