< Jeremiah 5 >

1 Run ye to and fro through the streets of Jerusalem, and see now, and know, and seek in its broad places, if ye can find a man, if there is [any] that executeth judgment, that seeketh the truth; and I will pardon it.
Kimbieni mkapite katika mitaa ya Yerusalemu, Tafuteni katika viwanja vyake. Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja anayetenda kwa haki na kufanya kwa uaminifu, basi nitaisamehe Yerusalemu.
2 And though they say, The LORD liveth; surely they swear falsely.
Hata kama wanasema, 'Kama BWANA aishivyo,' wanaapa uongo.”
3 O LORD, [are] not thy eyes upon the truth? thou hast stricken them, but they have not grieved; thou hast consumed them, [but] they have refused to receive correction: they have made their faces harder than a rock; they have refused to return.
BWANA, macho yako hayatazami uaminifu? Unawapiga watu, lakini hawasikii maumivu. Umewaangsmiza kabisa, lakini bado wanakataa kuwa waadilifu. Wanafanya nyuso zao kuwa ngumu kama mwamba. kwa kuwa wanakataa kutubu.
4 Therefore I said, Surely these [are] poor; they are foolish: for they know not the way of the LORD, [nor] the judgment of their God.
Kwa hiyo nilisema, “Hakika hawa ni watu masikini, Ni wapumbavu, Kwa kuwa hawazijui njia za BWANA, wala maagizo ya Mungu wao.
5 I will go to the great men, and will speak to them; for they have known the way of the LORD, [and] the judgment of their God: but these have altogether broken the yoke, [and] burst the bonds.
Nitaenda kwa watu wa muhimu na kutangaza ujumbe wa Mungu kwao, kwa kuwa angalau wanazijua njia za BWANA, maagizo ya Mungu wao. Lakini wote wanavunja nira yao pamoja; wote wanaivunja ile minyororo inayowafunga kwa ajili ya Mungu.
6 Wherefore a lion from the forest shall slay them, [and] a wolf of the evenings shall spoil them, a leopard shall watch over their cities: every one that goeth out thence shall be torn in pieces: because their transgressions are many, [and] their backslidings are increased.
Kwa hiyo simba kutoka mwituni atawavamia. Mbweha kutoka Arabaha atawaangamiza. Chui ataivunja miji yao. Mtu yeyota anayeenda nje ya mji wake atavunjwavunjwa. Kwa kuwa maovu yao yameongezeka. Matendo yao ya uasi hayana ukomo.
7 How shall I pardon thee for this? thy children have forsaken me, and sworn by [them that are] no gods: when I had fed them to the full, then they committed adultery, and assembled themselves by troops in the harlots' houses.
Kwa nini niwasamehe hawa watu? Wana wenu wameniacha na wamefanya viapo na wale ambao si miungu. Niliwalisha vya kutosha, lakini wamefanya uasherati na kuchukua alama za nyumba ya uzinzi.
8 They were [as] fed horses in the morning: every one neighed after his neighbor's wife.
Walikuwa farasi wanaotafuta kupandwa. Walitembea huku na huku wakitafutwa kupandwa. Kila mwanamume alimkaribia mke wa jirani yake.
9 Shall I not visit for these [things]? saith the LORD: and shall not my soul be avenged on such a nation as this?
Kwa hiyo kwa nini nisiwaadhibu - asema BWANA - na kwa nini nisijilipizie kisasi juu ya taifa kama hili?
10 Go ye up upon her walls, and destroy; but make not a full end: take away her battlements; for they [are] not the LORD'S.
Nenda hadi kwenye kuta za shamba lake la mizabibu na zihariibuni. Lakini wao msiwaharibu kabisa. Ondoeni matawi kwa sababu hayatoki kwa BWANA.
11 For the house of Israel and the house of Judah have dealt very treacherously against me, saith the LORD.
Kwa sababu nyumba ya Yuda na Israeli wamenisaliti kabisa - asema BWANA -
12 They have belied the LORD, and said, [It is] not he; neither shall evil come upon us; neither shall we see sword nor famine:
na wamenikataa. Wanasema, ''Yeye si halisi. Maovu hayawezi kutupata, wala hatutaona upanga wala njaa.
13 And the prophets shall become wind, and the word [is] not in them: thus shall it be done to them.
Kwa kuwa manabii wamekuwa si kitu kama upepo na hakuna mtu mwiingine wa kunena ujumbe wa BWANA kwetu. Vitisho vyao na viwjie wao wenyewe.”'
14 Wherefore thus saith the LORD God of hosts, Because ye speak this word, Behold, I will make my words in thy mouth fire, and this people wood, and it shall devour them.
Kwa hiyo BWANA, Mungu wa majeshi asema hivi, tazama nataka kuweka maneno yangu katika kinywa chako. Yatakuwa kama moto na watu hawa watakuwa kama kuni! Kwa kuwa utawaramba.
15 Lo, I will bring a nation upon you from far, O house of Israel, saith the LORD: it [is] a mighty nation, it [is] an ancient nation, a nation whose language thou knowest not, neither understandest what they say.
Tazama nataka kuleta taifa dhidi yenu kutoka mbali, enyi nyumba ya Israeli - asema BWANA - ni taifa linalodumu, taifa la kale! Ni taifa ambalo lugha yake hamuijui, wala hamtaelewa wasemacho.
16 Their quiver [is] as an open sepulcher, they [are] all mighty men.
Podo lao ni kaburi wazi. Wote ni wanajeshi.
17 And they shall eat up thy harvest, and thy bread, [which] thy sons and thy daughters should eat: they shall eat up thy flocks and thy herds: they shall eat up thy vines and thy fig-trees: they shall impoverish with the sword thy fortified cities, in which thou hast trusted.
Kwa hiyo mavuno yako yataliwa, wana wako na binti zako pia, na chakula chako. Watakula kondoo wako na ng'ombe wako, watakula matunda ya zabibu zako na ya mitiini. Wataiangusha chini miji yenu na boma zake ambazo mnazitumainia.
18 Nevertheless in those days, saith the LORD, I will not make a full end with you.
Lakini hata katika siku hizo - asema BWANA - sikusudii kuwaharibu kabisa.
19 And it shall come to pass, when ye shall say, Why doeth the LORD our God all these [things] to us? then shalt thou answer them, As ye have forsaken me, and served strange gods in your land, so shall ye serve strangers in a land [that is] not yours.
Itatokea kwenu, ninyi Yuda na Israeli, mkisema, 'Kwa nini BWANA, Mungu wetu ametufanyia haya yote?' kwamba wewe Yeremia, utawaambia, 'Kama vile mlivyomwacha BWANA na kuabudu miungu mingine katika nchi yenu, vivyo hivyo mtawatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.'
20 Declare this in the house of Jacob, and publish it in Judah, saying,
Waambia haya watu wa nyumba ya Yakobo na yasikike katika Yuda. Waambie,
21 Hear now this, O foolish people, and without understanding; who have eyes, and see not; who have ears, and hear not:
'Sikilizeni hili, eny watu wapumbavu! Sanamu hazina matakwa; zina masikio lakini haziwawezi kusikia.
22 Fear ye not me? saith the LORD: will ye not tremble at my presence, who have placed the sand [for] the bound of the sea by a perpetual decree, that it cannot pass it: and though its waves toss themselves, yet can they not prevail; though they roar, yet can they not pass over it?
Je, hamnihofu mimi - asema BWANA - au kutetemeka mbele ya uso wangu? Nimeweka mpaka wa mchanga kwenye bahari, ambao ni agizo la kudumu ambalo halibomoki - hata kama bahari ina kupwa na kujaa, bado hauwenzi kubomoka. Hata kama mawimbi yake yanaunguruma, hayawezi kuvuka.
23 But this people have a revolting and a rebellious heart; they have revolted and gone.
Lakini hawa watu wana mioyo ya usumbufu. Hugeuka kuwa wapinzani na kuondoka.
24 Neither say they in their heart, Let us now fear the LORD our God, that giveth rain, both the former and the latter, in its season: he reserveth to us the appointed weeks of harvest.
Kwa kuwa hawasemi mioyoni mwao, “basi na tumche BWANA, Mungu wetu, yeye aletaye mvua za awali na mvua za vuli - kwa wakati wake, ambaye hutuzna majuma ya mavuno kwa ajili yetu.”
25 Your iniquities have turned away these [things], and your sins have withheld good [things] from you.
uovu wako umezuia haya yasitokee. Dhambi zako zimeyazuia mambo mema yasitokee.
26 For among my people are found wicked [men]: they lay wait, as he that setteth snares; they set a trap, they catch men.
Kwa watu waovu wamo kati ya watu wangu. Wanatazama kama mtu anayenyatia ili kukamata ndege; wanaweka mitego na kukamata watu;
27 As a cage is full of birds, so [are] their houses full of deceit: therefore they have become great, and have grown rich.
Kama tundu la mtego lijaavyo ndege, nyumba zao zimejaa uongo. Kwa hiyo wanakua na kutajirika.
28 They have become fat, they shine: yes, they surpass the deeds of the wicked: they judge not the cause, the cause of the fatherless, yet they prosper; and the right of the needy do they not judge.
Wamenenepa; wanang'aa na kupendeza. Wamepitiliza hata mipika ya maovu. Wala hawajali sababu ya kuwepo kwa watu na wala uwepo wa yatima. Wanafanikiwa hata kama hawatoi hukumu ya haki kwa yatima.
29 Shall I not visit for these [things]? saith the LORD: shall not my soul be avenged on such a nation as this?
Kwa nini nisiwadhibu kwa sababu ya haya - asema BWANA - sitajilipizia kisasi juu ya taifa la namna hii?
30 A wonderful and horrible thing is committed in the land;
Jambo la ajabu na la kuchukiza limetokea katika nchi hii.
31 The prophets prophesy falsely, and the priests bear rule by their means; and my people love [to have it] so: and what will ye do in the end thereof?
Mananbii wanatabiri kwa uongo, na makuhani wanatwala kwa msaada wa wa hao. Watu wangu wanapenda mambo ya hivyo, lakini mwisho kitatokea nini?

< Jeremiah 5 >