< Acts 13 >

1 Now there were in the church that was at Antioch certain prophets and teachers; as Barnabas, and Simeon that was called Niger, and Lucius of Cyrene, and Manaen, who had been brought up with Herod the tetrarch, and Saul.
Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
2 As they ministered to the Lord, and fasted, the Holy Spirit said, Separate for me Barnabas and Saul, for the work to which I have called them.
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
3 And when they had fasted and prayed, and laid [their] hands on them, they sent [them] away.
Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
4 So they being sent forth by the Holy Spirit, departed to Seleucia; and from thence they sailed to Cyprus.
Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
5 And when they were at Salamis, they preached the word of God in the synagogues of the Jews. And they had also John for [their] minister.
Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
6 And when they had gone through the isle to Paphos, they found a certain sorcerer, a false prophet, a Jew, whose name [was] Barjesus:
Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
7 Who was with the deputy of the country, Sergius Paulus, a prudent man; who called for Barnabas and Saul, and desired to hear the word of God.
Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
8 But Elymas the sorcerer (for so is his name by interpretation) withstood them, seeking to turn away the deputy from the faith.
Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
9 Then Saul (who also [is called] Paul) filled with the Holy Spirit, set his eyes on him,
Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
10 And said, O full of all subtilty, and all mischief, [thou] child of the devil, [thou] enemy of all righteousness, wilt thou not cease to pervert the right ways of the Lord?
na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
11 And now behold, the hand of the Lord [is] upon thee, and thou shalt be blind, not seeing the sun for a season. And immediately there fell on him a mist and a darkness; and he went about seeking some to lead him by the hand.
Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
12 Then the deputy, when he saw what was done, believed, being astonished at the doctrine of the Lord.
Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
13 Now when Paul and his company loosed from Paphos, they came to Perga in Pamphylia. And John departing from them, returned to Jerusalem.
Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
14 But when they departed from Perga, they came to Antioch in Pisidia, and went into the synagogue on the sabbath, and sat down.
Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
15 And after the reading of the law and the prophets, the rulers of the synagogue sent to them, saying, Men, brethren, if ye have any word of exhortation for the people, speak.
Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
16 Then Paul stood up, and beckoning with [his] hand, said, Men of Israel, and ye that fear God, give audience.
Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
17 The God of this people Israel chose our fathers, and exalted the people when they dwelt as strangers in the land of Egypt, and with a high arm he brought them out of it.
Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
18 And about the time of forty years he suffered their manners in the wilderness.
Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
19 And when he had destroyed seven nations in the land of Canaan, he divided their land to them by lot.
Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
20 And after that he gave [to them] judges, about the space of four hundred and fifty years, until Samuel the prophet.
Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
21 And afterward they desired a king: and God gave to them Saul the son of Kish, a man of the tribe of Benjamin, by the space of forty years.
Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
22 And when he had removed him, he raised up to them David to be their king: to whom also he gave testimony, and said, I have found David the [son] of Jesse, a man after my own heart, who shall fulfill all my will.
Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
23 Of this man's offspring hath God, according to [his] promise, raised up to Israel a Savior, Jesus:
Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
24 John having first preached, before his coming, the baptism of repentance to all the people of Israel.
Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
25 And as John fulfilled his course, he said, Whom think ye that I am? I am not [he]. But behold, there cometh one after me, whose shoes of [his] feet I am not worthy to loose.
Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
26 Men, brethren, children of the stock of Abraham, and whoever among you feareth God, to you is the word of this salvation sent.
Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
27 For they that dwell at Jerusalem, and their rulers, because they knew him not, nor yet the words of the prophets which are read every sabbath, they have fulfilled [them] in condemning [him].
Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
28 And though they found no cause of death [in him], yet they desired Pilate that he should be put to death.
Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
29 And when they had fulfilled all that was written concerning him, they took [him] down from the tree, and laid [him] in a sepulcher.
Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
30 But God raised him from the dead:
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 And he was seen many days by them who came up with him from Galilee to Jerusalem, who are his witnesses to the people.
Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
32 And we declare to you the glad tidings, that the promise which was made to the fathers,
Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
33 God hath fulfilled the same to us their children, in that he hath raised up Jesus again; as it is also written in the second psalm, Thou art my Son, this day have I begotten thee.
Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
34 And as concerning that he raised him from the dead, [now] no more to return to corruption, he said on this wise, I will give you the sure mercies of David.
Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
35 Wherefore he saith also in another [psalm], Thou wilt not suffer thy Holy One to see corruption.
Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
36 For David, after he had served his own generation by the will of God, fell asleep, and was laid to his fathers, and saw corruption:
Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
37 But he whom God raised again, saw no corruption.
Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
38 Be it known to you therefore, men, brethren, that through this man is preached to you the forgiveness of sins;
Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
39 And by him all that believe are justified from all things, from which ye could not be justified by the law of Moses.
Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
40 Beware therefore, lest that come upon you which is spoken in the prophets;
Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
41 Behold, ye despisers, and wonder, and perish: for I work a work in your days, a work which ye will in no wise believe, though a man declare it to you.
'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
42 And when the Jews had gone out of the synagogue, the Gentiles besought that these words might be preached to them the next sabbath.
Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
43 Now when the congregation was broken up, many of the Jews and religious proselytes followed Paul and Barnabas; who speaking to them, persuaded them to continue in the grace of God.
Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
44 And the next sabbath came almost the whole city together to hear the word of God.
Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
45 But when the Jews saw the multitudes, they were filled with envy, and spoke against those things which were uttered by Paul, contradicting and blaspheming.
Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
46 Then Paul and Barnabas became bold, and said, It was necessary that the word of God should first be spoken to you: but seeing ye reject it, and judge yourselves unworthy of everlasting life, lo, we turn to the Gentiles. (aiōnios g166)
Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios g166)
47 For so hath the Lord commanded us, [saying], I have set thee to be a light of the Gentiles, that thou shouldst be for salvation to the ends of the earth.
Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
48 And when the Gentiles heard this, they were glad, and glorified the word of the Lord: and as many as were ordained to eternal life, believed. (aiōnios g166)
Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios g166)
49 And the word of the Lord was published throughout all the region.
Neno la Bwana lilienea nchi yote.
50 But the Jews stirred up the devout and honorable women, and the chief men of the city, and raised persecution against Paul and Barnabas, and expelled them from their borders.
Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
51 But they shook off the dust of their feet against them, and came to Iconium.
Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
52 And the disciples were filled with joy and with the Holy Spirit.
Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.

< Acts 13 >