< Job 3 >
1 After this Job opened his mouth, and cursed his day.
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 And Job spoke, and said,
Kisha akasema:
3 Let the day perish in which I was born, and the night [in which] it was said, There is a man child conceived.
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Let that day be darkness; let not God regard it from above, neither let the light shine upon it.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 Let darkness and the shades of death stain it; let a cloud dwell upon it; let the blackness of the day terrify it.
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 As [for] that night, let darkness seize upon it; let it not be joined to the days of the year, let it not come into the number of the months.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 Lo, let that night be solitary, let no joyful voice come therein.
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 Let them curse it that curse the day, who are ready to raise up their mourning.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Let the stars of its twilight be dark; let it look for light, but [have] none; neither let it see the dawning of the day:
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 Because it prevented not my birth, nor hid sorrow from my eyes.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 Why died I not from the womb? [why] did I [not] expire at the time of my birth?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 Why did the knees receive me? or why the breasts that I should be nursed?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 For now should I have lain still and been quiet, I should have slept: then had I been at rest,
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 With kings and counselors of the earth, who built desolate places for themselves;
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 Or with princes that had gold, who filled their houses with silver:
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 Or as a hidden untimely birth I had not been; as infants [which] never saw light.
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 There the wicked cease [from] troubling; and there the weary are at rest.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 [There] the prisoners rest together; they hear not the voice of the oppressor.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 The small and great are there; and the servant [is] free from his master.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 Why is light given to him that is in misery, and life to the bitter [in] soul;
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 Who long for death, but it [cometh] not; and dig for it more than for hid treasures;
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 Who rejoice exceedingly, [and] are glad, when they can find the grave?
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 [Why is light given] to a man whose way is hid, and whom God hath hedged in?
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 For my sighing cometh before I eat, and my roarings are poured out like the waters.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 For the thing which I greatly feared hath come upon me, and that which I dreaded hath come to me.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 I was not in safety, neither had I rest, neither was I quiet; yet trouble came.
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”