< Psalms 49 >
1 For the chief musician. A psalm of the sons of Korah. Hear this, all you peoples; give ear, all you inhabitants of the world,
Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
2 both low and high, rich and poor together.
wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
3 My mouth will speak wisdom and the meditation of my heart will be of understanding.
Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
4 I will incline my ear to a parable; I will begin my parable with the harp.
Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
5 Why should I fear the days of evil, when iniquity surrounds me at my heels?
Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
6 Why should I fear those who trust in their wealth and boast about the amount of their riches?
Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
7 It is certain that no one can redeem his brother or give God a ransom for him,
Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
8 For the redemption of one's life is costly, and no one can pay what we owe.
Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
9 No one can live forever so that his body should not decay.
Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
10 For he will see decay. Wise men die; the fool and the brute alike perish and leave their wealth to others.
Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
11 Their inner thought is that their families will continue forever, and the places where they live, to all generations; they call their lands after their own names.
Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
12 But man, having wealth, does not remain alive; he is like the beasts that perish.
Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
13 This, their way, is their folly; yet after them, men approve of their sayings. (Selah)
Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
14 Like sheep they are appointed for Sheol, and death will be their shepherd. The upright will rule over them in the morning, and their bodies will be consumed in Sheol, with no place for them to live. (Sheol )
Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol )
15 But God will redeem my life from the power of Sheol; he will receive me. (Selah) (Sheol )
Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol )
16 Do not be afraid when one becomes rich, and the glory of his house increases.
Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
17 For when he dies he will take nothing away; his glory will not go down after him.
Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
18 He blessed his soul while he lived— and men praise you when you live for yourself—
Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
19 he will go to the generation of his fathers and they will never see the light again.
naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
20 One who has wealth but no understanding is like the beasts, which perish.
Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.