< John 13 >
1 Now before the feast of the passover, when Jesus knew that his hour was come that he should depart out of this world to the Father, having loved his own who were in the world, he loved them to the end.
Sasa kabla ya sikukuu ya pasaka, kwa sababu Yesu alifahamu kuwa saa yake imefika ambayo atatoka katika dunia hii kwenda kwa baba, akiwa amewapenda watu wake ambao walikuwa duniani, aliwapenda upeo.
2 And supper being ended (the devil having now put into the heart of Judas Iscariot, Simon's [son], to betray him; )
Na ibilisi alikuwa amewekwa tayari katika moyo wa Yuda Isikariote, mwana wa simoni, kumsaliti Yesu.
3 Jesus knowing that the Father had given all things into his hands, and that he had come from God, and was going to God;
Yesu alifahamu kuwa baba ameweka vitu vyote katika mikono yake na kwamba ametoka kwa Mungu na alikuwa anakwenda tena kwa Mungu.
4 He riseth from supper, and laid aside his garments; and took a towel, and girded himself.
Aliamka chakulani na akatandika chini vazi lake la nje. Kisha alichukua taulo na akajifunga mwenyewe.
5 After that, he poured water into a basin, and began to wash the disciples feet, and to wipe [them] with the towel with which he was girded.
Kisha akatia maji katika bakuli na akaanza kuwaosha miguu wanafunzi wake na kuwafuta na taulo ambayo alijifunga yeye mwenyewe.
6 Then he cometh to Simon Peter: and Peter saith to him, Lord, dost thou wash my feet?
Akaja kwa Simoni Petro, na Petro akamwambia, “Bwana, Unataka kuniosha miguu yangu?”
7 Jesus answered and said to him, What I do thou knowest not now; but thou shalt know hereafter.
Yesu akajibu na kumwambia, “Nifanyalo hulijui sasa, lakini utaelewa baadaye.”
8 Peter saith to him, Thou shalt never wash my feet. Jesus answered him, If I wash thee not, thou hast no part with me. (aiōn )
Petro akamwambia, “Hutaniosha miguu yangu kamwe.” Yesu akamjibu, “Ikiwa sitakuosha, hutakuwa na sehemu pamoja nami.” (aiōn )
9 Simon Peter saith to him, Lord, not my feet only, but also [my] hands and [my] head.
Simoni Petro akamwambia, “Bwana, usinioshe miguu yangu tuu, bali pia na mikono na kichwa changu.”
10 Jesus saith to him, He that is washed needeth not save to wash [his] feet, but is wholly clean: and ye are clean, but not all.
Yesu akamwambia, “Yeyote ambaye amekwisha kuoga haitaji kuoga isipokuwa miguu yake, na amekuwa safi mwili wake wote; ninyi mmekuwa safi, lakini si nyote.”
11 For he knew who would betray him; therefore said he, Ye are not all clean.
Kwa kuwa Yesu alijua yule atakaye msaliti; hii ndiyo sababu alisema, si nyote mmekuwa safi.”
12 So after he had washed their feet, and had taken his garments, and was set down again, he said to them, Know ye what I have done to you?
Wakati Yesu alipokuwa amewaosha miguu yao na akiisha chukua vazi lake na kukaa tena, aliwaambia, “Je Mnaelewa kile ambacho nimewafanyia?
13 Ye call me Master, and Lord: and ye say well; for [so] I am.
Mnaniita mimi “Mwalimu” na Bwana hii mnasema kweli, maana ndivyo nilivyo.
14 If I then, [your] Lord and Master, have washed your feet; ye also ought to wash one another's feet.
Ikiwa mimi Bwana na mwalimu, nimewaosha miguu yenu, ninyi pia imewapasa kuwaosha wenzenu miguu.
15 For I have given you an example, that ye should do as I have done to you.
Kwa kuwa nimewapa mfano ili kwamba ninyi pia mfanye kama mimi nilivyo fanya kwenu.
16 Verily, verily, I say to you, The servant is not greater than his lord; neither he that is sent greater than he that sent him.
Amini, Amini, nawambia, mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala yule ambaye ametumwa ni mkuu kuliko yule aliye mtuma.
17 If ye know these things, happy are ye if ye do them.
Ikiwa unafahamu mambo haya, umebarikiwa ukiyatenda.
18 I speak not of you all; I know whom I have chosen: but that the scripture may be fulfilled, He that eateth bread with me, hath lifted up his heel against me.
Sisemi kuhusu ninyi nyote, kwa kuwa nawajua wale ambao nimewachagua - bali nasema haya ili kwamba maandiko yaweze kutimilizwa: 'Yeye alaye mkate wangu ameniinulia kisigino chake.'
19 Now I tell you before it cometh, that when it hath come to pass, ye may believe that I am [he].
Ninawambia hili sasa kabla halijatokea ili kwamba litakapotokea, muweze kuamini kuwa mimi NDIYE.
20 Verily, verily, I say to you, He that receiveth whomsoever I send, receiveth me; and he that receiveth me, receiveth him that sent me.
“Amini, amini, nawambia, anipokeaye mimi humpokea ambaye nina mtuma, na yule anipokeaye mimi humpokea yule aliye nituma mimi.”
21 When Jesus had thus said, he was troubled in spirit, and testified, and said, Verily, verily, I say to you, that one of you will betray me.
Wakati Yesu aliposema haya, alisumbuka rohoni, alishuhudia na kusema, “Amini, amini, nawambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”
22 Then the disciples looked one on another, doubting of whom he spoke.
Wanafunzi wake wakatazamana, wakishangaa ni kwa ajili ya nani alizungumza.
23 Now there was leaning on Jesus' bosom, one of his disciples, whom Jesus loved.
Kulikuwa katika meza, mmoja wa wanafunzi wake ameegama kifuani mwa Yesu yule ambaye Yesu alimpenda.
24 Simon Peter therefore beckoned to him, to ask who it should be of whom he spoke.
Simoni Petro alimuuliza mwanafunzi huyu na kusema, “Twambie ni yupi ambaye kwake anazungumza.”
25 He then lying on Jesus' breast, saith to him, Lord, who is it?
Mwanafunzi yule aliye egama kifuani mwa Yesu na akamwambia, “Bwana, ni nani?”
26 Jesus answered, He it is to whom I shall give a sop, when I have dipped [it]. And when he had dipped the sop, he gave [it] to Judas Iscariot, [the son] of Simon.
Kisha Yesu alijibu, “Ni kwake yule nitakaye chovya kipande cha mkate na kumpatia.” Hivyo alipo kuwa amechovya mkate, alimpatia Yuda mwana wa Simon Iskariote.
27 And after the sop Satan entered into him. Then said Jesus to him, What thou doest, do quickly.
Na baada ya mkate, Shetani alimuingia. Kisha Yesu akamwambia, “Kile ambacho unataka kukifanya ukifanye haraka.”
28 Now no man at the table knew for what intent he spoke this to him.
Sasa hakuna mtu katika meza alijua sababu ya Yesu kusema jambo hili kwake.
29 For some [of them] thought, because Judas had the bag, that Jesus had said to him, Buy [those things] that we have need of against the feast; or, that he should give something to the poor.
Baadhi yao walidhani kwamba, kwa sababu Yuda alishika mfuko wa fedha, Yesu alimwambia, “Nunua vitu tunavyohitaji kwa ajili ya sikukuu,” au kwamba anapaswa kutoa kitu kwa masikini.
30 He then having received the sop, went immediately out: and it was night.
Baada ya Yuda kupokea mkate, alitoka nje harak; na ilikuwa usiku.
31 Therefore when he had gone out, Jesus said, Now is the Son of man glorified, and God is glorified in him.
Wakati Yuda alipokuwa ameondoka, Yesu alisema, “Sasa mwana wa Adam ametukuzwa, na Mungu ametukuzwa katika yeye.
32 If God is glorified in him, God will also glorify him in himself, and will immediately glorify him.
Mungu atamtukuza katika yeye mwenyewe, na atamtukuza haraka.
33 Little children, yet a little while I am with you. Ye will seek me: and, as I said to the Jews, Whither I go, ye cannot come; so now I say to you.
Watoto wadogo, niko pamoja nanyi kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama nilivyowambia Wayahudi, 'Niendako, hamuwezi kuja.' sasa nawambia ninyi, pia.
34 A new commandment I give to you, That ye love one another; as I have loved you, that ye also love one another.
Ninawapa amri mpya, kwamba mpendane; kama mimi nilivyo wapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi pia imewapasa kupendana ninyi kwa ninyi.
35 By this shall all [men] know that ye are my disciples, if ye have love one to another.
Kwa ajili ya hili watu watatambua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa mna upendo kwa kila mmoja na mwingine.”
36 Simon Peter said to him, Lord, whither goest thou? Jesus answered him, Whither I go, thou canst not follow me now; but thou shalt follow me afterward.
Simoni Petro alimwambia, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akajibu, “Mahali ninapokwenda kwa sasa hutaweza kunifuata, lakini utanifuata baadaye.”
37 Peter said to him, Lord, why cannot I follow thee now? I will lay down my life for thy sake.
Petro akamwambia, “Bwana, kwa nini nisikufuate hata sasa? Mimi nitayatoa maisha yangu kwa ajili yako.”
38 Jesus answered him, Wilt thou lay down thy life for my sake? Verily, verily, I say to thee, The cock will not crow, till thou hast denied me thrice.
Yesu akajibu, “Je utayatoa maisha yako kwa ajili yangu? Amini amini nakwambia, jogoo hatawika kabla hujanikana mara tatu.”