< Acts 3 >
1 Now Peter and John went up together into the temple, at the hour of prayer, [being] the ninth [hour].
Siku moja, saa tisa alasiri, Petro na Yohane walikuwa wanakwenda Hekaluni, wakati wa sala.
2 And a certain man lame from his mother's womb was carried, whom they laid daily at the gate of the temple which is called Beautiful, to ask alms of them that entered into the temple.
Na pale karibu na mlango wa Hekalu uitwao “Mlango Mzuri”, palikuwa na mtu mmoja, kiwete tangu kuzaliwa. Watu walimbeba huyo mtu kila siku na kumweka hapo ili aombe chochote kwa wale waliokuwa wakiingia Hekaluni.
3 Who, seeing Peter and John about to go into the temple, asked an alms.
Alipowaona Petro na Yohane wakiingia Hekaluni, aliwaomba wampe chochote.
4 And Peter fastening his eyes upon him with John, said, Look on us.
Petro na Yohane walimkodolea macho, naye Petro akamwambia, “Tutazame!”
5 And he gave heed to them, expecting to receive something from them.
Naye akawageukia, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6 Then Peter said, Silver and gold have I none; but such as I have I give thee: in the name of Jesus Christ of Nazareth, rise up and walk.
Kisha Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu lakini kile nilicho nacho nitakupa. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
7 And he took him by the right hand, and lifted [him] up: and immediately his feet and ankle bones received strength.
Halafu, akamshika mkono wa kulia, akamwinua. Papo hapo miguu na magoti yake yakapata nguvu.
8 And he leaping up stood, and walked, and entered with them into the temple, walking, and leaping, and praising God.
Akaruka, akasimama na kuanza kutembea. Halafu akaingia pamoja nao Hekaluni, akitembea na kurukaruka huku akimtukuza Mungu.
9 And all the people saw him walking and praising God:
Watu wote waliokuwa hapo walimwona akitembea na kumsifu Mungu.
10 And they knew that it was he who sat for alms at the Beautiful gate of the temple: and they were filled with wonder and amazement at that which had happened to him.
Walipomtambua kuwa ndiye yule aliyekuwa anaombaomba karibu na ule “Mlango Mzuri” wa Hekalu, wakashangaa mno hata wasiweze kuelewa yaliyompata.
11 And as the lame man who was healed held Peter and John, all the people ran together to them in the porch that is called Solomon's, greatly wondering.
Watu wote, wakiwa na mshangao mkubwa wakaanza kukimbilia mahali palipoitwa “Ukumbi wa Solomoni,” ambapo yule mtu alikuwa bado anaandamana na Petro na Yohane.
12 And when Peter saw [it], he answered to the people, Ye men of Israel, why marvel ye at this? or why look ye so earnestly on us, as though by our own power or holiness we had made this man to walk?
Basi, Petro alipowaona watu hao akawaambia, “Wananchi wa Israeli, kwa nini mnashangazwa na jambo hili? Mbona mnatukodolea macho kana kwamba ni kwa nguvu zetu au utakatifu wetu sisi wenyewe tumemfanya mtu huyu aweze kutembea?
13 The God of Abraham, and of Isaac, and of Jacob, the God of our fathers hath glorified his Son Jesus; whom ye delivered up, and denied him in the presence of Pilate, when he was determined to let [him] go.
Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Yesu mtumishi wake. Yeye ndiye yuleyule mliyemtia mikononi mwa wakuu na kumkataa mbele ya Pilato hata baada ya Pilato kuamua kumwacha huru.
14 But ye denied the Holy One, and the Just, and desired a murderer to be granted to you,
Alikuwa mtakatifu na mwema; lakini ninyi mlimkataa, mkataka mtu mwingine aliyekuwa muuaji afunguliwe.
15 And killed the Prince of life, whom God hath raised from the dead; of which we are witnesses.
Basi, mlimuua yule ambaye ni chanzo cha uzima. Lakini Mungu alimfufua, na sisi ni mashahidi wa tukio hilo.
16 And his name, through faith in his name, hath made this man strong, whom ye see and know: yes, the faith which is by him, hath given him this perfect soundness in the presence of you all.
Jina la Yesu na imani katika jina hilo ndivyo vilivyompa nguvu mtu huyu mnayemwona na kumfahamu. Imani kwa Yesu ndiyo iliyomponya kabisa mtu huyu kama mnavyoona nyote.
17 And now, brethren, I know that through ignorance ye did [it], as [did] also your rulers.
“Sasa ndugu zangu, nafahamu kwamba ninyi na wakuu wenu mlitenda hayo kwa sababu ya kutojua kwenu.
18 But those things which God before had shown by the mouth of all his prophets, that Christ should suffer, he hath so fulfilled.
Lakini ndivyo Mungu alivyotimiza yale aliyotangaza zamani kwa njia ya manabii wote, kwamba ilikuwa lazima Kristo wake ateseke.
19 Repent ye therefore, and be converted, that your sins may be blotted out, when the times of refreshing shall come from the presence of the Lord,
Basi, tubuni mkamrudie Mungu ili afute dhambi zenu.
20 And he will send Jesus Christ, who before was preached to you:
Fanyeni hivyo ili Bwana awape nyakati za kuburudika rohoni na kuwaletea yule Kristo aliyemteua ambaye ndiye Yesu.
21 Whom the heaven must receive, until the times of restitution of all things, which God hath spoken by the mouth of all his holy prophets, since the world began. (aiōn )
Ni lazima yeye abaki huko mbinguni mpaka utakapofika wakati wa kurekebishwa vitu vyote, kama Mungu alivyosema kwa njia ya manabii wake watakatifu wa tangu zamani. (aiōn )
22 For Moses truly said to the fathers, A Prophet will the Lord your God raise up to you, of your brethren, like me; him shall ye hear in all things, whatever he shall say to you.
Kwa maana Mose alisema, Bwana Mungu wenu atawapelekeeni nabii kama mimi kutoka kati yenu ninyi wenyewe.
23 And it shall come to pass, [that] every soul who will not hear that Prophet, shall be destroyed from among the people.
Yeyote yule ambaye hatamsikiliza nabii huyo atatengwa mbali na watu wa Mungu na kuangamizwa.
24 And all the prophets also from Samuel, and those that follow, as many as have spoken, have likewise foretold these days.
Manabii wote, kuanzia Samweli na wale waliomfuata, walitangaza habari za mambo haya ambayo yamekuwa yakitendeka siku hizi.
25 Ye are the children of the prophets, and of the covenant which God made with our fathers, saying to Abraham, And in thy seed shall all the kindreds of the earth be blessed.
Ahadi zile Mungu alizotoa kwa njia ya manabii ni kwa ajili yenu; na mnashiriki lile agano Mungu alilofanya na babu zenu, kama alivyomwambia Abrahamu: Kwa njia ya wazawa wako, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.
26 To you first, God having raised up his Son Jesus, sent him to bless you, in turning away every one of you from his iniquities.
Basi, ilikuwa kwa ajili yenu kwanza kwamba Mungu alimfufua mtumishi wake, alimtuma awabariki kwa kumfanya kila mmoja wenu aachane kabisa na maovu yake.”