< Proverbs 9 >

1 Wisdom has built her own house; she has carved seven pillars out of rocks.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 She has slaughtered her animals; she has mixed her wine; and she has set her table.
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 She has sent out her maids; she calls out from the highest points of the city,
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 “Who is naive? Let him turn aside here!” To the one lacking good sense she speaks.
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 “Come, eat my food, and drink the wine I have mixed.
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 Leave your naive actions and live; walk in the path of understanding.
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 Whoever disciplines a mocker receives abuse, and whoever rebukes a wicked person receives insults.
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 Do not reprove a mocker, or he will hate you; reprove a wise man, and he will love you.
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 Give to a wise person, and he will become even wiser; teach a righteous person, and he will add to his learning.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 The fear of Yahweh is the beginning of wisdom, and the knowledge of the Holy One is understanding.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 For through me your days will be multiplied, and years of life will be added to you.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 If you are wise, you are wise for yourself, and if you mock, you will carry it by yourself.”
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 The woman of foolishness is ignorant; she is untaught and knows nothing.
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 She sits at the door of her house, on a seat in the highest places of the town.
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 She is calling out to those who pass by in the streets, to people walking straight on their way.
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 “Let anyone who is naive turn aside here,” she says to those who have no sense.
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 “Stolen waters are sweet, and bread of secrecy is delicious.”
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 But he does not know that the dead are there, that her invited guests are in the depths of Sheol. (Sheol h7585)
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbs 9 >