< Psalms 48 >

1 A song; a psalm of the sons of Korah. Great is Yahweh and greatly to be praised, in the city of our God on his holy mountain.
Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
2 Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, is Mount Zion, on the sides of the north, the city of the great King.
Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
3 God has made himself known in her palaces as a refuge.
Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
4 For, see, the kings assembled themselves; they passed by together.
Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
5 They saw it, then they were amazed; they were dismayed, and they hurried away.
Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
6 Trembling took hold of them there, pain as when a woman is in labor.
Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
7 With the east wind you break the ships of Tarshish.
Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
8 As we have heard, so have we seen in the city of Yahweh of hosts, in the city of our God; God will establish it forever. (Selah)
Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
9 We have thought about your covenant faithfulness, God, in the middle of your temple.
Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
10 As your name is, God, so is your praise to the ends of the earth; your right hand is full of righteousness.
Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
11 Let Mount Zion be glad, let the daughters of Judah rejoice because of your righteous decrees.
Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
12 Walk around Mount Zion, go round about her; count her towers,
Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
13 notice well her walls, and look at her palaces so that you may tell it to the next generation.
mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
14 For this God is our God forever and ever; he will be our guide to death.
Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.

< Psalms 48 >