< Proverbs 11 >

1 Yahweh hates scales that are not accurate, but he delights in a precise weight.
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
2 When pride comes, then comes disgrace, but with humility comes wisdom.
Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
3 The integrity of the upright guides them, but the crooked ways of the treacherous destroy them.
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
4 Wealth is worthless on the day of wrath, but doing right keeps you from death.
Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5 The right conduct of a blameless person makes his way straight, but the wicked will fall because of their own wickedness.
Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
6 The right conduct of those who please God keeps them safe, but the treacherous are trapped by their cravings.
Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
7 When a wicked man dies, his hope perishes and the hope that was in his strength comes to nothing.
Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
8 The righteous person is kept away from trouble and it comes upon the wicked instead.
Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
9 With his mouth the godless person destroys his neighbor, but through knowledge righteous people are kept safe.
Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
10 When righteous people prosper, a city rejoices; when the wicked perish, there are shouts of joy.
Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
11 Through the good gifts of those who please God, the city becomes great; by the mouth of the wicked, the city is torn down.
Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
12 The man who has contempt for his friend has no sense, but a man of understanding keeps quiet.
Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
13 Whoever goes around slandering reveals secrets, but a faithful person keeps a matter covered.
Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
14 Where there is no wise direction, a nation falls, but victory comes by consulting many advisors.
Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
15 Whoever guarantees a loan for a stranger will surely suffer harm, but the one who hates giving a pledge in that kind of promise is safe.
Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
16 A gracious woman gets honor, but ruthless people grasp for wealth.
Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
17 A kind person benefits himself, but one who is cruel hurts himself.
Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
18 The wicked person lies to get his wages, but one who sows what is right reaps the wages of truth.
Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
19 An honest person who does what is right will live, but the one who pursues evil will die.
Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
20 Yahweh hates those whose hearts are perverse, but he delights in those whose ways are blameless.
Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
21 Be sure of this—the wicked person will not go unpunished, but the descendants of righteous people will be kept safe.
Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
22 Like a gold ring in a pig's nose is a beautiful woman without discretion.
Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
23 The desires of righteous people result in good, but wicked people can only hope for wrath.
Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
24 There is one who scatters—he will accumulate even more; another withholds what he should give—he comes to poverty.
Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
25 The generous person will prosper and the one who gives water to others will have water for himself.
Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
26 People curse the man who refuses to sell grain, but good gifts crown the head of him who sells it.
Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
27 The one who diligently seeks good is also seeking favor, but the one who searches for evil will find it.
Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
28 Those who trust in their riches will fall, but like the leaf, righteous people will flourish.
Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29 The one who brings trouble on his own household will inherit the wind and the fool will become a servant to the wise of heart.
Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
30 The righteous person will be like a tree of life, but violence takes away lives.
Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
31 Behold! The righteous person receives what he deserves; how much more the wicked and the sinner!
Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

< Proverbs 11 >