< Psalms 38 >

1 A psalm of David, to bring to remembrance. Yahweh, do not rebuke me in your anger; do not punish me in your wrath.
Zaburi ya Daudi. Maombi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.
2 For your arrows pierce me, and your hand presses me down.
Kwa kuwa mishale yako imenichoma, na mkono wako umenishukia.
3 My whole body is sick because of your anger; there is no health in my bones because of my sin.
Hakuna afya mwilini mwangu kwa sababu ya ghadhabu yako, mifupa yangu haina uzima kwa sababu ya dhambi zangu.
4 For my iniquities overwhelm me; they are a burden too heavy for me.
Maovu yangu yamenifunika kama mzigo usiochukulika.
5 My wounds are infected and smell because of my foolish sins.
Majeraha yangu yameoza na yananuka, kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6 I am stooped over and humiliated every day; I go about mourning all day long.
Nimeinamishwa chini na kushushwa sana, mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.
7 For within me, I am filled with burning; there is no health in my flesh.
Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo, hakuna afya mwilini mwangu.
8 I am numb and utterly crushed; I groan because of the anguish of my heart.
Nimedhoofika na kupondwa kabisa, nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.
9 Lord, you understand my heart's deepest yearnings, and my groanings are not hidden from you.
Ee Bwana, yote ninayoyaonea shauku yako wazi mbele zako, kutamani kwangu sana hakufichiki mbele zako.
10 My heart pounds, my strength fades, and my eyesight dims.
Moyo wangu unapigapiga, nguvu zangu zimeniishia; hata macho yangu yametiwa giza.
11 My friends and companions shun me because of my condition; my neighbors stand far off.
Rafiki na wenzangu wananikwepa kwa sababu ya majeraha yangu; majirani zangu wanakaa mbali nami.
12 Those who seek my life lay snares for me. They who seek my harm speak destructive words and say deceitful words all day long.
Wale wanaotafuta uhai wangu wanatega mitego yao, wale ambao wangetaka kunidhuru huongea juu ya maangamizi yangu; hufanya shauri la hila mchana kutwa.
13 But I, I am like a deaf man and hear nothing; I am like a mute man who says nothing.
Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia, ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,
14 I am like a man who does not hear and who has no reply.
nimekuwa kama mtu asiyesikia, ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.
15 Surely I wait for you, Yahweh; you will answer, Lord my God.
Ee Bwana, ninakungojea wewe, Ee Bwana Mungu wangu, utajibu.
16 I say this so that my enemies will not gloat over me. If my foot slips, they will do terrible things to me.
Kwa kuwa nilisema, “Usiwaache wafurahie, wala wasijitukuze juu yangu mguu wangu unapoteleza.”
17 For I am about to stumble, and I am in constant pain.
Kwa maana ninakaribia kuanguka, na maumivu yangu yananiandama siku zote.
18 I confess my guilt; I am concerned about my sin.
Naungama uovu wangu, ninataabishwa na dhambi yangu.
19 But my enemies are numerous; those who hate me wrongfully are many.
Wengi ni wale ambao ni adui zangu hodari, wale wanaonichukia bila sababu ni wengi.
20 They repay me evil for good; they hurl accusations at me although I have pursued what is good.
Wanaolipa maovu kwa wema wangu hunisingizia ninapofuata lililo jema.
21 Do not abandon me, Yahweh; my God, do not stay far away from me.
Ee Bwana, usiniache, usiwe mbali nami, Ee Mungu wangu.
22 Come quickly to help me, Lord, my salvation.
Ee Bwana Mwokozi wangu, uje upesi kunisaidia.

< Psalms 38 >