< Deuteronomy 8 >
1 All the commandments which I command thee this day shall ye observe to do, that ye may live, and multiply, and go in and possess the land which the LORD swore to your fathers.
Mnapaswa kuyashika maagizo yote ninayowapa leo, ili kwamba mweze kuishi na kuongezeka, na kuingia na kuimiliki nchi ambayo Yahwe aliaapa kwa baba zenu.
2 And thou shalt remember all the way which the LORD thy God hath led thee these forty years in the wilderness, to humble thee, [and] to prove thee, to know what [was] in thy heart, whether thou wouldst keep his commandments, or not.
Mtakumbuka akilini njia zote ambazo Yahwe Mungu amewaongoza miaka hii arobaini kwenye jangwa, ili kwamba apate kuwanyenyekeza, ili kwamba awajaribu kujua nini kilikuwa ndani ya mioyo yenu, kama mungeweza kuyashika maagizo yake au hapana.
3 And he humbled thee, and suffered thee to hunger, and fed thee with manna, which thou knewest not, neither did thy fathers know; that he might make thee know that man doth not live by bread only, but by every [word] that proceedeth out of the mouth of the LORD doth man live.
Aliwanyenyekeza, na kuwafanya kuwa na njaa, na kuwalisha manna, ambayo hamkuijua na ambayo baba zenu hawakuijua. Alifanya hivyo kuwafanya nyie kujua si kwa mkate tu watu wanaishi, badala ni kwa chochote hutoka kwenye kinywa cha Yahwe kwamba watu wanaishi.
4 Thy raiment hath not become old upon thee, neither hath thy foot swelled these forty years.
Mavazi yenu hayakuchanika na kudondoka, na miguu yenu haikuvimba kipindi cha miaka hiyo arobaini.
5 Thou shalt also consider in thy heart, that as a man chasteneth his son, [so] the LORD thy God chasteneth thee.
Mtatafakari katika mioyo yenu kuhusu, namna, kama mtu anavyo mwadibisha kijana wake, hivyo Yahwe Mungu wenu anawadibisha ninyi.
6 Therefore thou shalt keep the commandments of the LORD thy God, to walk in his ways, and to fear him.
Mtayashika maagizo ya Yahwe Mungu wenu, ili kwamba mweze kutembea katika njia zake na kumheshimu.
7 For the LORD thy God bringeth thee into a good land, a land of brooks of water, of fountains, and depths that spring out of valleys and hills;
Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi ya vijito vya maji, visima na chemchemi, vitiririkavyo kwenda kwenye mabonde na miongoni mwa milima,
8 A land of wheat, and barley, and vines, and fig-trees, and pomegranates, a land of olive-oil, and honey;
nchi ya ngano na shayiri, mizabibu, mtini, na komamanga; nchi mizeituni na asali.
9 A land in which thou shalt eat bread without scarceness, thou shalt not lack any [thing] in it, a land whose stones [are] iron, and out of whose hills thou mayest dig brass.
Ni nchi ambayo mtakula mkate bila kupungukiwa, na ambapo mtaenda bila chochote; nchi ambayo mawe yametengenezwa kwa chuma, na kutokana na milima mtaweze kuchimba shaba.
10 When thou hast eaten and art full, then thou shalt bless the LORD thy God for the good land which he hath given thee.
Mtakula na kushiba, na mtambariki Yahwe Mungu wenu kwa nchi nzuri ambayo amewapa.
11 Beware that thou forget not the LORD thy God, in not keeping his commandments, and his judgments, and his statutes, which I command thee this day:
Iweni makini kwamba msimsahau Yahwe Mungu wenu, na kwamba msipuuzie maagizo yake, hukumu zake, na sheria zake ambazo ninakuamuru leo,
12 Lest [when] thou hast eaten, and art full, and hast built goodly houses, and dwelt [in them];
vinginenyo unapokula na ukashiba, na wakati unajenga nyumba nzuri na kuishi ndani zao.
13 And [when] thy herds and thy flocks multiply, and thy silver and thy gold are increased, and all that thou hast is increased;
Na muwe makini wakati makundi yenu na mifugo yenu ikiongezeka, na wakati wa fedha zenu na dhahabu zenu zikiongezeka, na vyote mlivyonavyo kuongezeka,
14 Then thy heart shall be lifted up, and thou shalt forget the LORD thy God (who brought thee out of the land of Egypt, from the house of bondage; )
basi kwamba mioyo yenu iliniuliza juu ya kumsahau Yahwe Mungu wenu-aliyewaleta kutoka nchi ya Misri, toka nyumba ya utumwa.
15 Who led thee through that great and terrible wilderness, [in which were] fiery serpents, and scorpions, and drouth, where [there was] no water; who brought thee forth water out of the rock of flint;
Usimsahau yeye aliyewaongoza kupitia jangwa kuu na la kutisha, ambako ndani yake kulikuwa na nyoka wa moto na nge, na pitia nchi yenye kiu ambako hapakuwa na maji, ambaye yeye alileta maji toka kwenye mwamba wa jiwe.
16 Who fed thee in the wilderness with manna, which thy fathers knew not, that he might humble thee, and that he might prove thee, to do thee good at thy latter end.
Ambaye aliwalisha kwenye jangwa kwa manna ambayo mababu zenu hawakuijua, ili kwamba awajaribu, kufanya uzuri kwenu mwishoni-
17 And thou shalt say in thy heart, My power and the might of my hand hath gotten me this wealth.
lakini mnaweza kusema mioyoni mwenu, Nguvu yangu na mkono wangu wa uweza umepata utajiri huu wote.
18 But thou shalt remember the LORD thy God: for [it is] he that giveth thee power to get wealth, that he may establish his covenant which he swore to thy fathers, as [it is] this day.
Lakini mtamkumbuka akilini Yahwe Mungu wenu, kwa kuwa ni yeye awapae ninyi nguvu ya kupata utajiri, ili kwamba aweze kuanzisha agano lake aliloapa kwa baba zenu, kama ilivyo leo.
19 And it shall be, if thou shalt at all forget the LORD thy God, and walk after other gods, and serve them, and worship them, I testify against you this day that ye shall surely perish.
Itakuwa kwamba, kama mtamsahau Yahwe Mungu wenu na kuwaendea miungu mingine, kuibudu, na kuiheshimu, nashuhudia kinyume dhidi yenu leo kwamba mtateketea.
20 As the nations which the LORD destroyeth before your face, so shall ye perish; because ye would not be obedient to the voice of the LORD your God.
Kama mataifa ambayo Yahwe anatengeneza kuyaangamiza mbele yenu, hivyo mtaangamia, kwa sababu hamkusikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu.