< Psalms 42 >
1 For the chief musician. A maschil of the sons of Korah. As the deer pants after streams of water, so I thirst for you, God.
Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
2 I thirst for God, for the living God, when will I come and appear before God?
Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
3 My tears have been my food day and night, while my enemies are always saying to me, “Where is your God?”
Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
4 These things I call to mind as I pour out my soul: how I went with the throng and led them to the house of God with the voice of joy and praise, a multitude celebrating a festival.
Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
5 Why are you bowed down, my soul? Why are you upset within me? Hope in God, for again I will praise him who is my salvation.
Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
6 My God, my soul is bowed down within me, therefore I call you to mind from the land of the Jordan, from the three peaks of Mount Hermon, and from the hill of Mizar.
Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
7 Deep calls to deep at the noise of your waterfalls; all your waves and your billows have gone over me.
Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
8 Yet Yahweh will command his covenant faithfulness in the daytime; in the night his song will be with me, a prayer to the God of my life.
Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
9 I will say to God, my rock, “Why have you forgotten me? Why do I go mourning because of the oppression of the enemy?”
Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
10 As with a sword in my bones, my adversaries rebuke me, while they always say to me, “Where is your God?”
Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
11 Why are you bowed down, my soul? Why are you upset within me? Hope in God, for again I will praise him who is my salvation and my God.
Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.