< 1 Chronicles 16 >

1 So they brought the ark of God, and set it in the midst of the tent that David had pitched for it: and they offered burnt-sacrifices and peace-offerings before God.
Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
2 And when David had made an end of offering the burnt-offerings and the peace-offerings, he blessed the people in the name of the LORD.
Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
3 And he dealt to every one of Israel, both man and woman, to every one a loaf of bread, and a good piece of flesh, and a flagon [of wine].
Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
4 And he appointed [certain] of the Levites to minister before the ark of the LORD, and to record, and to thank and praise the LORD God of Israel:
Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
5 Asaph the chief, and next to him Zechariah, Jeiel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Mattithiah, and Eliab, and Benaiah, and Obed-edom: and Jeiel with psalteries and with harps; but Asaph made a sound with cymbals;
Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
6 Benaiah also and Jahaziel the priests with trumpets continually before the ark of the covenant of God.
nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
7 Then on that day David delivered first [this psalm] to thank the LORD into the hand of Asaph and his brethren.
Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
8 Give thanks to the LORD, call upon his name, make known his deeds among the people.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
9 Sing to him, sing psalms to him, talk ye of all his wonderous works.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
10 Glory ye in his holy name: let the heart of them rejoice that seek the LORD.
Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
11 Seek the LORD and his strength, seek his face continually.
Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
12 Remember his wonderful works that he hath done, his wonders, and the judgments of his mouth;
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
13 O ye seed of Israel his servant, ye children of Jacob, his chosen ones.
enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14 He [is] the LORD our God; his judgments [are] in all the earth.
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
15 Be ye mindful always of his covenant; the word [which] he commanded to a thousand generations;
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
16 [Even of the covenant] which he made with Abraham, and of his oath to Isaac;
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17 And which he confirmed to Jacob for a law, [and] to Israel [for] an everlasting covenant,
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
18 Saying, To thee will I give the land of Canaan, the lot of your inheritance;
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
19 When ye were but few, even a few, and strangers in it.
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
20 And [when] they went from nation to nation, and from [one] kingdom to another people;
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
21 He suffered no man to do them wrong: yea, he reproved kings for their sakes,
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
22 [Saying], Touch not my anointed, and do my prophets no harm.
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
23 Sing to the LORD, all the earth; show forth from day to day his salvation.
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
24 Declare his glory among the heathen; his wonderful works among all nations.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
25 For great [is] the LORD, and greatly to be praised: he also [is] to be feared above all gods.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
26 For all the gods of the people [are] idols: but the LORD made the heavens.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
27 Glory and honor [are] in his presence; strength and gladness [are] in his place.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
28 Give to the LORD, ye kindreds of the people, give to the LORD glory and strength.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
29 Give to the LORD the glory [due] to his name: bring an offering, and come before him: worship the LORD in the beauty of holiness.
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
30 Fear before him, all the earth: the world also shall be stable, that it be not moved.
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
31 Let the heavens be glad, and let the earth rejoice: and let [men] say among the nations, The LORD reigneth.
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
32 Let the sea roar, and the fullness thereof: let the fields rejoice, and all that [is] therein.
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
33 Then shall the trees of the wood sing at the presence of the LORD, because he cometh to judge the earth.
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
34 O give thanks to the LORD; for [he is] good; for his mercy [endureth] for ever.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
35 And say ye, Save us, O God of our salvation, and gather us together, and deliver us from the heathen, that we may give thanks to thy holy name, [and] glory in thy praise.
Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
36 Blessed [be] the LORD God of Israel for ever and ever. And all the people said, Amen, and praised the LORD.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
37 So he left there before the ark of the covenant of the LORD Asaph and his brethren, to minister before the ark continually, as every day's work required:
Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
38 And Obed-edom with their brethren, sixty and eight; Obed-edom also the son of Jeduthun and Hosah [to be] porters:
Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
39 And Zadok the priest, and his brethren the priests, before the tabernacle of the LORD in the high place that [was] at Gibeon,
Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
40 To offer burnt-offerings to the LORD upon the altar of the burnt-offering continually morning and evening, and [to do] according to all that is written in the law of the LORD, which he commanded Israel;
ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
41 And with them Heman and Jeduthun, and the rest that were chosen, who were expressed by name, to give thanks to the LORD, because his mercy [endureth] for ever;
Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
42 And with them Heman and Jeduthun with trumpets and cymbals for those that should make a sound, and with musical instruments of God. And the sons of Jeduthun [were] porters.
Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
43 And all the people departed every man to his house: and David returned to bless his house.
Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.

< 1 Chronicles 16 >