< Psalms 108 >

1 A song, a psalm of David. My heart is fixed, God; I will sing, yes, I will sing praises also with my honored heart.
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 Wake up, lute and harp; I will wake up the dawn.
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 I will give thanks to you, Yahweh, among the peoples; I will sing praises to you among the nations.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 For your covenant faithfulness is great above the heavens; and your trustworthiness reaches to the skies.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 Be exalted, God, above the heavens, and may your glory be exalted over all the earth.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 So that those you love may be rescued, rescue us with your right hand and answer me.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 God has spoken in his holiness; “I will rejoice; I will divide Shechem and apportion out the Valley of Succoth.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Gilead is mine, and Manasseh is mine; Ephraim also is my helmet; Judah is my scepter.
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 Moab is my washbasin; over Edom I will throw my shoe; I will shout in triumph because of Philistia.
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 Who will bring me into the strong city? Who will lead me to Edom?”
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 God, have you not rejected us? You do not go into battle with our army.
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Give us help against the enemy, for man's help is futile.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 We will triumph with God's help; he will trample down our enemies.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Psalms 108 >