< Psalms 50 >

1 A psalm of Asaph. The Mighty One, God, Yahweh, has spoken and called the earth from the rising of the sun to its setting.
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 Out of Zion, the perfection of beauty, God has shone.
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Our God comes and does not stay silent; a fire devours before him, and it is very stormy around him.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 He calls to the heavens above and to the earth so that he may judge his people:
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 “Gather my faithful ones together to me, those who have made a covenant with me by sacrifice.”
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 The heavens will declare his righteousness, for God himself is judge. (Selah)
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 “Hear, my people, and I will speak; I am God, your God.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 I will not reprove you for your sacrifices; your burnt offerings are always before me.
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 I will take no bull out of your house, or male goats out of your folds.
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 For every beast of the forest is mine, and the cattle on a thousand hills.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 I know all the birds of the mountains, and the wild beasts of the field are mine.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 If I were hungry, I would not tell you; for the world is mine, and everything in it.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 Will I eat the flesh of bulls or drink the blood of goats?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Offer to God the sacrifice of thanksgiving, and pay your vows to the Most High.
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 Call on me in the day of trouble; I will rescue you, and you will glorify me.”
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 But to the wicked God says, “What have you to do with declaring my statutes, that you have taken my covenant in your mouth,
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 since you hate instruction and throw my words away?
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 When you see a thief, you agree with him; you participate with those who commit adultery.
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 You give your mouth to evil, and your tongue expresses deceit.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 You sit and speak against your brother; you slander your own mother's son.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 You have done these things, but I have kept silent, so you thought that I was someone just like yourself. But I will reprove you and bring up, right before your eyes, all the things you have done.
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 Give this careful consideration, you who forget God, otherwise I will tear you to pieces, and there will be no one to come to help you!
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 The one who offers a sacrifice of thanksgiving praises me, and to anyone who plans his path in the right way I will show God's salvation.”
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”

< Psalms 50 >