< Acts 21 >
1 And it came to pass, that after we were separated from them, and had lanched, we came with a straight course to Coos, and the [day] following to Rhodes, and from thence to Patara:
Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
2 And finding a ship sailing over to Phenicia, we went aboard, and set forth.
Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
3 Now when we had discovered Cyprus, we left it on the left hand, and sailed into Syria, and landed at Tyre: for there the ship was to unlade her burden.
Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
4 And finding disciples, we tarried there seven days: who said to Paul through the Spirit, that he should not go up to Jerusalem.
Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
5 And when we had accomplished those days, we departed, and proceeded on our way; and they all conducted us with wives and children, till [we were] out of the city; and we kneeled down on the shore, and prayed.
Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
6 And when we had taken our leave one of another, we took ship; and they returned home again.
Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
7 And when we had finished [our] course from Tyre, we came to Ptolemais, and saluted the brethren, and abode with them one day.
Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
8 And the next [day] we that were of Paul's company departed, and came to Cesarea; and we entered into the house of Philip the evangelist, who was [one] of the seven; and abode with him.
Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
9 And the same man had four daughters, virgins, who prophesied.
Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
10 And as we tarried [there] many days, there came down from Judea a certain prophet, named Agabus.
Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
11 And when he had come to us, he took Paul's girdle, and bound his own hands and feet, and said, Thus saith the Holy Spirit, So will the Jews at Jerusalem bind the man that owneth this girdle, and will deliver [him] into the hands of the Gentiles.
Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema “Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa.”
12 And when we heard these things, both we, and they of that place, besought him not to go up to Jerusalem.
Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
13 Then Paul answered, What mean ye to weep, and to break my heart? for I am ready not to be bound only, but also to die at Jerusalem for the name of the Lord Jesus.
Lakini yeye alijibu, “Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu.”
14 And when he would not be persuaded, we ceased, saying, The will of the Lord be done.
Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: “Mapenzi ya Bwana yafanyike”
15 And after those days we took up our furniture, and went up to Jerusalem.
Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
16 There went with us also [certain] of the disciples of Cesarea, and brought with them one Mnason of Cyprus, an old disciple, with whom we should lodge.
Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
17 And when we had come to Jerusalem, the brethren received us gladly.
Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
18 And the [day] following Paul went in with us to James: and all the elders were present.
Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
19 And when he had saluted them, he declared particularly what things God had wrought among the Gentiles by his ministry.
Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
20 And when they heard [it], they glorified the Lord, and said to him, Thou seest, brother, how many thousands of Jews there are who believe; and they are all zealous of the law:
Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
21 And they are informed concerning thee, that thou teachest all the Jews who are among the Gentiles to forsake Moses, saying, That they ought not to circumcise [their] children, neither to walk after the customs.
Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
22 What is it therefore? the multitude must needs come together: for they will hear that thou art come.
Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
23 Do therefore this that we say to thee: we have four men who have a vow on them;
Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
24 Take them, and purify thyself with them, and be at charges with them, that they may shave [their] heads: and all may know that those things of which they were informed concerning thee, are nothing; but [that] thou thyself also walkest orderly, and keepest the law.
Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
25 As concerning the Gentiles who believe, we have written [and] concluded that they observe no such thing, save only that they keep themselves from [things] offered to idols, and from blood, and from strangled, and from lewdness.
Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
26 Then Paul took the men, and the next day purifying himself with them, entered into the temple, to signify the accomplishment of the days of purification, until an offering should be offered for every one of them.
Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27 And when the seven days were almost ended, the Jews who were from Asia, when they saw him in the temple, stirred up all the people, and laid hands on him,
Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
28 Crying out, Men of Israel, help. This is the man that teacheth all [men] every where against the people, and the law, and this place: and further, hath brought Greeks also into the temple; and hath polluted this holy place.
wakipiga kelele: “Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu.”
29 (For they had seen before with him in the city, Trophimus, an Ephesian, whom they supposed that Paul had brought into the temple.)
Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
30 And all the city was moved, and the people ran together: and they took Paul and drew him out of the temple. And forthwith the doors were shut.
Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
31 And as they went about to kill him, tidings came to the chief captain of the band, that all Jerusalem was in an uproar.
Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
32 Who immediately took soldiers and centurions, and ran down to them. And when they saw the chief captain and the soldiers, they left beating Paul.
Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
33 Then the chief captain came near and took him, and commanded [him] to be bound with two chains: and inquired who he was, and what he had done.
Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, “Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?”
34 And some cried one thing, some another, among the multitude: and when he could not know the certainty for the tumult, he commanded him to be carried into the castle.
Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
35 And when he came upon the stairs, so it was that he was borne by the soldiers, for the violence of the people.
Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
36 For the multitude of the people followed, crying, Away with him.
Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, “Muulie mbali!”
37 And as Paul was to be led into the castle, he said to the chief captain, May I speak to thee? Who said, Canst thou speak Greek?
Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akamjibu, “Je unajua Kigiriki?
38 Art not thou that Egyptian, who before these days madest an uproar, and leddest out into the wilderness four thousand men that were murderers?
Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?”
39 But Paul said, I am a man [who am] a Jew of Tarsus, [a city] of Cilicia, a citizen of no mean city: and I beseech thee suffer me to speak to the people.
Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
40 And when he had given him license, Paul stood on the stairs, and beckoned with the hand to the people. And when there was made entire silence, he spoke to [them] in the Hebrew language, saying,
Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.