< Job 30 >

1 But now [they that are] younger than I, have me in derision, whose fathers I would have disdained to set with the dogs of my flock.
Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
2 Yes, to what [might] the strength of their hands [profit] me, in whom old age had perished?
Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
3 For want and famine [they were] solitary; fleeing into the wilderness in former time desolate and waste.
Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
4 Who cut up mallows by the bushes, and juniper roots [for] their food.
Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
5 They were driven forth from among [men], (they cried after them, as [after] a thief; )
Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
6 To dwell in the clefts of the valleys, [in] caves of the earth, and [in] the rocks.
Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
7 Among the bushes they brayed; under the nettles they were collected.
Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
8 [They were] children of fools, yes, children of base men: they were viler than the earth.
Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
9 And now I am their song, yes, I am their by-word.
Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
10 They abhor me, they flee far from me, and spare not to spit in my face.
Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
11 Because he hath loosed my cord, and afflicted me, they have also let loose the bridle before me.
Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
12 Upon [my] right [hand] rise the youth; they push away my feet, and they raise up against me the ways of their destruction.
Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
13 They mar my path, they set forward my calamity, they have no helper.
Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
14 They came [upon me] as a wide breaking in [of waters]: in the desolation they rolled themselves [upon me].
Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
15 Terrors are turned upon me: they pursue my soul as the wind: and my welfare passeth away as a cloud.
Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
16 And now my soul is poured out upon me; the days of affliction have taken hold upon me.
Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
17 My bones are pierced in me in the night season: and my sinews take no rest.
Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
18 By the great force [of my disease] is my garment changed: it bindeth me about as the collar of my coat.
Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
19 He hath cast me into the mire, and I have become like dust and ashes.
Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
20 I cry to thee, and thou dost not hear me: I stand up, and thou regardest me [not].
Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
21 Thou hast become cruel to me: with thy strong hand thou opposest thyself against me.
Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
22 Thou liftest me up to the wind; thou causest me to ride [upon it], and dissolvest my substance.
Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
23 For I know [that] thou wilt bring me [to] death, and [to] the house appointed for all living.
Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
24 Yet he will not stretch out [his] hand to the grave, though they cry in his destruction.
Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
25 Did not I weep for him that was in trouble? was [not] my soul grieved for the poor?
Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
26 When I looked for good, then evil came: and when I waited for light, there came darkness.
Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
27 My bowels boiled, and rested not: the days of affliction came upon me.
Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
28 I went mourning without the sun: I stood up, [and] I cried in the congregation.
Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
29 I am a brother to dragons, and a companion to owls.
Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
30 My skin is black upon me, and my bones are burned with heat.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
31 My harp also is [turned] to mourning, and my organ into the voice of them that weep.
Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.

< Job 30 >