< Job 36 >
1 Elihu also proceeded, and said,
Elihu akaendelea kusema:
2 Suffer me a little, and I will show thee that [I have] yet to speak on God's behalf.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 I will bring my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Maker.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 For truly my words [shall] not [be] false: he that is perfect in knowledge [is] with thee.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 Behold, God [is] mighty, and despiseth not [any]: [he is] mighty in strength [and] wisdom.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 He preserveth not the life of the wicked: but giveth right to the poor.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 He withdraweth not his eyes from the righteous: but with kings [are they] on the throne; yes, he doth establish them for ever, and they are exalted.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 And if [they are] bound in fetters, [and] are held in cords of affliction;
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 Then he showeth them their work, and their transgressions that they have exceeded.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 He openeth also their ear to discipline, and commandeth that they return from iniquity.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 If they obey and serve [him], they shall spend their days in prosperity, and their years in pleasures.
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 But if they obey not, they shall perish by the sword, and they shall die without knowledge.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 But the hypocrites in heart heap up wrath: they cry not when he bindeth them.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 They die in youth, and their life [is] among the unclean.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 He delivereth the poor in his affliction, and openeth their ears in oppression.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 Even so would he have removed thee out of the strait [into] a broad place, where [there is] no straitness; and that which should be set on thy table [would be] full of fatness.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 But thou hast fulfilled the judgment of the wicked: judgment and justice take hold [on thee].
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Because [there is] wrath, [beware] lest he take thee away with [his] stroke: then a great ransom cannot deliver thee.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 Will he esteem thy riches? [no], not gold, nor all the forces of strength.
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 Desire not the night, when people are cut off in their place.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Take heed, regard not iniquity: for this hast thou chosen rather than affliction.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Behold, God exalteth by his power: who teacheth like him?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who hath enjoined him his way? or who can say, Thou hast wrought iniquity?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 Remember that thou magnify his work, which men behold.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 Every man may see it; man may behold [it] afar off.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 Behold, God [is] great, and we know [him] not, neither can the number of his years be searched out.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 For he maketh small the drops of water: they pour down rain according to the vapor of it.
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 Which the clouds do drop [and] distill upon man abundantly.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Also can [any] understand the spreadings of the clouds, [or] the noise of his tabernacle?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Behold, he spreadeth his light upon it, and covereth the bottom of the sea.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 For by them he judgeth the people; he giveth food in abundance.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 With clouds he covereth the light; and commandeth it [not to shine] by [the] intervening [cloud].
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 The noise of it showeth concerning it, the cattle also concerning the vapor.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.