< Matthew 26 >

1 And it came to pass, when Jesus had finished all these sayings, he said to his disciples,
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
2 Ye know that after two days is the passover, and the Son of man is betrayed to be crucified.
“Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe.”
3 Then assembled the chief priests, and the scribes, and the elders of the people, in the palace of the high priest, who was called Caiaphas,
Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
4 And consulted that they might take Jesus by guile, and kill him.
Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
5 But they said, Not on the feast day, lest there be an uproar among the people.
Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
6 Now when Jesus was in Bethany, in the house of Simon the leper,
Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
7 There came to him a woman having an alabaster box of very precious ointment, and poured it on his head, as he was eating.
mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
8 But when his disciples saw it, they had indignation, saying, To what purpose is this waste?
Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Ya nini hasara hii?
9 For this ointment might have been sold for much, and given to the poor.
Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha.”
10 When Jesus understood it, he said to them, Why trouble ye the woman? for she hath wrought a good work upon me.
Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
11 For ye have the poor always with you; but me ye have not always.
Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
12 For in that she hath poured this ointment on my body, she did it for my burial.
Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
13 Verily I say to you, Wherever this gospel shall be preached in the whole world, there shall also this, what this woman hath done, be told for a memorial of her.
Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye.”
14 Then one of the twelve, called Judas Iscariot, went to the chief priests,
Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
15 And said, What will ye give me, and I will deliver him to you? And they agreed with him for thirty pieces of silver.
akawaambia, “Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?” Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
16 And from that time he sought opportunity to betray him.
na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
17 Now the first day of the feast of unleavened bread the disciples came to Jesus, saying to him, Where wilt thou that we prepare for thee to eat the passover?
Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, “Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?”
18 And he said, Go into the city to such a man, and say to him, The Master saith, My time is at hand; I will keep the passover at thy house with my disciples.
Yeye akawajibu, “Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu.”
19 And the disciples did as Jesus had appointed them; and they made ready the passover.
Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
20 Now when the evening was come, he sat down with the twelve.
Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
21 And as they were eating, he said, Verily I say to you, that one of you shall betray me.
Walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti.”
22 And they were exceeding sorrowful, and began every one of them to say to him, Lord, is it I?
Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, “Bwana! Je, ni mimi?”
23 And he answered and said, He that dippeth his hand with me in the dish, the same shall betray me.
Yesu akajibu, “Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
24 The Son of man goeth as it is written concerning him: but woe to that man by whom the Son of man is betrayed! it had been good for that man if he had not been born.
Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa.”
25 Then Judas, who betrayed him, answered and said, Master, is it I? He said to him, Thou hast said.
Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, “Mwalimu! Je, ni mimi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
26 And as they were eating, Jesus took bread, and blessed it, and broke it, and gave it to the disciples, and said, Take, eat; this is my body.
Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni mle; huu ni mwili wangu.”
27 And he took the cup, and gave thanks, and gave it to them, saying, Drink ye all of it;
Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, “Nyweni nyote;
28 For this is my blood of the new testament, which is shed for many for the remission of sins.
maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
29 But I say to you, I will not drink henceforth of this fruit of the vine, until that day when I drink it new with you in my Father’s kingdom.
Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30 And when they had sung an hymn, they went out to the mount of Olives.
Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
31 Then saith Jesus to them, All ye shall be offended because of me this night: for it is written, I will smite the shepherd, and the sheep of the flock shall be scattered abroad.
Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
32 But after I am risen again, I will go before you into Galilee.
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya.”
33 Peter answered and said to him, Though all men shall be offended because of thee, yet will I never be offended.
Petro akamwambia Yesu “Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe.”
34 Jesus said to him, Verily I say to thee, That this night, before the cock shall crow, thou shalt deny me three times.
Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 Peter said to him, Though I should die with thee, yet will I not deny thee. Likewise also said all the disciples.
Petro akamwambia, “Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 Then cometh Jesus with them to a place called Gethsemane, and saith to the disciples, Sit ye here, while I go yonder, and pray.
Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali.”
37 And he took with him Peter and the two sons of Zebedee, and began to be sorrowful and very heavy.
Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
38 Then saith he to them, My soul is exceeding sorrowful, even to death: tarry ye here, and watch with me.
Hapo akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.”
39 And he went a little further, and fell on his face, and prayed, saying, O my Father, if it is possible, let this cup pass from me: nevertheless not as I will, but as thou wilt.
Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: “Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe.”
40 And he cometh to the disciples, and findeth them asleep, and saith to Peter, What, could ye not watch with me one hour?
Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
41 Watch and pray, that ye enter not into temptation: the spirit indeed is willing, but the flesh is weak.
Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu.”
42 He went away again the second time, and prayed, saying, O my Father, if this cup may not pass away from me, except I drink it, thy will be done.
Akaenda tena mara ya pili akasali: “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike.”
43 And he came and found them asleep again: for their eyes were heavy.
Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
44 And he left them, and went away again, and prayed the third time, saying the same words.
Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
45 Then he cometh to his disciples, and saith to them, Sleep on now, and take your rest: behold, the hour is at hand, and the Son of man is betrayed into the hands of sinners.
Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, “Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
46 Rise, let us be going: behold, he is at hand that doth betray me.
Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti.”
47 And while he was yet speaking, lo, Judas, one of the twelve, came, and with him a great multitude with swords and staffs, from the chief priests and elders of the people.
Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
48 Now he that betrayed him gave them a sign, saying, Whomever I shall kiss, that same is he: hold him fast.
Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: “Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni.”
49 And immediately he came to Jesus, and said, Hail, master; and kissed him.
Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, “Shikamoo, Mwalimu!” Kisha akambusu.
50 And Jesus said to him, Friend, why art thou come? Then they came, and laid hands on Jesus, and took him.
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya ulichokuja kufanya.” Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
51 And, behold, one of them who were with Jesus stretched out his hand, and drew his sword, and struck a servant of the high priest’s, and smote off his ear.
Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52 Then said Jesus to him, Put up again thy sword into its place: for all they that take the sword shall perish by the sword.
Hapo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
53 Thinkest thou that I cannot now pray to my Father, and he shall presently give me more than twelve legions of angels?
Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 But how then shall the scriptures be fulfilled, that thus it must be?
Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?”
55 In that same hour said Jesus to the multitudes, Are ye come out as against a thief with swords and staffs to take me? I sat daily with you teaching in the temple, and ye laid no hold on me.
Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, “Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
56 But all this was done, that the scriptures of the prophets might be fulfilled. Then all the disciples forsook him, and fled.
Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie.” Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
57 And they that had laid hold on Jesus led him away to Caiaphas the high priest, where the scribes and the elders were assembled.
Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
58 But Peter followed him from afar off to the high priest’s courtyard, and went in, and sat with the servants, to see the end.
Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
59 Now the chief priests, and elders, and all the council, sought false testimony against Jesus, to put him to death;
Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
60 But found none: and, though many false witnesses came, yet found they none. At the last came two false witnesses,
lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
61 And said, This man said, I am able to destroy the temple of God, and to build it in three days.
wakasema, “Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.”
62 And the high priest arose, and said to him, Answerest thou nothing? what is it which these testify against thee?
Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, “Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
63 But Jesus held his peace. And the high priest answered and said to him, I adjure thee by the living God, that thou tell us whether thou art the Christ, the Son of God.
Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!”
64 Jesus saith to him, Thou hast said: nevertheless I say to you, After this shall ye see the Son of man sitting on the right hand of power, and coming in the clouds of heaven.
Yesu akamwambia, “Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 Then the high priest tore his clothes, saying, He hath spoken blasphemy; what further need have we of witnesses? behold, now ye have heard his blasphemy.
Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
66 What think ye? They answered and said, He is guilty of death.
Ninyi mwaonaje?” Wao wakamjibu, “Anastahili kufa!”
67 Then they spat in his face, and buffeted him; and others smote him with the palms of their hands,
Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
68 Saying, Prophesy to us, thou Christ, Who is he that smote thee?
wakasema, “Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!”
69 Now Peter sat outside in the courtyard: and a maid came to him, saying, Thou also wast with Jesus of Galilee.
Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, “Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70 But he denied before them all, saying, I know not what thou sayest.
Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”
71 And when he had gone out into the porch, another maid saw him, and said to them that were there, This man was also with Jesus of Nazareth.
Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
72 And again he denied with an oath, I do not know the man.
Petro akakana tena kwa kiapo: “Simjui mtu huyo.”
73 And after a while came to him they that stood by, and said to Peter, Surely thou also art one of them; for thy speech betrayeth thee.
Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha.”
74 Then began he to curse and to swear, saying, I know not the man. And immediately the cock crowed.
Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, “Simjui mtu huyo!” Mara jogoo akawika.
75 And Peter remembered the word of Jesus, who said to him, Before the cock shall crow, thou shalt deny me three times. And he went out, and wept bitterly.
Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Basi, akatoka nje akalia sana.

< Matthew 26 >