< Psalms 28 >

1 A psalm of David. To you, Yahweh, I cry out; my rock, do not ignore me. If you do not respond to me, I will join those who go down to the grave.
Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
2 Hear the sound of my pleading when I call for help from you, when I lift up my hands toward your most holy place!
Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
3 Do not drag me away with the wicked, those who do iniquity, who speak peace with their neighbors but have evil in their hearts.
Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
4 Give them what their deeds deserve and repay them what their wickedness demands, repay them for the work of their hands and render to them their due.
Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
5 Because they do not understand the deeds of Yahweh or the work of his hands, he will tear them down and never rebuild them.
Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
6 Blessed be Yahweh because he has heard the sound of my pleading!
Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
7 Yahweh is my strength and my shield; my heart trusts in him, and I am helped. Therefore my heart greatly rejoices, and I will praise him with singing.
Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
8 Yahweh is the strength of his people, and he is the saving refuge of his anointed one.
Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9 Save your people and bless your inheritance. Be their shepherd and carry them forever.
Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

< Psalms 28 >