< Psalms 138 >
1 A psalm of David. I will give you thanks with my whole heart; before the gods I will sing praises to you.
Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
2 I will bow down toward your holy temple and give thanks to your name for your covenant faithfulness and for your trustworthiness. You have made your word and your name more important than anything else.
Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
3 On the day that I called you, you answered me; you made me bold and strengthened my soul.
Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
4 All the kings of the earth will give you thanks, Yahweh, for they will hear the words from your mouth.
Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
5 Indeed, they will sing of the deeds of Yahweh, for great is the glory of Yahweh.
Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
6 For though Yahweh is high, yet he cares for the lowly, but the proud he knows from far off.
Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
7 Though I walk in the middle of danger, you will preserve my life; you will reach out with your hand against the anger of my enemies, and your right hand will save me.
Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
8 Yahweh is with me to the end; your covenant faithfulness, Yahweh, endures forever. Do not forsake the ones whom your hands have made.
Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.