< Romans 6 >
1 What shall we say then? Shall we continue in sin, that grace may abound?
Tuseme nini basi? Tuendelee katika dhambi ili neema iongezeke?
2 By no means. How shall we, that are dead to sin, live any longer in it?
La hasha. Sisi tuliokufa katika dhambi, tunawezaje tena kuishi katika hiyo?
3 Know ye not, that so many of us as were baptized into Jesus Christ were baptized into his death?
Je hamjui ya kuwa wale waliobatizwa katika Kristo walibatizwa katika mauti yake?
4 Therefore we are buried with him by baptism into death: that as Christ was raised from the dead by the glory of the Father, even so we also should walk in newness of life.
Tulikuwa tumezikwa pamoja naye kupitia ubatizo katika kifo. Hii ilifanyika ili kwamba kama vile Kristo alivyoinuliwa kutoka mauti kupitia utukufu wa Baba, ili kwamba nasi tuweze kutembea katika upya wa maisha.
5 For if we have been planted together in the likeness of his death, we shall be also in the likeness of his resurrection:
Maana ikiwa tumeunganishwa pamoja naye katika mfano wa kifo chake, pia tutaunganishwa katika ufufuo wake.
6 Knowing this, that our old man is crucified with him, that the body of sin may be destroyed, that henceforth we should not serve sin.
Sisi tunajua hivi, utu wetu wa zamani ulisulubiwa pamoja naye, ili kwamba mwili wa dhambi uharibiwe. Hii ilitokea ili kwamba tusiendelee kuwa watumwa wa dhambi.
7 For he that is dead is freed from sin.
Yeye aliyekufa amefanywa mwenye haki kulingana na dhambi.
8 Now if we are dead with Christ, we believe that we shall also live with him:
Lakini kama tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pamoja naye pia.
9 Knowing that Christ being raised from the dead dieth no more; death hath no more dominion over him.
Tunajua kwamba Kristo amefufuliwa kutoka katika wafu, na kwamba si mfu tena. Kifo hakimtawali tena.
10 For in that he died, he died to sin once: but in that he liveth, he liveth to God.
Maana kwa habari ya kifo alichokufa kwa dhambi, alikufa mara moja kwa ajili ya wote. Hata hivyo, maisha anayoishi, anaishi kwa ajili ya Mungu.
11 Likewise reckon ye also yourselves to be dead indeed to sin, but alive to God through Jesus Christ our Lord.
Kwa njia iyo hiyo, nanyi pia mnapaswa kujihesabu kuwa wafu katika dhambi, bali hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
12 Let not sin therefore reign in your mortal body, that ye should obey it in its lusts.
Kwa sababu hiyo usiruhusu dhambi itawale mwili wako ili kusudi uweze kuzitii tamaa zake.
13 Neither yield ye your members as instruments of unrighteousness to sin: but yield yourselves to God, as those that are alive from the dead, and your members as instruments of righteousness to God.
Usitoe sehemu za mwili wako katika dhambi kama vyombo visivyo na haki, bali jitoeni wenyewe kwa Mungu, kama walio hai kutoka mautini. Na zitoeni sehemu za miili yenu kama vyombo vya haki kwa Mungu.
14 For sin shall not have dominion over you: for ye are not under the law, but under grace.
Msiiruhusu dhambi iwatawale. Kwa kuwa hamko chini ya sheria, bali chini ya neema.
15 What then? shall we sin, because we are not under the law, but under grace? By no means.
Nini basi? Tutende dhambi kwa kuwa hatupo chini ya sheria, bali chini ya neema? La hasha.
16 Know ye not, that to whom ye yield yourselves servants in obedience, his servants ye are whom ye obey; whether of sin to death, or of obedience to righteousness?
Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa wenyewe kama watumishi ndiye ambaye ninyi mnakuwa watumishi wake, yeye mnayepaswa kumtii? Hii ni kweli hata kama ninyi ni watumwa katika dhambi ambayo inapelekea mauti, au watumwa wa utii unaopelekea haki.
17 But God be thanked, that ye were the servants of sin, but ye have obeyed from the heart that form of doctrine which was delivered to you.
Lakini ashukuriwe Mungu! Kwa kuwa mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mmetii kutoka moyoni ile namna ya fundisho mliopewa.
18 Being then made free from sin, ye became the servants of righteousness.
Mmefanywa huru kutoka kwenye dhambi, na mmefanywa watumwa wa haki.
19 I speak after the manner of men because of the infirmity of your flesh: for as ye have yielded your members servants to uncleanness and to iniquity to work iniquity; even so now yield your members servants to righteousness to work holiness.
Ninazungumza kama mtu kwa sababu ya madhaifu ya miili yenu. Kwa maana kama vile mlivyotoa viungo vya miili yenu kuwa watumwa kwa uchafu na uovu, kwa jinsi iyo hiyo, sasa toeni viungo vya miili yenu kuwa watumwa wa haki kwa utakaso.
20 For when ye were the servants of sin, ye were free from righteousness.
Kwa kuwa mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki.
21 What fruit had ye then in those things of which ye are now ashamed? for the end of those things is death.
Kwa wakati huo, mlikuwa na tunda lipi kwa mambo ambayo kwa sasa mnaona aibu kwayo? Kwa kuwa matokeo ya mambo hayo ni kifo.
22 But now being made free from sin, and having become servants to God, ye have your fruit to holiness, and the end everlasting life. (aiōnios )
Lakini kwa kuwa sasa mmefanywa huru mbali na dhambi na mmefanyika watumwa kwa Mungu, mna tunda kwa ajili ya utakaso. Tokeo ni uzima wa milele. (aiōnios )
23 For the wages of sin is death; but the gift of God is eternal life through Jesus Christ our Lord. (aiōnios )
Kwa kuwa mshahara wa dhambi ni mauti, bali zawadi ya bure ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios )