< Genesis 22 >
1 And it came to pass after these things, that God tempted Abraham, and said to him, Abraham: and he said, Behold, [here] I [am].
Ikawa kwamba baada ya mambo hayo Mungu akampima Abraham. Akamwambia, “Abraham!” Abraham akasema, “Mimi hapa.”
2 And he said, Take now thy son, thy only [son] Isaac, whom thou lovest, and go into the land of Moriah; and offer him there for a burnt-offering upon one of the mountains which I will name to thee.
Kisha Mungu akasema, “Mchukue mwanao, mwanao wa pekee, umpendaye, Isaka, na uende katika nchi ya Moria. Mtoe kama sadaka ya kuteketezwa mahali pale juu ya moja ya milima hiyo, ambayo nitakwambia.”
3 And Abraham rose early in the morning, and saddled his ass, and took two of his young men with him, and Isaac his son, and cleft the wood for the burnt-offering, and rose and went to the place which God had named to him.
Kwa hiyo Abraham akaamka asubuhi na mapema, akatandika punda wake, akawachukuwa vijana wake wawili, pamoja na Isaka mwanawe. Akakata kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, kisha akapanga safari kwenda mahali ambapo Mungu alimwambia.
4 Then on the third day Abraham lifted up his eyes, and saw the place afar off.
Siku ya tatu Abraham akatazama juu na akaona mahali pakiwa mbali.
5 And Abraham said to his young men, Abide you here with the ass, and I and the lad will go yonder and worship, and return to you.
Abraham akawambia vijana wake, “kaeni hapa pamoja na punda, mimi pamoja na Isaka tutakwenda pale. Tutaabudu na kisha tutarudi hapa penu.”
6 And Abraham took the wood of the burnt-offering, and laid [it] upon Isaac his son; and he took the fire in his hand, and a knife: and they went both of them together.
Ndipo Abraham akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa akaziweka juu ya Isaka mwanawe. Mkononi mwake akachukua moto na kisu; na wote wawili wakaondoka pamoja.
7 And Isaac spoke to Abraham his father, and said, My father: and he said, here [am] I, my son. And he said, Behold the fire and the wood: but where [is] the lamb for a burnt-offering?
Isaka akazungumza na Abraham baba yake akisema, “Baba yangu,” naye akasema, “Ndiyo mwanangu.” Akasema, “Tazama huu ni moto na kuni, lakini yuko wapi mwanakondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”
8 And Abraham said, My son, God will provide himself a lamb for a burnt-offering: so they went both of them together.
Abraham akasema, “Mungu mwenyewe atatupatia mwanakondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, mwanangu.” Kwa hiyo wakaendelea, wote wawili pamoja.
9 And they came to the place which God had named to him; and Abraham built an altar there, and laid the wood in order; and bound Isaac his son, and laid him on the altar upon the wood.
Walipofika mahali ambapo Mungu alikuwa amemwambia, Abraham akajenga madhabahu pale na akaweka kuni juu yake. Kisha akamfunga Isaka mwanawe, na akamlaza juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.
10 And Abraham stretched forth his hand, and took the knife to slay his son.
Abraham akanyoosha mkono wake akachukua kisu ili kumuua mwanawe.
11 And the angel of the LORD called to him from heaven, and said, Abraham, Abraham. And he said, Here [am] I.
Ndipo malaika wa Yahwe akamwita kutoka mbinguni na kusema, “Abraham, Abraham!” naye akasema, “Mimi hapa.”
12 And he said, Lay not thy hand upon the lad, neither do thou any thing to him: for now I know that thou fearest God, seeing thou hast not withheld from me thy son, thy only [son].
Akasema, “usinyooshe mkono wako juu ya kijana, wala usifanye jambo lolote kumdhuru, kwa kuwa sasa najua unamcha Mungu, kwa kuona kuwa hukumzuilia mwanao, mwanao wa pekee, kwa ajili yangu.”
13 And Abraham lifted up his eyes, and looked, and behold, behind [him] a ram caught in a thicket by his horns: And Abraham went and took the ram, and offered him for a burnt-offering in the stead of his son.
Abraham akatazama juu na tazama, nyuma yake kulikuwa na kondoo mume amenaswa pembe zake kichakani. Abraham akaenda akamchukua kondoo na akamtoa kama sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
14 And Abraham called the name of that place Jehovah-jireh: as it is said [to] this day, In the mount of the LORD it will be seen.
Kwa hiyo Abraham akapaita mahali pale, Yahwe atatoa,” na panaitwa hivyo hata leo. “Juu ya mlima wa Yahwe itatolewa.”
15 And the angel of the LORD called to Abraham from heaven the second time,
Malaika wa Yahwe akamwita Abraham kwa mara ya pili kutoka mbinguni
16 And said, By myself have I sworn, saith the LORD, for because thou hast done this thing, and hast not withheld thy son, thy only [son]:
na kusema - Hiki ni kiapo cha Yahwe, “Kwa ajili ya nafsi yangu nimeapa kwamba kwa kuwa umefanya jambo hili, na hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
17 That in blessing I will bless thee, and in multiplying I will multiply thy seed as the stars of heaven, and as the sand which [is] on the sea shore; and thy seed shall possess the gate of his enemies;
hakika nitakubariki na nitakuzidishia uzao wako kama nyota za angani, na kama mchanga ulioko kwenye ufukwe wa bahari; na uzao wakowatamiliki lango la adui zao.
18 And in thy seed shall all the nations of the earth be blessed: because thou hast obeyed my voice.
Kupitia uzao wako mataifa yote ya dunia watabarikiwa, kwa sababu umetii sauti yangu.”
19 So Abraham returned to his young men, and they rose and went together to Beer-sheba; and Abraham dwelt at Beer-sheba.
Kwa hiyo Abraham akarejea kwa vijana wake, na wakaondoka wakaenda pamoja Beerisheba, hivyo akakaa Beerisheba.
20 And it came to pass after these things, that it was told to Abraham, saying, Behold, Milcah, she hath also borne children to thy brother Nahor;
Ikawa kwamba baada ya mambo haya ambayo Abraham aliambiwa, “Milka amemzalia pia watoto, ndugu yako Nahori.”
21 Huz his first-born, and Buz his brother, and Kemuel the father of Aram,
Hawa walikuwa ni Usi mzaliwa wa kwanza, Busi ndugu yake, Kemueli aliye mzaa Aramu,
22 And Chesed, and Hazo, and Pildash, and Jidlaph, and Bethuel.
Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu, na Bethueli.
23 And Bethuel begat Rebekah: these eight Milcah bore to Nahor Abraham's brother.
Bethuel akamzaa Rebeka. Hawa walikuwa ni wale watoto wanane ambao Milka alizaa kwa Nahori, ndugu yake na Abraham.
24 And his concubine, whose name [was] Reumah, she bore also Tebah, and Gaham, and Thahash, and Maachah.
Suria wake, ambaye aliitwa Reuma, pia akamzaa Teba, Gahamu, Tahashi, na Maaka.