< Exodus 1 >
1 Now these [are] the names of the children of Israel, who came into Egypt; every man and his household came with Jacob.
Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli ambao walikwenda Misri na Yakobo, kila mmoja akiwa pamoja na jamaa yake:
2 Reuben, Simeon, Levi, and Judah,
Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
3 Issachar, Zebulun, and Benjamin,
Isakari, Zabuloni na Benyamini;
4 Dan, and Naphtali, Gad, and Asher.
Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
5 And all the souls that descended from Jacob, were seventy souls: for Joseph was in Egypt [already].
Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yosefu alikuwa tayari yuko Misri.
6 And Joseph died, and all his brethren, and all that generation.
Basi Yosefu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
7 And the children of Israel were fruitful, and increased abundantly, and multiplied, and became exceeding mighty; and the land was filled with them.
lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, kwa hiyo wakaijaza nchi.
8 Now there arose a new king over Egypt, who knew not Joseph.
Kisha mfalme mpya ambaye hakufahamu habari za Yosefu akatawala Misri.
9 And he said to his people, Behold, the people of the children of Israel [are] more and mightier than we.
Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kutuliko sisi.
10 Come, let us deal wisely with them: lest they multiply, and it shall come to pass, that when there falleth out any war, they will join with our enemies, and fight against us, and depart from the land.
Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana dhidi yetu na kuondoka katika nchi hii.”
11 Therefore they set over them task-masters, to afflict them with their burdens. And they built for Pharaoh treasure-cities, Pithom, and Raamses.
Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
12 But the more they afflicted them, the more they multiplied and grew. And they were grieved because of the children of Israel.
Lakini walivyozidi kuteswa ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi; Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
13 And the Egyptians made the children of Israel to serve with rigor.
kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
14 And they made their lives bitter with hard bondage, in mortar, and in brick, and in all manner of service in the field: all their service in which they made them serve, [was] with rigor.
Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
15 And the king of Egypt spoke to the Hebrew midwives (of which the name of one [was] Shiphrah, and the name of the other Puah: )
Mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kimisri waliowazalisha wanawake wa Kiebrania, ambao majina yao ni Shifra na Pua,
16 And he said, When ye do the office of a midwife to the Hebrew women, and see [them] upon the stools; if it [shall be] a son, then ye shall kill him; but if it [shall be] a daughter, then she shall live.
“Mtakapowazalisha wanawake wa Kiebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni, lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
17 But the midwives feared God, and did not as the king of Egypt commanded them, but saved the male-children alive.
Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
18 And the king of Egypt called for the midwives, and said to them, Why have ye done this thing, and have saved the male-children alive?
Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
19 And the midwives said to Pharaoh, Because the Hebrew women [are] not as the Egyptian women: for they [are] lively, and are delivered ere the midwives come in to them.
Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania ni tofauti na wanawake wa Kimisri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
20 Therefore God dealt well with the midwives: and the people multiplied, and became very mighty.
Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
21 And it came to pass, because the midwives feared God, that he made them houses.
Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
22 And Pharaoh charged all his people, saying, Every son that is born ye shall cast into the river, and every daughter ye shall save alive.
Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”