< Psalms 1 >

1 Blessed is the man who does not walk in the advice of the wicked, or stand in the pathway with sinners, or sit in the assembly of mockers.
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 But his delight is in the law of Yahweh, and on his law he meditates day and night.
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 He will be like a tree planted by the streams of water that produces its fruit in its season, whose leaves do not wither; whatever he does will prosper.
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 The wicked are not so, but are instead like the chaff that the wind drives away.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 So the wicked will not stand in the judgment, nor sinners in the assembly of the righteous.
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For Yahweh approves of the way of the righteous, but the way of the wicked will perish.
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< Psalms 1 >