< Genesis 39 >

1 And Joseph was brought down to Egypt: and Potiphar, an officer of Pharaoh, captain of the guard, an Egyptian, bought him of the hands of the Ishmaelites, who had brought him down thither.
Yusufu akaletwa Misri. Potifa, aliyekuwa afisa wa Farao mkuu wa walinzi na Mmisri, akamnunua kutoka kwa Waishmaeli, waliokuwa wamempeleka pale.
2 And the LORD was with Joseph, and he was a prosperous man: and he was in the house of his master the Egyptian.
Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na akawa mtu aliyefanikiwa. Aliishi katika nyumba ya Mmisri bwana wake.
3 And his master saw that the LORD [was] with him, and that the LORD made all that he did to prosper in his hand.
Bwana wake akaona kwamba Yahwe alikuwa pamoja naye na kwamba Yahwe alifanikisha kila kitu alichokifanya.
4 And Joseph found grace in his sight, and he served him: and he made him overseer over his house, and all [that] he had he put into his hand.
Yusufu akapata kibali mbele zake. Akamtumikia Potifa. Potifa akamfanya msimamizi juu ya nyumba yake, na kila alichokimiliki, akakiweka chini ya uangalizi wake.
5 And it came to pass from the time [that] he had made him overseer in his house, and over all that he had, that the LORD blessed the Egyptian's house for Joseph's sake: and the blessing of the LORD was on all that he had in the house, and in the field.
Ikawa alipomfanya msimamizi juu ya nyumba yake na juu ya kila kitu alichomiliki, Yahwe akaibariki nyumba ya Mmisri kwa sababu ya Yusufu. Baraka za Yahwe zilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa nyumbani na shambani.
6 And he left all that he had in Joseph's hand; and he knew not aught he had, save the bread which he ate; and Joseph was [a] goodly [person], and well favored.
Potifa akaweka kila alichokuwa nacho chini ya uangalizi wa Yusufu. Hakuwa na haja ya kufikiri juu ya lolote isipokuwa chakula alichokula tu. Basi Yusufu alikuwa kijana mzuri na wa kuvutia.
7 And it came to pass after these things, that his master's wife cast her eyes upon Joseph: and she said, Lie with me.
Ikawa baada ya hayo mke wa bwana wake akamtamani Yusufu. Akamwambia, “Lala nami.”
8 But he refused, and said to his master's wife, Behold, my master knoweth not what [is] with me in the house, and he hath committed all that he hath to my hand:
Lakini yeye alikataa na kumwambia mke wa bwana wake, “Tazama, bwana wangu haangalii chochote nikifanyacho nyumbani, na ameweka kila kitu anachokimiliki chini ya uangalizi wangu.
9 [There is] none greater in his house than I; neither hath he kept back any thing from me but thee, because thou [art] his wife: how then can I do this great wickedness, and sin against God?
Hakuna mtu aliye mkuu katika nyumba hii kuliko mimi. Hajanidhuiria chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe ni mkewe. Ni kwa namna gani basi naweza kufanya uovu mkuu namna hii na kumtenda dhambi Mungu?
10 And it came to pass, as she spoke to Joseph day by day, that he hearkened not to her, to lie by her, [or] to be with her.
Akamwambia Yusufu siku baada ya siku, lakini yeye akakataa kulala naye wala kuwa naye.
11 And it came to pass, about this time, that [Joseph] went into the house to do his business; and [there was] none of the men of the house there within.
Ikawa siku moja aliingia ndani kufanya kazi yake. Hakuna mtu yeyote wa nyumbani aliyekuwepo pale ndani.
12 And she caught him by his garment, saying, Lie with me: and he left his garment in her hand, and fled, and went out.
Akashika nguo zake na kusema, “Lala nami.” Akaacha nguo zake mikononi mwake, akakimbia, na kutoka nje.
13 And it came to pass, when she saw that he had left his garment in her hand, and had fled forth,
Ikawa, alipoona kwamba ameziacha nguo zake mikononi mwake na kwamba amekimbia nje,
14 That she called to the men of her house, and spoke to them, saying, See, he hath brought in a Hebrew to us to mock us: he came in to me to lie with me, and I cried with a loud voice:
akawaita watu wa nyumbani mwake na kuwambia, “Tazama, Potifa ameleta Mwebrania huyu kutudhihaki. Aliingia kulala nami, na nikapiga kelele.
15 And it came to pass, when he heard that I raised my voice and cried, that he left his garment with me, and fled, and went out.
Ikawa aliponisikia nikipiga kelele, akaniacha na nguo yake, akakimbia, na kutoka nje.”
16 And she laid up his garment by her until his lord came home.
Akaweka nguo zake karibu naye hata bwana yake alipokuja nyumbani.
17 And she spoke to him according to these words, saying, The Hebrew servant, which thou hast brought to us, came in to me to mock me.
Akamwambia maelelezo haya, “Yule mtumishi Mwebrania uliyemleta kwetu, aliingia kunidhihaki.
18 And it came to pass, as I raised my voice and cried, that he left his garment with me, and fled.
Ikawa nilipopiga kelele, akaacha nguo yake kwangu akakimbia nje.”
19 And it came to pass, when his master heard the words of his wife, which she spoke to him, saying, After this manner did thy servant to me; that his wrath was kindled.
Ikawa, bwana wake aliposikia maelezo aliyoambiwa na mkewe, “Hivi ndivyo mtumishi wako alivyonitenda,” alikasirika sana.
20 And Joseph's master took him, and put him into the prison, a place where the king's prisoners [were] bound: and he was there in the prison.
Bwana wa Yusufu akamchukua na kumweka gerezani, mahali walipowekwa wafungwa wa mfalme. Akawa pale kifungoni.
21 But the LORD was with Joseph, and showed him mercy, and gave him favor in the sight of the keeper of the prison.
Lakini Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na kumwonyesha uaminifu wa agano. Akampa kibali mbele ya mlinzi wa gereza.
22 And the keeper of the prison committed to Joseph's hand all the prisoners that [were] in the prison; and whatever they did there, was done by him.
Mlinzi wa gereza akawaweka mikononi mwa Yusufu wafungwa wote waliokuwa gerezani. Chochote walichokifanya, kilikuwa chini ya uangalizi wa Yusufu.
23 The keeper of the prison looked not to any thing [that was] under his hand; because the LORD was with him: and [that] which he did the LORD made [it] to prosper.
Mlinzi wa gereza hakuwa na wasiwasi juu ya chochote kilichokuwa mkononi mwake, kwa sababu Yahwe alikuwa pamoja naye. Yahwe akafanikisha kila alichokifanya.

< Genesis 39 >