< Psalms 141 >

1 A psalm of David. Yahweh, I am crying out to you; come quickly to me. Listen to me when I call to you.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
2 May my prayer be like incense before you; may my lifted hands be like the evening sacrifice.
Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
3 Yahweh, place a guard over my mouth; guard the door of my lips.
Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
4 Do not let my heart desire any evil thing or participate in sinful activities with men who behave wickedly. May I not eat any of their delicacies.
Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
5 Let a righteous man hit me; it will be a kindness to me. Let him correct me; it will be like oil on my head; may my head not refuse to accept it. But my prayer is always against their wicked deeds.
Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
6 Their leaders will be thrown down from the top of cliffs; they will hear that my own words are pleasant.
watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
7 They will have to say, “As when one plows and breaks up the ground, so our bones have been scattered at the mouth of Sheol.” (Sheol h7585)
Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
8 Surely my eyes are on you, Yahweh, Lord; in you I take refuge; do not leave my soul defenseless.
Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
9 Protect me from the snares that they have laid for me, from the traps of evildoers.
Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
10 Let the wicked fall into their own nets while I escape.
Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.

< Psalms 141 >