< Psalms 53 >
1 For the chief musician; set to Mahalath. A maschil of David. A fool says in his heart, “There is no God.” They are corrupt and have done abominable iniquity; there is no one who does good.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi. Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, hakuna hata mmoja atendaye mema.
2 God looks down from heaven on the children of mankind to see if there are any who understand, who seek after him.
Mungu anawachungulia wanadamu chini kutoka mbinguni aone kama wako wenye akili, wowote wanaomtafuta Mungu.
3 They have all turned away. Together they have become corrupt. There is not one who does good, not even one.
Kila mmoja amegeukia mbali, wameharibika wote pamoja, hakuna atendaye mema. Naam, hakuna hata mmoja!
4 Do those who commit iniquity have no understanding— those who devour my people as if they were eating bread and they do not call on God?
Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Mungu?
5 They were in great fear, although no reason to fear was there; for God will scatter the bones of whoever will camp against you; such people will be put to shame because God has rejected them.
Hapo waliingiwa na hofu kuu, ambapo hapakuwa cha kutetemesha. Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia; uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.
6 Oh, that the salvation of Israel would come from Zion! When God brings back his people from the captivity, then Jacob will rejoice and Israel will be glad!
Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!