< Psalms 81 >

1 For the chief musician; set to the Gittith style. A psalm of Asaph. Sing aloud to God our strength; shout out for joy to the God of Jacob.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Sing a song and play the tambourine, the pleasant lyre with the harp.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Blow the trumpet on the day of the new moon, on the day of the full moon, when our feast day begins.
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 For it is a statute for Israel, a decree given by the God of Jacob.
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 He issued it as a regulation in Joseph when he went against the land of Egypt, where I heard a voice that I did not recognize:
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 “I removed the burden from his shoulder; his hands were freed from holding the basket.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 In your distress you called out, and I helped you; I answered you from a dark thundercloud. I tested you at the waters of Meribah. (Selah)
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Listen, my people, for I will warn you, Israel, if you would only listen to me!
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 There must be no foreign god among you; you must not worship any foreign god.
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 I am Yahweh your God, who brought you out of the land of Egypt. Open your mouth wide, and I will fill it.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 But my people did not listen to my words; Israel did not obey me.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 So I gave them over to their own stubborn way so that they might do what seemed right to them.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 Oh, that my people would listen to me; oh, that my people would walk in my paths.
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 Then I would quickly subdue their enemies and turn my hand against their oppressors.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 May those who hate Yahweh cringe in fear before him! May they be humiliated forever.
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 I would feed Israel with the finest wheat; I would satisfy you with honey out of the rock.”
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”

< Psalms 81 >