< Psalms 57 >
1 To the chief Musician, Altaschith, Michtam of David, when he fled from Saul in the cave. Be merciful to me, O God, be merciful to me: for my soul trusteth in thee: yea, in the shadow of thy wings will I make my refuge, until these calamities are past by.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Usiharibu!” Utenzi wa Daudi. Baada ya kumponyoka Sauli pangoni. Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia mpaka maafa yapite.
2 I will cry to God most high; to God that performeth all things for me.
Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, Mungu atimizaye makusudi yake kwangu.
3 He shall send from heaven, and save me from the reproach of him that would swallow me up. (Selah) God shall send forth his mercy and his truth.
Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake.
4 My soul is among lions: and I lie even among them that are set on fire, even the sons of men, whose teeth are spears and arrows, and their tongue a sharp sword.
Niko katikati ya simba, nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, ambao ndimi zao ni panga kali.
5 Be thou exalted, O God, above the heavens; let thy glory be above all the earth.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 They have prepared a net for my steps; my soul is bowed down: they have dug a pit before me, into the midst of which they have fallen themselves. (Selah)
Waliitegea miguu yangu nyavu, nikainamishwa chini na dhiki. Wamechimba shimo katika njia yangu, lakini wametumbukia humo wao wenyewe.
7 My heart is fixed, O God, my heart is fixed: I will sing and give praise.
Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
8 Awake, my glory; awake, psaltery and harp: I myself will awake early.
Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
9 I will praise thee, O Lord, among the people: I will sing to thee among the nations.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
10 For thy mercy is great to the heavens, and thy truth to the clouds.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, uaminifu wako unazifikia anga.
11 Be thou exalted, O God, above the heavens: let thy glory be above all the earth.
Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, utukufu wako na uwe duniani pote.