< Exodus 21 >
1 Now these [are] the judgments which thou shalt set before them.
“Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
2 If thou shalt buy a Hebrew servant, six years he shall serve: and in the seventh he shall depart free for nothing.
“Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
3 If he came in by himself, he shall depart by himself: if he was married, then his wife shall depart with him.
Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
4 If his master hath given him a wife, and she hath borne him sons or daughters; the wife and her children shall be her master's, and he shall depart by himself.
Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
5 And if the servant shall plainly say, I love my master, my wife, and my children; I will not depart free:
“Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
6 Then his master shall bring him to the judges; he shall also bring him to the door, or to the door-post: and his master shall bore his ear through with an awl; and he shall serve him for ever.
ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
7 And if a man shall sell his daughter to be a maid-servant, she shall not depart as the men-servants do.
“Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
8 If she shall not please her master, who hath betrothed her to himself, then shall he let her be redeemed: to sell her to a strange nation he shall have no power, seeing he hath dealt deceitfully with her.
Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
9 And if he hath betrothed her to his son, he shall deal with her after the manner of daughters.
Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
10 If he shall take him another [wife]; her food, her raiment, and her duty of marriage shall he not diminish.
Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
11 And if he shall not perform these three to her, then shall she depart free without money.
Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
12 He that smiteth a man, so that he dieth, shall be surely put to death.
“Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
13 And if a man shall not lie in wait, but God shall deliver [him] into his hand; then I will appoint thee a place whither he shall flee.
Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
14 But if a man shall come presumptuously upon his neighbor, to slay him with guile; thou shalt take him from my altar, that he may die.
Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
15 And he that smiteth his father, or his mother, shall be surely put to death.
“Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
16 And he that stealeth a man, and selleth him, or if he shall be found in his hand, he shall surely be put to death.
“Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
17 And he that curseth his father, or his mother, shall surely be put to death.
“Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
18 And if men contend together, and one shall smite another with a stone, or with [his] fist, and he shall not die, but keep [his] bed:
“Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
19 If he shall rise again, and walk abroad upon his staff, then shall he that smote [him] be quit: only he shall pay [for] the loss of his time, and shall cause [him] to be thoroughly healed.
yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
20 And if a man shall smite his servant, or his maid, with a rod, and he shall die under his hand; he shall be surely punished.
“Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
21 Notwithstanding, if he shall continue a day or two, he shall not be punished; for he [is] his money.
lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
22 If men shall contend, and hurt a woman with child, so that her fruit shall depart [from her], and yet no mischief follow: he shall be surely punished, according as the woman's husband will lay upon him; and he shall pay as the judges [determine].
“Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
23 And if [any] mischief shall follow, then thou shalt give life for life,
Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
24 Eye for eye, tooth for tooth, hand for hand, foot for foot,
jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
25 Burning for burning, wound for wound, stripe for stripe.
kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
26 And if a man shall smite the eye of his servant, or the eye of his maid, that it shall perish; he shall let him go free for his eye's sake.
“Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
27 And if he shall smite out his man-servant's tooth, or his maid-servant's tooth; he shall let him go free for his tooth's sake.
Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
28 If an ox shall gore a man or a woman, that they die: then the ox shall be surely stoned, and his flesh shall not be eaten; but the owner of the ox [shall be] quit.
“Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
29 But if the ox was accustomed to push with his horn in time past, and it hath been testified to his owner, and he hath not restrained him, but that he hath killed a man or a woman; the ox shall be stoned, and his owner also shall be put to death.
Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
30 If there shall be laid on him a sum of money, then he shall give for the ransom of his life whatever is laid upon him.
Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
31 Whether he hath gored a son, or hath gored a daughter, according to this judgment shall it be done to him.
Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
32 If the ox shall push a man-servant, or maid-servant; he shall give to their master thirty shekels of silver, and the ox shall be stoned.
Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
33 And if a man shall open a pit, or if a man shall dig a pit, and not cover it, and an ox or an ass shall fall into it;
“Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
34 The owner of the pit shall make compensation, [and] give money to the owner of them; and the dead [beast] shall be his.
mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
35 And if one man's ox shall hurt another's that he shall die, then they shall sell the live ox, and divide the money of it, and the dead [ox] also they shall divide.
“Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
36 Or if it shall be known that the ox hath used to push in time past, and his owner hath not restrained him; he shall surely pay ox for ox, and the dead shall be his own.
Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.