< 1 Samuel 24 >
1 And it came to pass, when Saul had returned from following the Philistines, that it was told to him, saying, Behold, David is in the wilderness of Engedi.
Baada ya Sauli kurudi kuwafuatia Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika Jangwa la En-Gedi.”
2 Then Saul took three thousand chosen men out of all Israel, and went to seek David and his men upon the rocks of the wild goats.
Basi Sauli akachukua watu hodari 3,000 kutoka Israeli yote kwenda kumsaka Daudi na watu wake karibu na Majabali ya Mbuzi-Mwitu.
3 And he came to the sheepfolds by the way, where was a cave; and Saul went in to cover his feet: and David and his men remained in the sides of the cave.
Akaja mpaka kwenye mazizi ya kondoo kando ya njia, hapo palikuwa na pango, na Sauli akaingia ndani kujipumzisha. Daudi na watu wake walikuwa wamo mle pangoni kwa ndani zaidi.
4 And the men of David said to him, Behold the day of which the LORD said to thee, Behold, I will deliver thy enemy into thy hand, that thou mayest do to him as it shall seem good to thee. Then David arose, and secretly cut off the skirt of Saul’s robe.
Watu wa Daudi wakasema, “Hii ndiyo siku aliyonena Bwana akikuambia, ‘Nitamtia adui yako mikononi mwako ili wewe umtendee utakavyo.’” Basi Daudi akanyemelea bila kuonekana na kukata upindo wa joho la Sauli.
5 And it came to pass afterward, that David’s heart smote him, because he had cut off Saul’s skirt.
Baada ya hilo, dhamiri ya Daudi ikataabika kwa kukata upindo wa joho la Sauli.
6 And he said to his men, The LORD forbid that I should do this thing to my master, the LORD’S anointed, to stretch forth my hand against him, seeing he is the anointed of the LORD.
Akawaambia watu wake, “Bwana na apishie mbali nisije nikafanya jambo kama hilo kwa bwana wangu, yeye ambaye ni mpakwa mafuta wa Bwana, au kuinua mkono wangu dhidi yake; kwani yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.”
7 So David restrained his servants with these words, and permitted them not to rise against Saul. But Saul rose out of the cave, and went on his way.
Kwa maneno haya Daudi akawaonya watu wake na hakuwaruhusu wamshambulie Sauli. Naye Sauli akaondoka pangoni na kwenda zake.
8 David also rose afterward, and went out of the cave, and cried after Saul, saying, My lord the king. And when Saul looked behind him, David stooped with his face to the earth, and bowed himself.
Ndipo Daudi naye akatoka pangoni na kumwita Sauli akisema, “Mfalme, bwana wangu!” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akainama na kusujudu uso wake mpaka nchi.
9 And David said to Saul, Why hearest thou men’s words, saying, Behold, David seeketh thy harm?
Akamwambia Sauli, “Kwa nini unasikiliza wakati watu wanapokuambia, ‘Daudi amenuia kukudhuru’?
10 Behold, this day thy eyes have seen how the LORD hath delivered thee to day into my hand in the cave: and some bade me kill thee: but my eye spared thee; and I said, I will not put forth my hand against my lord; for he is the LORD’S anointed.
Leo umeona kwa macho yako mwenyewe jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu huko pangoni. Watu wengine walisisitiza nikuue, lakini nilikuacha, nikisema, ‘Sitainua mkono wangu dhidi ya bwana wangu, kwa sababu yeye ni mpakwa mafuta wa Bwana.’
11 Moreover, my father, see, yea, see the skirt of thy robe in my hand: for in that I cut off the skirt of thy robe, and killed thee not, know thou and see that there is neither evil nor transgression in my hand, and I have not sinned against thee; yet thou huntest my soul to take it.
Tazama, baba yangu, ona kipande hiki cha joho lako mkononi mwangu! Nilikata upindo wa joho lako lakini sikukuua. Basi ujue na kutambua kuwa sina hatia ya kutenda mabaya wala ya kuasi. Wewe sijakukosea, lakini wewe unaniwinda mimi ili kuuondoa uhai wangu.
12 The LORD judge between me and thee, and the LORD avenge me of thee: but my hand shall not be upon thee.
Bwana na ahukumu kati yangu na wewe. Naye Bwana alipize mabaya unayonitendea, lakini mkono wangu hautakugusa.
13 As saith the proverb of the ancients, Wickedness proceedeth from the wicked: but my hand shall not be upon thee.
Kama msemo wa kale usemavyo, ‘Kutoka kwa watenda maovu hutoka matendo maovu,’ kwa hiyo mkono wangu hautakugusa wewe.
14 After whom is the king of Israel come out? after whom dost thou pursue? after a dead dog, after a flea.
“Je, mfalme wa Israeli ametoka dhidi ya nani? Ni nani unayemfuatia? Je, ni mbwa mfu? Ni kiroboto?
15 The LORD therefore be judge, and judge between me and thee, and see, and plead my cause, and deliver me out of thy hand.
Bwana na awe mwamuzi wetu, yeye na aamue kati yetu. Yeye na anitetee shauri langu; anihesabie haki kwa kuniokoa mkononi mwako.”
16 And it came to pass, when David had finished speaking these words to Saul, that Saul said, Is this thy voice, my son David? And Saul lifted up his voice, and wept.
Daudi alipomaliza kusema haya, Sauli akamuuliza, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Ndipo Sauli akalia kwa sauti kuu, akisema,
17 And he said to David, Thou art more righteous than I: for thou hast rewarded me with good, though I have rewarded thee with evil.
“Wewe ni mwenye haki kuliko mimi; umenitendea mema, lakini mimi nimekutendea mabaya.
18 And thou hast showed this day how thou hast dealt with me: forasmuch as when the LORD had delivered me into thy hand, thou didst not kill me.
Sasa umeniambia juu ya mema uliyonitendea. Bwana alinitia mikononi mwako, lakini wewe hukuniua.
19 For if a man findeth his enemy, will he let him go away well? therefore the LORD reward thee with good for what thou hast done to me this day.
Je, mtu ampatapo adui yake, humwacha aende zake bila kumdhuru? Bwana na akulipe mema kwa jinsi ulivyonitenda leo.
20 And now, behold, I know well that thou shalt surely be king, and that the kingdom of Israel shall be established in thy hand.
Ninajua kwamba hakika utakuwa mfalme na ya kwamba ufalme wa Israeli utakuwa imara mikononi mwako.
21 Swear now therefore to me by the LORD, that thou wilt not cut off my seed after me, and that thou wilt not destroy my name out of my father’s house.
Sasa niapie kwa Bwana kwamba hutakatilia mbali uzao wangu wala kulifuta jina langu kutoka jamaa ya baba yangu.”
22 And David swore to Saul. And Saul went home; but David and his men went up to the strong hold.
Basi Daudi akamwapia Sauli. Kisha Sauli akarudi zake nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.