< 2 Corinthians 11 >

1 I earnestly wish ye could bear with me a little in [my] folly: and indeed bear with me.
Laiti mngenivumilia kidogo, hata kama mimi ni mjinga kiasi fulani! Naam, nivumilieni kidogo.
2 For I am jealous over you with godly jealousy: for I have espoused you to one husband, that I may present [you as] a chaste virgin to Christ.
Ninawaoneeni wivu lakini ni wivu wa Mungu; maana ninyi ni kama bikira safi niliyemposa kwa mwanamume mmoja tu ambaye ndiye Kristo.
3 But I fear, lest by any means, as the serpent beguiled Eve through his subtilty, so your minds should be corrupted from the simplicity that is in Christ.
Lakini naogopa kwamba, kama vile yule nyoka kwa hila zake za uongo alimdanganya Hawa, fikira zenu zaweza kupotoshwa, mkauacha uaminifu wenu wa kweli kwa Kristo.
4 For if he that cometh preacheth another Jesus, whom we have not preached, or [if] ye receive another spirit, which ye have not received, or another gospel, which ye have not accepted, ye might well bear with [him].
Maana mtu yeyote ajaye na kumhubiri Yesu aliye tofauti na yule tuliyemhubiri, ninyi mwampokea kwa mikono miwili; au mnakubali roho au habari njema tofauti kabisa na ile mliyopokea kutoka kwetu!
5 For I suppose I was not a whit behind the very greatest apostles.
Sidhani kwamba mimi ni mdogo kuliko hao “mitume wakuu.”
6 But though [I am] rude in speech, yet not in knowledge; but we have been thoroughly made manifest among you in all things.
Labda sina ufasaha wa lugha, lakini elimu ninayo; jambo hili tumelionyesha wazi kwenu, kila mahali na kila wakati.
7 Have I committed an offense in abasing myself that ye might be exalted, because I have preached to you the gospel of God without reward?
Mimi niliihubiri kwenu Habari Njema ya Mungu bila kudai mshahara; nilijinyenyekeza ili nipate kuwakweza ninyi. Je, nilifanya vibaya?
8 I robbed other churches, taking wages [of them], to do you service.
Nilipofanya kazi kati yenu, mahitaji yangu yaligharimiwa na makanisa mengine. Kwa namna moja au nyingine niliwapokonya wao mali yao nipate kuwatumikia ninyi.
9 And when I was present with you, and wanted, I was chargeable to no man: for that which was lacking to me the brethren who came from Macedonia supplied: and in all [things] I have kept myself from being burdensome to you, and [so] will I keep [myself].
Nilipokuwa nanyi sikumsumbua mtu yeyote nilipohitaji fedha; ndugu waliotoka Makedonia waliniletea kila kitu nilichohitaji. Nilikuwa mwangalifu sana nisiwe mzigo kwa namna yoyote ile, na nitaendelea kufanya hivyo.
10 As the truth of Christ is in me, no man shall stop me of this boasting in the regions of Achaia.
Naahidi kwa ule ukweli wa Kristo ulio ndani yangu, kwamba hakuna kitakachoweza kunizuia kujivunia jambo hilo popote katika Akaya.
11 Why? because I love you not? God knoweth.
Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu eti siwapendi ninyi? Mungu anajua kwamba nawapenda!
12 But what I do, that I will do, that I may cut off occasion from them who desire occasion; that in what they glory, they may be found even as we.
Nitaendelea kufanya kama ninavyofanya sasa, ili nisiwape nafasi wale wanaotafuta nafasi, nafasi ya kujivuna kwamba eti wanafanya kazi kama sisi.
13 For such [are] false apostles, deceitful workers, transforming themselves into the apostles of Christ.
Maana, hao ni mitume wa uongo, wafanyakazi wadanganyifu wanojisingizia kuwa mitume wa Kristo.
14 And no wonder; for Satan himself is transformed into an angel of light.
Wala si ajabu, maana hata Shetani mwenyewe hujisingizia kuwa malaika wa mwanga!
15 Therefore [it is] no great thing if his ministers also are transformed as the ministers of righteousness; whose end shall be according to their works.
Kwa hiyo si jambo la kushangaza ikiwa na hao watumishi wake wanajisingizia kuwa watumishi wa haki. Mwisho wao watapata kile wanachostahili kufuatana na matendo yao.
16 I say again, Let no man think me a fool; if otherwise, yet as a fool receive me, that I may boast myself a little.
Tena nasema: Mtu asinifikirie kuwa mpumbavu. Lakini kama mkifikiri hivyo, basi, nichukueni kama mpumbavu ili nami nipate kuwa na cha kujivunia angaa kidogo.
17 That which I speak, I speak [it] not according to the Lord, but as it were foolishly, in this confidence of boasting.
Ninachosema sasa si kile alichoniagiza Bwana; kuhusu jambo hili la kujivuna, nasema tu kama mtu mpumbavu.
18 Seeing that many glory after the flesh, I will glory also.
Maadam wengi hujivuna kwa sababu za kidunia, nami pia nitajivuna.
19 For ye suffer fools gladly, seeing ye [yourselves] are wise.
Ninyi ni wenye busara, ndiyo maana hata mnawavumilia wapumbavu!
20 For ye suffer, if a man bringeth you into bondage, if a man devoureth [you], if a man taketh [from you], if a man exalteth himself, if a man smiteth you on the face.
Mnamvumilia hata mtu anayewafanya ninyi watumwa, mtu mwenye kuwanyonya, mwenye kuwakandamiza, mwenye kuwadharau na kuwapiga usoni!
21 I speak as concerning reproach, as though we had been weak. But in whatever respect any is bold, (I speak foolishly) I am bold also.
Kwa aibu nakubali kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Iwe iwavyo, lakini kama kuna mtu yeyote anayethubutu kujivunia kitu—nasema kama mtu mpumbavu—mimi nathubutu pia.
22 Are they Hebrews? so [am] I. Are they Israelites? so [am] I. Are they the offspring of Abraham? so [am] I.
Je, wao ni Waebrania? Hata mimi. Je, wao ni Waisraeli? Hata mimi. Wao ni wazawa wa Abrahamu? Hata mimi.
23 Are they ministers of Christ? (I speak as a fool) I [am] more; in labors more abundant, in stripes above measure, in prisons more frequent, in deaths often.
Wao ni watumishi wa Kristo? Hata mimi—nanena hayo kiwazimu—ni mtumishi wa Kristo zaidi kuliko wao. Mimi nimefanya kazi ngumu zaidi, nimekaa gerezani mara nyingi zaidi, nimepigwa mara nyingi zaidi na nimekaribia kifo mara nyingi.
24 From the Jews five times I received forty [stripes] save one.
Mara tano nilichapwa vile viboko thelathini na tisa vya Wayahudi.
25 Thrice was I beaten with rods, once I was stoned, thrice I suffered shipwreck, a night and a day I have been in the deep;
Nilipigwa viboko mara tatu, nilipigwa mawe mara moja; mara tatu nilivunjikiwa meli baharini, na humo nikakesha usiku kucha na kushinda mchana kutwa.
26 [In] journeyings often, [in] perils of waters, [in] perils of robbers, [in] perils by [my own] countrymen, [in] perils by the heathen, [in] perils in the city, [in] perils in the wilderness, [in] perils in the sea, [in] perils among false brethren;
Kila mara safarini nimekabiliwa na hatari za mafuriko ya mito, na hatari za wanyama; hatari kutoka kwa wananchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine; hatari za mjini, hatari za porini, hatari za baharini, hatari kutoka kwa ndugu wa uongo
27 In weariness and painfulness, in watchings often, in hunger and thirst, in fastings often, in cold and nakedness.
Nimefanya kazi na kutaabika, nimekesha bila usingizi mara nyingi; nimekuwa na njaa na kiu; mara nyingi nimefunga na kukaa katika baridi bila nguo.
28 Besides those things that are without, that which cometh upon me daily, the care of all the churches.
Na, licha ya mengine mengi, kila siku nakabiliwa na shughuli za makanisa yote.
29 Who is weak, and I am not weak? who is made to fall into sin, and I burn not?
Kama mtu yeyote ni dhaifu, nami pia ni dhaifu; mtu yeyote akikwazwa, nami pia huwa na wasiwasi.
30 If I must needs glory, I will glory of the things which concern my infirmities.
Ikinilazimu kujivuna, basi, nitajivunia udhaifu wangu.
31 The God and Father of our Lord Jesus Christ, who is blessed for evermore, knoweth that I lie not. (aiōn g165)
Mungu na Baba wa Bwana Yesu—jina lake litukuzwe milele—yeye anajua kwamba sisemi uongo. (aiōn g165)
32 In Damascus the governor under Aretas the king kept the city of the Damascenes with a garrison, desirous to apprehend me:
Nilipokuwa Damasko, mkuu wa mkoa, aliyekuwa chini ya mfalme Areta, alikuwa akiulinda mji wa Damasko ili apate kunikamata.
33 And through a window in a basket I was let down by the wall, and escaped his hands.
Lakini, ndani ya kapu kubwa, niliteremshwa nje kupitia katika nafasi ukutani, nikachopoka mikononi mwake.

< 2 Corinthians 11 >