< 3 John 1 >

1 The elder to the well-beloved Gaius, whom I love in truth.
Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2 Beloved, I wish above all things that thou mayest prosper and be in health, even as thy soul prospereth.
Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
3 For I rejoiced greatly, when the brethren came and testified of the truth that is in thee, even as thou walkest in the truth.
Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
4 I have no greater joy than to hear that my children walk in truth.
Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
5 Beloved, thou doest faithfully whatever thou doest to the brethren, and to strangers;
Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
6 Who have borne testimony of thy charity before the church: whom if thou shalt bring forward on their journey after a godly sort, thou wilt do well:
Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
7 Because for his name's sake they went forth, taking nothing from the Gentiles.
Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
8 We therefore ought to receive such, that we may be fellow-helpers to the truth.
Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
9 I wrote to the church: but Diotrephes, who loveth to have the pre-eminence among them, receiveth us not.
Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
10 Wherefore, if I come, I will remember his deeds which he doeth, prating against us with malicious words: and not content with that, neither doth he himself receive the brethren, and forbiddeth them that would, and casteth [them] out of the church.
Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
11 Beloved, follow not that which is evil, but that which is good. He that doeth good is of God: but he that doeth evil hath not seen God.
Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12 Demetrius hath good report by all [men], and by the truth itself: and we [also] bear testimony; and ye know that our testimony is true.
Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
13 I had many things to write, but I will not with ink and pen write to thee:
Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
14 But I trust I shall shortly see thee, and we shall speak face to face. Peace [be] to thee. [Our] friends salute thee. Greet the friends by name.
Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.

< 3 John 1 >