< Proverbs 26 >
1 Like snow in summer or rain in harvest, so a fool does not deserve honor.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 As the sparrow flitters and the swallow darts when they fly, so an undeserved curse does not alight.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 A whip is for the horse, a bridle is for the donkey and a rod is for the back of fools.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Do not answer a fool according to his folly, or you will become like him.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Answer a fool and join in on his folly, so he will not become wise in his own eyes.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 Whoever sends a message by the hand of a fool cuts off his own feet and drinks violence.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Like the legs of a paralytic which hang down is a proverb in the mouth of fools.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Like tying a stone in a sling is giving honor to a fool.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Like a thorn that goes into the hand of a drunkard is a proverb in the mouth of fools.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 Like an archer who wounds all those around him is one who hires a fool or hires anyone who passes by.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 As a dog returns to his own vomit, so is a fool who repeats his folly.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 Do you see someone who is wise in his own eyes? There is more hope for a fool than for him.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 The lazy person says, “There is a lion on the road! There is a lion between the open places!”
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 As the door turns on its hinges, so is the lazy person upon his bed.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 The lazy person puts his hand into the dish and yet he has no strength to lift it up to his mouth.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 The lazy person is wiser in his own eyes than seven men who respond with good judgment.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 Like one who takes hold of the ears of a dog, is a passerby who becomes angry at a dispute that is not his own.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Like a madman who shoots burning arrows,
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 is the one who deceives his neighbor and says, “Was I not telling a joke?”
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 For lack of wood, the fire goes out; and where there is no gossiper quarreling ceases.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 As charcoal is to burning coals and wood is to fire, so is a quarrelsome person for kindling strife.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 The words of a gossip are like delicious morsels; they go down into the inner parts of the body.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Like the glaze overlaying an earthen vessel so are burning lips and an evil heart.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 One who hates others disguises his feelings with his lips and he lays up deceit within himself.
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 He will speak graciously, but do not believe him, for there are seven abominations in his heart.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Though his hatred is covered with deception, his wickedness will be exposed in the assembly.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 Whoever digs a pit will fall into it and the stone will roll back on the one who pushed it.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 A lying tongue hates the people it crushes and a flattering mouth brings about ruin.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.