< John 20 >
1 The first [day] of the week cometh Mary Magdalene early, when it was yet dark, to the sepulcher, and seeth the stone taken away from the sepulcher.
Mapema siku ya kwanza ya juma, kungali bado giza, Mariamu Magdalena alikuja kaburini; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
2 Then she runneth, and cometh to Simon Peter, and to the other disciple whom Jesus loved, and saith to them, They have taken away the Lord out of the sepulcher, and we know not where they have laid him.
Kwa hiyo akakimbia mbio kwenda kwa Simon Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, kisha akawaambia, “wamemchukua Bwana kaburini, nasi hatujui kule walikomlaza.”
3 Peter therefore went forth, and that other disciple, and came to the sepulcher.
Kisha Petro na yule mwanafunzi mwingine wakatoka, kuelekea kaburini.
4 So they ran both together: and the other disciple outran Peter, and came first to the sepulcher.
Wote walipiga mbio kwa pamoja; yule mwanafunzi mwingine alikimbia kwa kasi zaidi ya Petro nakufika kaburini wa kwanza.
5 And he stooping down, saw the linen cloths lying; yet he went not in.
Akasimama na kisha kuangalia kaburini; akaiona ile sanda ya kitani imelala, lakini hakuingia ndani.
6 Then cometh Simon Peter following him, and went into the sepulcher, and seeth the linen cloths lying;
Kisha Simon Petro naye akafika akaingia ndani ya Kaburi. Akaiona ile sanda ya kitani imelala pale
7 And the napkin that was about his head, not lying with the linen cloths, but wrapped together in a place by itself.
na ile leso iliyokuwa kichwani pake haikuwa imelala pamoja na zile sanda za kitani bali ilikuwa imelala pembeni peke yake.
8 Then went in also that other disciple who came first to the sepulcher, and he saw, and believed.
Ndipo yule mwanafunzi mwingine naye alipoingia ndani ya kaburi; akaona na kuamini.
9 For as yet they knew not the scripture, that he must rise again from the dead.
Kwa kuwa hadi wakati huo walikuwa bado hawajayajua maandiko kwamba ilimlazimu Yesu afufuke tena katika wafu.
10 Then the disciples went away again to their own home.
Kisha wanafunzi wakaenda tena nyumbani kwao.
11 But Mary stood without at the sepulcher weeping: and as she wept she stooped down [to look] into the sepulcher,
Hata hivyo, Mariamu alikuwa amesimama kaburini akilia, alivyokuwa akiendelea kulia alisimama kisha akatazama kaburini.
12 And seeth two angels in white, sitting, the one at the head, and the other at the feet, where the body of Jesus had lain.
Akaona malaika wawili wenye sura nyeupe wamekaa mmoja kichwani na mwingine miguuni mahali ambapo Yesu alikuwa amelala.
13 And they say to her, Woman, why weepest thou? she saith to them, Because they have taken away my Lord, and I know not where they have laid him.
Nao wakamwambia, “Mwanamke, kwa nini unalia?” Naye akawaambia, “Ni kwa sababu wamemchukua Bwana wangu, nami sijui walikomweka.”
14 And when she had thus said, she turned herself about, and saw Jesus standing, and knew not that it was Jesus.
Alipokwisha sema hayo, aligeuka na kumwona Yesu akiwa amesimama. Lakini hakutambua kama huyo alikuwa Yesu.
15 Jesus saith to her, Woman, why weepest thou? whom seekest thou? She, supposing him to be the gardener, saith to him, Sir, if thou hast borne him hence, tell me where thou hast laid him, and I will take him away.
Naye Yesu akamwambia, “Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Naye huku akidhani kuwa ni mtunza bustani akamwambia, “Bwana, kama ni wewe uliyemchukua, niambie ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Jesus saith to her, Mary. She turned herself, and saith to him, Rabboni, which is to say, Master.
Yesu akamwambia, “Mariamu.” Naye akageuka mwenyewe na kumwambia kwa Kiaramu, “Raboni,” yaani hii ni kusema, “Mwalimu.”
17 Jesus saith to her, Touch me not: for I have not yet ascended to my Father: but go to my brethren, and say to them, I ascend to my Father and your Father, and [to] my God and your God.
Yesu akamwambia, “Usiniguse, kwani bado sijapaa kwenda kwa baba; bali uende kwa ndugu zangu ukawaambie kuwa nitapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye pia ni Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
18 Mary Magdalene came and told the disciples that she had seen the Lord, and [that] he had spoken these things to her.
Mariamu Magdalena akaja kuwaambia wanafunzi, “Nimemwona Bwana,” na kwamba amemwambia mambo haya.
19 Then the same day at evening, being the first [day] of the week, when the doors were shut where the disciples were assembled for fear of the Jews, Jesus came and stood in the midst, and saith to them, Peace [be] to you.
Na ilipokuwa jioni, siku hiyo, siku ya kwanza ya juma, na milango ikiwa imefungwa mahali wanafunzi walipokuwapo kwa kuwahofia Wayahudi, Yesu alikuja na kusimama katikati yao na kuwaambia, “Amani iwe kwenu.”
20 And when he had so said, he showed to them [his] hands and his side. Then were the disciples glad when they saw the Lord.
Alipokwisha sema haya akawaonesha mikono yake na ubavu wake. Nao wanafunzi walipomwona Bwana walifurahi.
21 Then said Jesus to them again, Peace [be] to you: as [my] Father hath sent me, even so I send you.
Kisha Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi. Kama vile Baba alivyonituma mimi, vivyo hivyo nami nawatuma ninyi.”
22 And when he had said this, he breathed on [them], and saith to them, Receive ye the Holy Spirit.
Yesu alipokwisha sema hayo, akawavuvia akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Whose soever sins ye remit, they are remitted to them; [and] whose soever [sins] ye retain, they are retained.
Yeyote mmsameheye dhambi, wamesamehewa; na wale mtakaowafungia watafungiwa.”
24 But Thomas, one of the twelve, called Didymus, was not with them when Jesus came.
Thomaso, mmoja wa wale kumi na wawili, aliyeitwa Didimas, hakuwa na wanafunzi wenzake Yesu alipokuja.
25 The other disciples therefore said to him, We have seen the Lord. But he said to them, Except I shall see in his hands the print of the nails, and put my finger into the print of the nails, and thrust my hand into his side, I will not believe.
Wale wanafunzi wengine waka mwambia baadaye, “Tumemwona Bwana.” Naye akawambia, “Kama sitaona alama za misumari katika mikono yake, na kuweka vidole vyangu kwenye hizo alama, na pia kuweka mkono wangu kwenye ubavu wake sitaamini.”
26 And after eight days again his disciples were within, and Thomas with them: [then] came Jesus, the doors being shut, and stood in the midst, and said, Peace [be] to you.
Baada ya siku nane wanafunzi walikuwa chumbani tena, naye Thomaso alikuwa pamoja nao. Wakati milango ilipokuwa imefungwa Yesu alisimama katikati yao. na akasema, “Amani na iwe nanyi.”
27 Then saith he to Thomas, Reach hither thy finger, and behold my hands; and reach hither thy hand, and thrust [it] into my side; and be not faithless, but believing.
Kisha akamwambia Thomaso, leta kidole chako na uone mikono yangu; leta hapa mikono yako na uweke kwenye ubavu wangu; wala usiwe asiyeamini bali aaminiye.”
28 And Thomas answered and said to him, My Lord and my God.
Naye Thomaso akajibu na kumwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu.”
29 Jesus saith to him, Thomas, because thou hast seen me, thou hast believed: blessed [are] they that have not seen, and [yet] have believed.
Yesu akamwambia, Kwa kuwa umeniona, umeamini. Wamebarikiwa wao wanaoamini, pasipokuona.”
30 And many other signs truly did Jesus in the presence of his disciples, which are not written in this book.
Kisha Yesu alifanya ishara nyingi mbele ya wanafunzi, ambazo hazijawahi kuandikwa katika kitabu hiki;
31 But these are written, that ye may believe that Jesus is the Christ, the Son of God, and that believing ye may have life through his name.
bali hizi zimeandikwa ili kwamba muweze kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo, mwana wa Mungu, na kwamba muaminipo muwe na uzima katika jina lake.