< Acts 9 >

1 And Saul, yet breathing out threatenings and slaughter against the disciples of the Lord, went to the high priest,
Wakati huo Saulo alikuwa akizidisha vitisho vikali vya kuwaua wafuasi wa Bwana. Alikwenda kwa Kuhani Mkuu,
2 And desired from him letters to Damascus to the synagogues, that if he should find any of this way, whether they were men or women, he might bring them bound to Jerusalem.
akaomba apatiwe barua za utambulisho kwa masunagogi ya Kiyahudi kule Damasko, ili akikuta huko wanaume au wanawake wanaofuata Njia ya Bwana, awakamate na kuwaleta Yerusalemu.
3 And as he journeyed, he came near Damascus: and suddenly there shined around him a light from heaven:
Lakini alipokuwa njiani karibu kufika Damasko, ghafla mwanga kutoka angani ulimwangazia pande zote.
4 And he fell to the earth, and heard a voice saying to him, Saul, Saul, why persecutest thou me?
Akaanguka chini na kusikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?”
5 And he said, Who art thou, Lord? And the Lord said, I am Jesus whom thou persecutest. [It is] hard for thee to kick against the goads.
Naye Saulo akauliza, “Ni nani wewe Bwana?” Na ile sauti ikajibu, “Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
6 And he trembling and astonished said, Lord, what wilt thou have me to do? And the Lord [said] to him, Arise, and go into the city, and it shall be told thee what thou must do.
Lakini simama sasa, uingie mjini na huko utaambiwa unachopaswa kufanya.”
7 And the men who journeyed with him stood speechless, hearing a voice, but seeing no man.
Wale watu waliokuwa wanasafiri pamoja na Saulo walisimama pale, wakiwa hawana la kusema; walisikia ile sauti lakini hawakumwona mtu.
8 And Saul arose from the earth; and when his eyes were opened, he saw no man: but they led him by the hand, and brought [him] into Damascus.
Saulo aliinuka, na alipofumbua macho yake hakuweza kuona chochote; hivyo wale watu wakamwongoza kwa kumshika mkono mpaka mjini Damasko.
9 And he was three days without sight, and neither ate nor drank.
Saulo alikaa siku tatu bila kuona, na wakati huo hakula au kunywa chochote.
10 And there was a certain disciple at Damascus, named Ananias; and to him said the Lord in a vision, Ananias. And he said, Behold, I [am here], Lord.
Basi, huko Damasko kulikuwa na mfuasi mmoja aitwaye Anania. Bwana akamwambia katika maono, “Anania!” Anania akaitika, “Niko hapa, Bwana.”
11 And the Lord [said] to him, Arise, and go into the street which is called Straight, and inquire in the house of Judas for [one] called Saul of Tarsus: for behold, he prayeth,
Naye Bwana akamwambia, “Jitayarishe uende kwenye barabara inayoitwa Barabara ya Moja kwa Moja, na katika nyumba ya Yuda umtake mtu mmoja kutoka Tarso aitwaye Saulo. Sasa anasali;
12 And hath seen in a vision a man named Ananias, coming in, and putting [his] hand on him, that he might receive his sight.
na katika maono ameona mtu aitwaye Anania akiingia ndani na kumwekea mikono ili apate kuona tena.”
13 Then Ananias answered, Lord, I have heard by many of this man, how much evil he hath done to thy saints at Jerusalem:
Lakini Anania akajibu, “Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kutoka kwa watu wengi; nimesikia juu ya mabaya aliyowatendea watu wako huko Yerusalemu.
14 And here he hath authority from the chief priests, to bind all that call on thy name.
Na amekuja hapa akiwa na mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu kuwatia nguvuni wote wanaoomba kwa jina lako.”
15 But the Lord said to him, Go, for he is a chosen vessel to me, to bear my name before the Gentiles, and kings, and the children of Israel.
Lakini Bwana akamwambia, “Nenda tu, kwa maana nimemchagua awe chombo changu, alitangaze jina langu kwa mataifa na wafalme wao na kwa watu wa Israeli.
16 For I will show him how great things he must suffer for my name's sake.
Mimi mwenyewe nitamwonyesha mengi yatakayomlazimu kuteswa kwa ajili ya jina langu.”
17 And Ananias went, and entered into the house; and putting his hands on him, said, Brother Saul, the Lord ([even] Jesus that appeared to thee in the way as thou camest) hath sent me, that thou mayest receive thy sight, and be filled with the Holy Spirit.
Basi, Anania akaenda, akaingia katika hiyo nyumba. Kisha akaweka mikono yake juu ya Saulo, akasema, “Ndugu Saulo, Bwana ambaye ndiye Yesu mwenyewe aliyekutokea ulipokuwa njiani kuja hapa, amenituma ili upate kuona tena na kujazwa Roho Mtakatifu.”
18 And immediately there fell from his eyes as it had been scales: and he received sight forthwith, and arose, and was baptized.
Mara vitu kama magamba vikaanguka kutoka macho ya Saulo, akaweza kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
19 And when he had received food, he was strengthened. Then was Saul certain days with the disciples who were at Damascus.
Na baada ya kula chakula, nguvu zake zikamrudia. Saulo alikaa siku chache pamoja na wafuasi huko Damasko.
20 And immediately he preached Christ in the synagogues, that he is the Son of God.
Mara alianza kuhubiri katika masunagogi kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
21 But all that heard [him] were amazed, and said, Is not this he that destroyed them who called on this name in Jerusalem, and came hither for that intent, that he might bring them bound to the chief priests?
Watu wote waliomsikia walishangaa, wakasema, “Je, mtu huyu si yuleyule aliyewaua wale waliokuwa wanaomba kwa jina hili kule Yerusalemu? Tena alikuja hapa akiwa na madhumuni ya kuwatia nguvuni watu hao na kuwapeleka kwa makuhani!”
22 But Saul increased the more in strength, and confounded the Jews who dwelt at Damascus, proving that this is very Christ.
Saulo alizidi kupata nguvu, na kwa jinsi alivyothibitisha wazi kwamba Yesu ndiye Kristo, Wayahudi wa huko Damasko walivurugika kabisa.
23 And after many days were fulfilled, the Jews took counsel to kill him.
Baada ya siku nyingi kupita, Wayahudi walikusanyika na kufanya mpango wa kumwua Saulo.
24 But their laying in wait, was known to Saul. And they watched the gates day and night to kill him.
Lakini Saulo alipata habari ya mpango huo. Usiku na mchana walilinda milango ya kuingia mjini ili wapate kumwua.
25 Then the disciples took him by night, and let [him] down by the wall in a basket.
Lakini wakati wa usiku wanafunzi wake walimchukua, wakamteremsha chini ndani ya kapu kubwa kwa kupitia nafasi iliyokuwako ukutani.
26 And when Saul had come to Jerusalem, he essayed to join himself to the disciples: but they were all afraid of him, and believed not that he was a disciple.
Saulo alipofika Yerusalemu alijaribu kujiunga na wale wanafunzi. Lakini wote walimwogopa, na hawakuweza kuamini kwamba yeye amekuwa mfuasi.
27 But Barnabas took him, and brought [him] to the apostles, and declared to them how he had seen the Lord in the way, and that he had spoken to him, and how he had preached boldly at Damascus in the name of Jesus.
Hapo, Barnaba alikuja akamchukua Saulo, akampeleka kwa mitume na kuwaeleza jinsi Saulo alivyomwona Bwana njiani na jinsi Bwana alivyoongea naye. Aliwaambia pia jinsi Saulo alivyokuwa amehubiri bila uoga kule Damasko.
28 And he was with them coming in and going out at Jerusalem.
Basi, Saulo alikaa pamoja nao, akatembelea Yerusalemu yote akihubiri neno la Bwana bila hofu.
29 And he spoke boldly in the name of the Lord Jesus, and disputed against the Grecians: but they went about to slay him.
Pia aliongea na kubishana na Wayahudi wasemao Kigiriki, lakini wao walijaribu kumwua.
30 [Which] when the brethren knew, they brought him down to Cesarea, and sent him forth to Tarsus.
Wale ndugu walipogundua jambo hilo walimchukua Saulo, wakampeleka Kaisarea, wakamwacha aende zake Tarso.
31 Then had the churches rest throughout all Judea, and Galilee, and Samaria, and were edified: and walking in the fear of the Lord, and in the comfort of the Holy Spirit, were multiplied.
Wakati huo kanisa likawa na amani popote katika Yudea, Galilaya, na Samaria. Lilijengwa na kukua katika kumcha Bwana, na kuongezeka likitiwa moyo na Roho Mtakatifu.
32 And it came to pass, as Peter passed throughout all [quarters], he came down also to the saints who dwelt at Lydda.
Petro alipokuwa anasafirisafiri kila mahali alifika pia kwa watu wa Mungu waliokuwa wanaishi Luda.
33 And there he found a certain man named Eneas, who had kept his bed eight years, and was sick with the palsy.
Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Enea ambaye kwa muda wa miaka minane alikuwa amelala kitandani kwa sababu alikuwa amepooza.
34 And Peter said to him, Eneas, Jesus Christ healeth thee: arise, and make thy bed. And he arose immediately.
Basi, Petro akamwambia, “Enea, Yesu Kristo anakuponya. Amka utandike kitanda chako.” Enea akaamka mara.
35 And all that dwelt at Lydda and Saron saw him, and turned to the Lord.
Wakazi wote wa Luda na Saroni walimwona Enea, na wote wakamgeukia Bwana.
36 Now there was at Joppa a certain disciple named Tabitha, who by interpretation is called Dorcas: this woman was full of good works and alms-deeds which she did.
Kulikuwa na mfuasi mmoja mwanamke mjini Yopa aitwaye Tabitha (kwa Kigiriki ni Dorka, maana yake, Paa). Huyo mwanamke alikuwa akitenda mema na kuwasaidia maskini daima.
37 And it came to pass in those days, that she was sick, and died: whom, when they had washed, they laid in an upper chamber.
Wakati huo ikawa kwamba aliugua, akafa. Watu wakauosha mwili wake, wakauzika katika chumba ghorofani.
38 And as Lydda was nigh to Joppa, and the disciples had heard that Peter was there, they sent to him two men, desiring [him] that he would not delay to come to them.
Yopa si mbali sana na Luda; kwa hiyo wafuasi waliposikia kwamba Petro alikuwa Luda, wakawatuma watu wawili kwake na ujumbe: “Njoo kwetu haraka iwezekanavyo.”
39 Then Peter arose, and went with them. When he had come, they brought him into the upper chamber: and all the widows stood by him weeping, and showing the coats and garments which Dorcas made, while she was with them.
Basi, Petro akaenda pamoja nao. Alipofika alipelekwa ghorofani katika kile chumba. Huko wajane wengi walimzunguka Petro wakilia na kumwonyesha makoti na nguo ambazo Dorka alikuwa akitengeneza wakati alipokuwa hai.
40 But Peter put them all forth, and kneeled down, and prayed; and turning to the body, said, Tabitha, arise. And she opened her eyes: and when she saw Peter, she sat up.
Petro aliwatoa nje wote, akapiga magoti, akasali. Kisha akamgeukia yule maiti, akasema, “Tabitha, amka” Naye akafumbua macho yake na alipomwona Petro, akaketi.
41 And he gave her [his] hand, and lifted her up; and when he had called the saints and widows, presented her alive.
Petro akamsaidia kusimama, halafu akawaita wale watu wa Mungu na wale wajane, akamkabidhi kwao akiwa mzima.
42 And it was known throughout all Joppa: and many believed in the Lord.
Habari ya tukio hili ilienea kila mahali huko Yopa, na watu wengi wakamwamini Bwana.
43 And it came to pass, that he tarried many days in Joppa with one Simon a tanner.
Petro alikaa siku kadhaa huko Yopa, akiishi kwa mtu mmoja mtengenezaji wa ngozi aitwaye Simoni.

< Acts 9 >